Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi natumia nafasi hii kukushukuru wewe, lakini kipekee nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika Taifa letu la Tanzania lakini katika Jimbo langu la Manyoni Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwashukuru hawa ndugu zangu wawili, Profesa Kitila na Daktari Mwigulu kwa kazi kubwa ambayo mnaifanya ya kumsaidia Rais katika hizo Wizara mbili nyeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi leo nina mambo machache sana na nitaanza na Profesa Kitila. Kwa Profesa Kitila nimekuwa nikitafakari ni jinsi gani tunaandaa hii miradi yetu mbalimbali kila mwaka kupitia, mpango wa maendeleo wa kila mwaka ambao tumeuvunja kwenye ule mpango wa maendeleo wa miaka mitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la kwanza huwa natafakari unakuta kwenye kijiji kimoja tumepeleka miradi mitatu, Mradi wa Maji, Mradi wa Umeme, Mradi wa Barabara lakini ukiangalia hii miradi yote haisomani, kwa lugha nyingine hakuna convergency.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningemshauri Mheshimiwa Waziri Profesa Kitila, katika eneo ambalo Wizara ya Mipango inahitaji kutusaidia ni kuhakikisha kwamba kunakuwa na convergency invent. Kwamba tunapoenda kwenye kijiji kimoja Mheshimiwa Rais amepeleka Mradi wa Maji, Mradi wa Umeme, Mradi wa Afya nini interpretation ya wananchi wa pale in terms of invent, hilo ni eneo la kwanza ningeliomba Mheshimiwa Waziri ulifanyie kazi. Tunahitaji kuja na framework ambayo ita-tap hizo convergency intervention zote tuone ni jinsi gani wananchi wapo satisfied na ile miradi yote iliyoenda katika eneo moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni suala la agenda ya vijana (youth agenda). Tumeshafanya mambo mengi sana, Mheshimiwa Rais amefanya mambo makubwa kwenye huduma za jamii, ninategemea sasa na ni matarajio yangu na ni matumaini yangu kuona huu mpango sasa una-move kutoka kwenye huduma za jamii kwenda kwenye agenda ya kuwaendeleza vijana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, agenda ya vijana ni global agenda na hasa hasa kwenye masuala ya kuwajenga kiuchumi. Kuna maeneo mawili nchi za wenzetu wamefanya na hasa hasa vijana ambao wapo out of the school. Tuna kundi kubwa la vijana waliomaliza shule ya msingi hawakufanikiwa kuendelea sekondari, waliomaliza sekondari hawakufanikiwa kuendelea vyuoni wapo mtaani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri mambo mawili, la kwanza tunahitaji sasa kuja na comprehensive program kwenye masuala ya elimu ujuzi. Katika hili eneo Ofisi ya Waziri Mkuu imefanya, lakini bado kuna changamoto. Changamoto ya kwanza tunawachukua vijana kutoka vijijini wanaenda kusoma Singida Mjini, kuna wengine wanashindwa kule kwa sababu ya gharama. Kwa nini tusianzishe program kama hizo za kuwajngenea ujuzi katika maeneo yao, kwenye zile locality zao, kwenye kata, kwenye tarafa ili kuwapunguzia huo mzigo wa wenyewe kusafiri kwenda kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, eneo ambalo tunaweza tukalifanya vizuri sana na tukaja na mradi mkubwa wa kuwasaidia vijana wa kitanzania hasa wale waliomaliza shule ya msingi, waliomaliza sekondari hawakufanikiwa kwenda kwenye vyuo vya juu, ni kuwajengea ujuzi kwa kupitia mafunzo ya muda mfupi, miezi miwili, miezi mitatu, wakitoka pale tunaweza tukawa-link kwenye viwanda mbalimbali ambavyo vipo hapa. Hili ni eneo ambalo ni muhimu sana linaweza likatusaidia sana kwenda na hii agenda ya vijana ili tuweze kuwasaidia vijana wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni eneo la mradi wa BBT wa Bashe. Mheshimiwa Bashe idea yako ya BBT it is a very brilliant idea, lakini Mheshimiwa Bashe usipokuwa makini na hii idea you will fail. Naomba nikushauri kitu kimoja, hii idea ni brilliant sana kwa sababu kwanza una-address youth agenda lakini kuna tatizo moja la selection bias. Umewahamisha vijana kutoka Manyoni umewapeleka Morogoro that is not sustainable. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeshauri tu-focus kwenye maeneo yao tujikite kwenye ile local economic development. Kama aneo ni potential kwa kilimo wakusanye wale vijana wanaotoka kwenye lile eneo BBT ifanye kazi kwenye lile eneo, lakini kuwatoa Manyoni kuwaleta Dodoma, kuwatoa Manyoni unawapeleka Morogoro kimsingi haitakuwa endelevu. Kwa hiyo, hili ni eneo ambalo mimi ningekushauri kwamba Serikali iweze kulifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ushauri kwa ndugu yangu Daktari Mwigulu kwenye suala la bajeti, tuna miradi mingi ambayo umeitaja pale Serikali inaenda kuitekeleza lakini kwa upande wa Manyoni mimi ningeshauri jambo moja. Tuna miradi ambayo imetajwa sana kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa mfano Daraja la Sanza, kila mwaka Daraja la Sanza kila awamu Daraja la Sanza huwa linatajwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Rais safari hiii, ameruhusu angalau mkandarasi ameshapatikana sasa tunaomba Daraja la Sanza liende likaanze kujengwa. Kuna Daraja la Ngonjigo chini ya TARURA vilevile kuna Bwawa la Mbwasa Mheshimiwa Bashe, hili bwawa kwenye kila Ilani ya CCM lipo. Nakushukuru na wewe mwaka huu naona umeshaliweka sasa nategemea kwamba kwenye bajeti hii sasa litaenda kutekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho Mheshimiwa Dkt. Mwigulu kuna huu Mradi wako wa Mwalala, kituo cha pamoja cha ukaguzi wa magari. Huu mradi ni wa zaidi ya bilioni 30 ulisimama tangu 2016 ulishafikia asilimia 60 mmetumia zaidi ya bilioni tano imeshakuwa pori pale. Nikuombe Mheshimiwa Dkt. Mwigulu zile ni fedha za watanzania twende tukauokoe huu mradi wananchi wanalalamika kwa nini mradi ulisimama tangu 2016 na mradi una tija naomba sana huu mradi safari hii kwenye bajeti hii, twende tukau-revival uanze kufanya kazi kwa sababu ni mojawapo ya miradi ambayo ina tija sana kwa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nirudie kumshukuru sana Mheshimiwa Rais, lakini niwashukuru hawa Mawaziri wawili Profesa Kitila na Daktari Mwigullu kwa kazi kubwa mnayoifanya. Baada ya kusema haya naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)