Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge kuhusu Wakala wa Kimataifa wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (International Renewable Energy Agency - IRENA) na Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika wa Mwaka 2019 (Treaty for the Establishment of the African Medicine Agency - AMA)

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia eneo hili. Wenzangu wamekwishakueleza kwamba kitu hiki kilianzishwa tangu 2009 mpaka 2011 ndipo ilipoanza kazi. Lengo kuu kabisa na malengo manne kutokana na Wizara walivyoweza kutueleza lakini mimi tataja malengo makubwa mawili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhamasisha teknolojia mbalimbali za kusaidia kuweza kupata nishati salama; la pili ni kuwezesha upatikanaji wa nishati safi na salama yenye gharama nafuu, tunajua kabisa fika kama Taifa kutegemea umeme huo mwingine ambao tunaotegemea sasa tunapitia kwenye madhira makubwa sana kutokana na tabianchi pia. Hivyo tutakapoamua kupitisha itatusaidia sana kuweza kupata umeme huu mwingine ambao tunafikiri utakuwa mzuri zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu kubwa sana sana la hii IRENA ni kujengea uwezo nchi mwanachama. Tunajua watalamu wetu watajengewa uwezo, lakini pamoja na hayo kwa jinsi ambavyo tumeelezwa na tumesoma tumeelewa tutakapojiunga kuwa wanachama ni rahisi kupata fedha kwa ajili ya kusaidia Taifa letu na kuweza kusaidia teknoloji hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, itatusaidia sana pia kupata umeme kwa urahisi zaidi ikiwemo gesi joto ambazo tayari utafiti umekwishafanywa. Na ili uweze kufanikiwa Serikali imeamua kuanza kufanya utafiti na kuweza kuelewa ni maeneo gani ambayo tunaweza tukapata nishati hii. Hilo peke yake hata wawekezaji itakuwa ni rahisi kufika kwa sababu tayari tumekwisha warahisishia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niseme kama Mjumbe wa Kamati lakini kama Mbunge mwenzenu kwamba kuna haja ya kupitisha sheria hii. Mimi siilaumu sana kwa kuchelewa kwa sababu wasi wasi ni akili. Mimi naamini muda mrefu uliyochukuliwa imetusaidia sisi kujua kwa kina, watalamu wetu kusimamia kwa kina. Kwa hiyo tusikimbie kusema tungefanya haraka hivyo walivyochelewa wamefanya vizuri na sasa ndiyo wakati sahihi wa kutoa maamuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niwapongeze Wizara mnaendelea; na kuna maeneo mengine tufanye taratibu kama nchi tukubaliane mwisho wa siku tupitishe kwa umoja. Ninaipongeza Wizara, ninampongeza Waziri husika kwa kuwa amefanya vizuri, pia hata Katibu wa Wizara amefanya kitu kizuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninaamini baada ya kupitisha IRENA tutaenda kufanikiwa kama Taifa. Wameishasema wenzangu kuna nchi ambazo zimetutangulia katika East Africa, tunafahamu Uganda na Kenya pamoja na Rwanda walishajiunga. Kwa hiyo na sisi tutakapojiunga Taifa letu linaenda kupata faida na kwa hivyo ninaunga mkono kwa mara ya kwanza mia kwa mia tuunge ajenda hii, ahsante. (Makofi)