Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi nashukuru kwa kunipa nafasi hii kuweza kuchangia katika ripoti hizi tatu ambazo zimewasilishwa.

Mheshimiwa Spika, mimi na-declare interest kwamba ni Mjumbe wa Kamati ya LAAC. Nachukua nafasi hii kwa kweli kuwashukuru Wajumbe wa Kamati ya LAAC, haya ambayo Waheshimiwa Wabunge ninyi mnakutana nayo sasa hivi sisi kwetu imekuwa ni kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unaweza ukaona uzito wa kazi yetu kwa kweli kama Wajumbe wa LAAC na namna ambavyo tunaathirika sana kwenye akili tunapokuwa tukichambua ripoti hizi za CAG hasa kwenye suala la Serikali zetu za Mitaa.

Ndugu zangu mimi nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa namna ambavyo mmeongelea kwa uchungu na sisi mmetuunga mkono kwenye uchungu wetu na hayo ndiyo ambayo yapo ndani ya nchi yetu na kwa kusema hivyo hatuna maana kwamba pamoja na haya ambayo yapo haina maana kwamba hakuna mazuri yaliyofanyika. Mazuri yapo mengi sana lakini katika hayo mazuri madoa yake makubwa ndiyo haya.

Mheshimiwa Spika, CAG ni chombo ambacho sisi wenyewe tumeridhia, tumeweka utaratibu ili kuiendesha nchi yetu, lakini inaonesha kwamba baadhi ya wenzetu wanaona anakuwa kama adui. Hili tunalipata kutokana na namna ambavyo CAG akitoa maoni yake yanashughulikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zipo Halmashauri nyingi sana hazijibu hoja za CAG, hoja ambazo zinaelezea ubadhirifu na upotevu wa hivi vitu na rasilimali za nchi katika Taifa letu. Sasa mimi nashindwa kuelewa kama sisi wenyewe tumepitisha na tumekubali kiwe ni chombo ambacho kinaweza kutusimamia, ni kwa nini hatuwezi kusimamiana na kuhakikisha kwamba hoja za CAG zinajibiwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu cha kwanza ambacho mimi nakiomba, kwanza zile Halmashauri ambazo hazijibu hoja za CAG ndiyo indicators za kwanza kwamba haziko tayari kuhakikisha kwamba zinasimamia rasilimali za nchi hii zinatumika kama zilivyopangwa na hiyo iwe ni indicator ya kuanza kuwafuatilia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine nilichokiona, mfumo wetu wa uendeshaji, hapa kila mtu analalamika. Mheshimiwa Rais amekabidhiwa hii ripoti analalamika, Wabunge tumekuja tunalalamika na Serikali nayo ikija italalamika, watendaji nao wanalalamika, sasa ni nani atakayekwenda kutatua hili tatizo?

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Jesca Msambatavangu kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Jenista Mhagama.

TAARIFA

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nampongeza Mheshimiwa Jesca kwa mchango wake, lakini naomba niweke sawa mchango wake pale anaposema kwamba Mheshimiwa Rais analalamika, hapana, Rais hajalalamika, kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 34 ama 36 Mheshimiwa Rais amepewa majukumu ya kukasimu madaraka yake kwa watendaji mbalimbali kwenye taasisi.

Mheshimiwa Spika, alichokuwa anakifanya Mheshimiwa Rais ni kujaribu kuwakumbusha watendaji wote wajibu wao wa kusimamia na kuhakikisha kila jambo linakwenda sawasawa. (Makofi)

Kwa hiyo, ukimtafsiri Rais kwa kuendelea kuwasimamia watendaji wake na kuwaelekeza kazi zinavyotakiwa kufanywa kule siyo kulalamika. Kwa hiyo, nilikuwa naomba kumpa taarifa Rais hajawahi kulalamika, anaendelea kutoa maelekezo. (Makofi)
MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika,…

SPIKA: Ngoja Mheshimiwa. (Kicheko)

Mheshimiwa Msambatavangu unaipokea taarifa hiyo?

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, sijui niipokee au nisiipokee? Nitabaki neutral lakini nataka kusema hivi, wakati Mheshimiwa Rais anakabidhiwa taarifa hii sisi wote ni Watanzania na tulikuwa tuna masikio, tulimsikia akilalamika kutokana na ubadhirifu uliofanywa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuendelea kujipamba hapa na kujitekenya wenyewe kwamba hakulalamika haisaidii. Kulalamika siyo dhambi, ni kutoridhika na hali inavyokwenda. Sasa sisi Wabunge hapa tunalalamika, Rais analalamika, ninyi Mawaziri ndiyo mnatetea, kwa hiyo ninyi mnakubaliana na huu uovu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Watanzania wamelalamika, sisi tunalalamika kwa sababu hatukubaliani na hii hali kwamba hiki kinachoendelea siyo sawa. Kwa hiyo, hakuna aliyepongeza, Rais hakupongeza kwamba hii taarifa iko sawasawa. Sisi tunachowaomba wao waende wakasimamie na mimi naomba tusichekeane, unajua kila mtu Mungu kamuumba kwa ajili ya uwezo wake. Kuna mahali…,kwa mfano naweza nikatoa mfano mdogo hapa kuna mahali tunahitaji daktari mpole wa kumfariji mgonjwa, kuna mahali tunahitaji nesi mkali wa kumpiga mama ili ajifungue. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, huwezi kuwalaumu manesi wote kwamba wote wanafanya kitu…hapana, kwa sababu watoto hawatazaliwa kama manesi wote wakianza ku-act kama wapole fulani hivi kama wachungaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lazima tufike mahali tusimamiane, Mheshimiwa CAG anaongea hapa mass dropout ya watoto, amesema watoto wa shule za msingi karibu 19,000 wameacha shule. Watoto hawa ni kati ya umri wa miaka sita mpaka 13 - 17 wamekwenda wapi? Tuna Wizara inashughulika na watoto, watoto leo ukipita wanavuta shisha, watoto leo ukipita kuna snacks zinawekwa bangi watoto wanakula. Serikali ipo mnaona, Waziri Mkuu alisimama hapa akazuia package za viroba ili watoto wetu wapone. Leo mmerudisha tena vinywaji vilevile vyenye package ndogo watoto wetu wanalewa mitaani, wanakufa tu haya yote CAG ameyasema. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunakaa hapa tunachekeana mimi nataka niwaambie hivi Taifa hili lina Mungu na nafasi uliyopewa Mungu ameamua uwepo. Ikishindikana sisi humu tunasema halafu hatua hazichukuliwi sisi tunaingia kwenye maombi Mungu atusaidie namna ya kuwa-overhaul, hatuwezi kuacha watoto wetu wanangamia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, CAG anasema hapa, leo kuna sababu CAG ametoa za mass dropout; ngoma, watu wanakwenda kwenye ngoma. Mkurugenzi wa Bagamoyo tunamuuliza kwa nini watoto wengi hawaendi shule namna hii anasema ngoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivi kweli watu tumekaa ni viongozi…, wewe nikuulize kina mama tupo humu ndani, Wabunge wanawake tupo humu ndani, wewe unaweza kuolewa na miaka 13 ukashika mimba kwa ile labor pain ukaenda kujifungua?

Mheshimiwa Spika, leo CAG anasema watoto wanapata mimba wakiwa na umei kati ya miaka 13 – 11. Watoto darasa la saba hawamalizi, tuna Wizara ya Elimu, tuna Maendeleo ya Jamii sijui tuna nini, watoto wanapotea hatuoni. Watoto wa sekondari, mass dropout sekondari, sisi zaidi ya asilimia 50 watoto wanatoka na division zero na division four kwenye public schools.

Mheshimiwa Spika, tuwashukuru Manispaa ya Moshi; Moshi tulipowauliza kwa nini watoto wanatoroka shule? Mkurugenzi akasema Moshi watoto wengi wametoka kwenye public schools wamehamia kwenye private schools. Sasa ndiyo tuulizane humu ndani wengine wanatoka kwenye shule za Serikali kwenda kwenye shule za watu binafsi, ni dropout hiyo. Lakini wengine wamekwenda ngoma, ni dropout hiyo, lakini wengine wanakwenda masoko ya usiku. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, Buhigwe, Kasulu eti kuna watoto wanakwenda masoko ya usiku; mnauza nyama kule, mnauza vitu, mnauza na watoto huko huko. Watoto wanashindwa kusoma, tumekaa hapa kama viongozi tunafanya nini? (Kicheko)

SPIKA: Sekunde 30 Mheshimiwa malizia mchango wako.

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, kitu kingine wafanyakazi; watumishi bado wanadai shilingi bilioni mia moja naa, kweli leo kuna Halmashauri moja ya Pwani watumishi saba wameamua wachange hela wapeleke kwenye Mfuko wa NSSF kwa sababu Serikali haikuwachangia ili walipwe mafao yao, wazee wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mbunge wa Kigoma alisema hapa kule mnafanya ni sehemu ya adhabu ni kweli. Kigoma na Nkasi watumishi wanadai mishahara, hawajalipwa mafao yao, tumesema kwa nini? Mkurugenzi anasema mimi nilikuwa bado sijafanya uhakiki. Kuna mtu anaitwa Urassa kutoka Kigoma ni Afisa Uchaguzi anadai shilingi milioni 63, mwingine anadai shilingi milioni 71. Kuna Godigodi anadai shilingi milioni 53 hawa ndiyo mnategemea wakasimamie miradi ya shilingi bilioni mbili, bilioni sita wakati wanawadai fedha zao, arrears za mshahara zaidi ya shilingi milioni 19 wataweza wapi? (Makofi