Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Awali ya yote naomba kuanza kwa kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayoifanya na uwekezaji mkubwa anaoufanya kwenye Wizara yetu kupitia sekta ndogo tunazozisimamia za umeme, mafuta na gesi.

Mheshimiwa Spika, pili, napenda kumpongeza Waziri wa Nishati na Naibu Waziri Mkuu, Dkt. Doto Mashaka Biteko, kwa kazi nzuri anayoifanya kwenye Wizara ya Nishati.

Mheshimiwa Spika, tatu, napenda kukupongeza Mheshimiwa Spika, pamoja na Kamati kwa kazi nzuri ambazo mmefanya ya kuhakikisha kwamba mnatupa maelekezo na kutusimamia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nne, napenda kumpongeza Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa kazi nzuri anayoifanya katika kuangazia masuala yanayofanywa na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho kwa pongezi, nawapongeza Waheshimiwa Wabunge kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kuonesha uzalendo kwa Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo napenda sasa nitolee ufafanuzi baadhi ya hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezizungumzia. Moja, kuhusiana na kampuni tanzu ya shirika letu la petroli, TPDC (TANOIL). Kampuni hii pamoja na historia ya huko nyuma, ilianza biashara mwaka 2021. Pamoja na majukumu ambayo wamepewa, kampuni ya TANOIL ilipewa jukumu la kununua mafuta lakini vile vile kuuza mafuta kwa wafanyabiashara wadogo, wafanyabiashara wa rejareja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mafuta kwa Taifa letu ni uchumi. Kwa hiyo, kama Serikali isingewezekana kuwachia wafanyabiashara binafsi watawale soko kwa asilimia 100. Ninyi mnafahamu, Watanzania hawa ni watu masikini. Takribani Watanzania milioni 26 wanaishi chini wa mstari wa umasikini. Kwa hiyo, isingewezekana kwa Serikali makini kuachia soko la mafuta, soko ambalo linabeba uchumi wa Taifa hili liweze kutawaliwa na sekta binafsi peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndiyo lazima kama Serikali tuhakikishe tuna sehemu kwenye soko la mafuta ili kulinda hali za Watanzania.

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Simama kwa ajili ya taarifa. Mheshimiwa Mohamed?

TAARIFA

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Spika, ndiyo.

Mheshimiwa Spika, nataka kumpa taarifa Mzungumzaji. Hatukuanziasha shirika hili kufanya wizi. Tumeanzisha shirika hili kuja kufanya biashara. Mpaka sasa hivi shirika hili lina hasara kubwa. Huyo anayezungumza atueleze, hii ripoti ya mkaguzi ni sawa ama si sawa? Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Judith Kapinga, unaipokea taarifa hiyo?

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, siipokei na nadhani nikimaliza kuongea Waheshimiwa Wabunge watakuwa wamenielewa, kwa sababu ndiyo kwanza nipo kwenye introduction. Subiri kidogo Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wote tunafahamu kama nilivyosema mafuta ni uchumi. Kwa kweli, adhma yetu kama Serikali ni kuhakikisha tuna sehemu kwenye soko la mafuta ili tuendelee kulinda hali za Watanzania. Ninyi mnafahamu, mwezi wa saba tulipata dhoruba ya kukosekana kwa mafuta katika Taifa letu. Wafanyabishara binafsi walikataa kuwauzia wafanyabiashara wa rejareja mafuta. Walileta mafuta kwa ajili ya kampuni zao. TANOIL ndiye aliyeagiza mafuta na kuweka mafuta kwa wafanyabiashara wa rejareja ambao wanawauzia mafuta watumiaji wa mafuta kwa asilimia 70. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, … (Makofi)

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, taarifa.
SPIKA: Mheshimiwa Mheshimiwa Judith Kapinga, kuna taarifa kwa Mheshimiwa Mbunge wa Kibamba, Mheshimiwa Mtemvu.

TAARIFA

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, anavyoendelea kuzungumza anatuchanganya kidogo. Underpriced ambayo imefanywa na management ya TANOIL kwa shilingi 70, imesababisha economic wealth ya shilingi bilioni 53. Yaani wasingefanya kushusha hivyo, tungeweza kuokoa shilingi bilioni 53. Pia, kwa sababu unasema sababu ni market…

SPIKA: Mheshimiwa, taarifa ni moja.

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, sababu ni moja hiyo hiyo, kwamba ni market penetration ndiyo maana wakawauzia wafanyabiashara wadogo. Ukweli ni kwamba, aliyeuziwa ni mmoja tu. Kituo cha mafuta kimoja tu. Hivyo ndivyo tulivyoambiwa na CAG. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Judith Kapinga, unaipokea taarifa hiyo?

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, taarifa hii siipokei na kwenye ukweli lazima tutasema ukweli juu ya umuhimu wa TANOIL. Ninapoelekea mbele nitasema changamoto na hatua ambazo kama Serikali tumechukua. Pamoja na kazi ambayo TANOIL imefanya, zipo changamoto ambazo zimejitokoza. Wote tumeona, watumishi wasio waaminifu na wafanyabiashara wasio waminifu waliunda mtandao kwa ajili ya kuhujumu masuala yanayofanyika na TANOIL. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa tunavyoongea, Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati kwa kutuongoza, alishaanza kuchukua hatua. Kwa upande wa watumishi, pamoja na watumishi wale kukaa kando, jana Mheshimiwa Waziri wa Nishati ameshapokea taarifa kutoka kwa TAKUKURU ya kwamba, wameshakamilisha uchunguzi na watumishi wale watapelekwa Mahakamani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, sisi tumechukua taratibu za ndani.

MHE. CONDESTER M. SICHWALE: Mheshimiwa Spika, taarifa.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa watu hawa ni watumishi, kwa taratibu na sheria ambazo tulizitunga sisi wenyewe, tumeshaanza utaratibu wa ndani ili kuhakikisha watumishi hao kwa kufata sheria, tunawaondoka kwenye utumishi. Wakiwa wanaenda Mahakamani, waende kushtakiwa wakiwa raia wa kawaida. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Judith Kapinga, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Condester Sichalwe.

TAARIFA

MHE. CONDESTER M. SICHWALE: Mheshimiwa Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya PAC. Taarifa tuliyowasilisha hapa, ni ambayo sisi Kamati tumejadili tukiwa na CAG mwenyewe na tukiwa tumewaita hao watu wa TANOIL. Anachotueleza Mheshimiwa Naibu Waziri, kinakinzana na kile ambacho kwenye majadiliano yetu tumejadiliana na CAG na tumewahoji wale watu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tunataka kujua, tuitishe Hansard zije hapa kwa sababu Kamati yetu ni Oversight Committee. Tunazo taarifa ambazo tumewahoji wale watu mbele ya CAG, wakatujibu na hiki ambacho anatujibu kinakinzana. Tushike kipi? (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Judith Kapinga, unaipokea taarifa hiyo?

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, sipokei kwa sababu nimeongelea masuala kadhaa… (Kicheko)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hakuna taarifa juu ya taarifa. Mheshimiwa Judith Kapinga.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ameongezea masuala kadhaa, sasa sijajua mahsusi alikuwa anazungumzia eneo gani. Tumechukua hatua kama ambazo nimezisema lakini vile vile kuendelea mbele, suala hili lina sehemu mbili. Lina suala la watumishi na lina suala la wafanyabiashara. Wafanya biashara wale kwa mtandao wao, ndiyo ambao wamekubali kuchukua discount nje ya utaratibu. Vilevile, wamekuwa na madeni makubwa ambayo wamegoma kuyalipa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa, kupitia Bunge lako Tukufu naomba niwataarifu…

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI:….kwamba kama ni mtumishi kama ni mfanya bishara anayehusika, wote hawako salama na tutachukua hatua kwa pande zote mbili. (Makofi)

MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Mwakasaka, nadhani ameshapewa taarifa tatu. Ameshapewa taarifa na Wabunge watatu tayari. Mseshimiwa Judith Kapinga.

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, hatutaishia kwa watumishi kama nilivyosema. Mfanyabishara yeyote ambaye anafahamu amenufaika kwa discount ambaye anafahamu amechukua mafuta bila kulipa, tutachukua hatua. Kwa kumalizia, nafahamu baada ya leo hii simu zitakuwa nyingi. Message zitakuwa nyingi, vi-note vitakuwa vingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nikuhakikishie hatutaangalia. Msumeno ambao umewakata watumishi, ndiyo msumeo ambao utaenda kuwakata wafanya biashara bila kuangalia ni nani. Baada ya kusema hayo, nakushukuru. (Makofi)