Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami nichukue nafasi hii kukupongeza sana kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa IPU. Jana nilipokutana nawe nilikuomba nikupe mkono na ulipokubali nilisema kwamba nina bahati ya kupewa mkono na Rais wa IPU. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa namna ambavyo ana-support sekta ya michezo. Tumeshuhudia mafanikio makubwa katika Sekta hii, tume-qualify kwa mara nyingine kwenda AFCON mwakani na tumekuwa wenyeji wa AFCON 2027 na kabla ya hapo tutakuwa wenyeji wa CHAN, 2025. Haya yote ni kazi nzuri. Sisi wasaidizi wake tunahakikisha kwamba tunapambana kuiweka Sekta ya Michezo katika muktadha unaostahili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika sekta ya michezo, tuna Chuo kimoja cha Michezo kinaitwa Chuo cha Maendeleo ya Michezo cha Malya. Chuo hiki, kwa asilimia 56.8 kipo katika Mkoa wa Mwanza na asilimia 43.2 kipo katika Mkoa wa Simiyu. Katika miaka minne iliyopita Serikali na Wizara hii na hasa watangulizi wangu wamefanya kazi nzuri ya kuhakikisha wanaboresha miundombinu ya chuo hiki. Takribani shilingi bilioni nne zimewekezwa pale katika kuboresha miundombinu ya ujenzi wa hosteli, kutatua changamoto ya maji, kujenga viwanja na ukarabati wa viwanja vya ndani, kujenga jengo la utawala pamoja madarasa. Kazi yangu ni kuendeleza kazi hiyo nzuri ambayo watangulizi wangu wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpango wa Serikali ni kuendelea kuwa na center of sports excellence katika kila Mkoa wa Tanzania. Pale Malya tayari ni center of excellence na inatumika kama Center of Excellence for East Africa, hatuna mpango wa kuhamisha Chuo cha Malya.

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.
WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, hatuna mpango wa kusema tunaondoa project yoyote Malya, tutaendelea na project katika mikoa yote. Tunawaomba wenye Mikoa hiyo watupe maeneo kama ambavyo Ilemela wamatupa eneo…

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Waziri, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Kasalali Mageni.

TAARIFA

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa mzungumzaji kwamba Chuo cha Malya, hakina Center of Sports Excellence kwa sababu Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo ilisaini mkataba wa ujenzi wa kituo hicho. Kwa hiyo, hakipo na kama kingekuwepo Serikali isingesaini mkataba.

Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 22 Agosti, 2021, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akipokea timu ya under 21 ya Taifa, naomba kwa ruhusa yako nimnukuu alisema maneno yafuatayo: “tuna mpango wa kujenga akademia ya michezo kwenye Chuo cha Michezo cha Malya, Mwanza. Pia kujenga viwanja vitatu vya kisasa vya mazoezi kwenye Mikoa ya Geita, Dar es Salaam na Dodoma, na kuja kujenga Sports Arena mbili Dar es Salaam na Dodoma.”

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba nimpe taarifa Mheshimiwa Waziri kwamba anachokizungumza kwamba ameshakifanya, hakijafanyika. Kilichofanyika ni mpango mzuri wa Mheshimiwa Rais wa kujenga hiki kitu, na kazi nzuri ya utekelezaji iliyofanywa na Waziri, Mheshimiwa Mchengerwa na Msaidizi wake Dkt. Abbas, ambayo yeye yuko busy kuiharibu. (Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Waziri, Dkt. Damas Ndumbaro, unaipokea taarifa hiyo?

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, siipokei hiyo taarifa. Mheshimiwa Kasalali, anapaswa kuelewa nini maana ya Center of Excellence? Center of Excellence ni kituo cha umahiri ambacho kinatoa huduma stahiki kwa Tanzania kwenye michezo. Kwa Afrika Mashariki our Center of Excellence ni Malya. Atofautishe na academia. Nukuu aliyoisema ya Mheshimiwa Rais inasema, ‘akademia,’ itajengwa akademia pale Malya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa akademia ni kuendele kuimarisha Center of Excellence. Kwa hiyo, asichanganye nukuu ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa akademia…

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, kuhusu Utaratibu.

SPIKA: Mheshimiwa Dkt. Damas Ndumbaro, inaonekana kuna kanuni inavunjwa. Mheshimiwa Kasalali Mageni.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, Kuhusu Utaratibu, Mheshimiwa Waziri, ameamua kulidanganya Bunge hadharani kwa sababu, kwa mujibu wa barua ambayo Wizara yake iliiandikia Halmashauri ya Ilemela, nanukuu: “Yahusu Maombi ya Kiwanja Na. 677A, Losi Busweru cha Ujenzi wa Kituo cha Ufundishaji Michezo kwa Ubora.”

Mheshimiwa Spika, kwa barua ambayo consultant aliwaandikia Wizara kwamba, naomba niisome kidogo kwa ruhusa yako.

SPIKA: Sawa. Sasa ngoja kidogo…

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, kwa barua hii ambayo wao walimwandikia contractor wakiomba kuhamisha Center for Excellence, kutoka Malya ambayo mkataba umesainiwa na Serikali imesaini Mkataba wa Ujenzi wa Center for Excellence Malya, na wao wanaomba kuhamisha Center of Excellence ya Malya kupeleka Ilemela, halafu Waziri anasimama na kulidanganya Bunge kwamba ilishajengwa, sasa atuambie hapa, kwamba huu mkataba ambao tunao hapa ni wa Serikali au ni wa nani? Ulikuwa ni wa kujenga nini pale Malya? (Makofi)

SPIKA: Sawa. Waheshimiwa Wabunge, hoja hii alipokuwa amechangia Mheshimiwa Kasalali Mageni, aliihusisha na Taarifa ya CAG kwa maana ya kwamba utaratibu usipofuatwa ndiyo inapelekea zile hoja za CAG. Sasa, naona mjadala wetu unakoelekea tutatoka nje kabisa ya Taarifa ya CAG. Sasa nataka kufanya maamuzi juu ya jambo hili ili tumalize Taarifa za CAG, halafu kuna mambo kama mawili matatu hivi ambayo yatatuhitaji kuyafanyia kazi.

Kwa hiyo, kwa sababu lililetwa hapa Bungeni na linataka kutupeleka nje ya taarifa ambayo tunayo, kwa sababu, Mheshimiwa Kasalali, aliitumia hiyo kama mfano, siyo kwamba ipo kwenye Taarifa ya CAG kwamba, pengine kuna jambo liko namna Fulani; sasa, tukubaliane hivi, Mheshimiwa Waziri kuhusu hoja hii utapewa nafasi baadaye. Mheshimiwa Kasalali Mageni, kuhusu hoja hii utapewa nafasi baadaye. Tutoe nafasi kwa Mheshimiwa Waziri kutoa ufafanuzi juu ya hoja zingine.

Hoja ya kuhamisha hiyo sijui ni uwanja wa mpira ama ni Center of Excellence ama ni akademia, kutoka Kwimba kuelekea Ilemela tutaijadili baadaye kidogo. Tumalizie kwanza hoja ya CAG.

Waheshimiwa Wabunge, nadhani tumeelewana vizuri. Tumeelewana vizuri?

WABUNGE FULANI: Ndiyo. (Makofi).

SPIKA: Sawa. Mheshimiwa Waziri, kwa sababu utapata nafasi baadaye kidogo ya kutoa ufafanuzi kuhusu jambo hili, maana Mbunge baada ya kukupa hii taarifa nimeona linatoka kabisa nje ya Taarifa ya CAG. Kwa hiyo, kama unayo mengine ya kufafanua ni sawa, kama huna, basi tuliache hili, nitakupa nafasi baadaye ili tuwe na jambo hilo Mezani. Ni sawa Mheshimiwa Waziri?

WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, ni sawa.