Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza kabisa nianze kwa kusema kwamba suala la bajeti ni moja ya jukumu muhimu sana la Kibunge ambapo linapima uwezo wa Bunge katika kushiriki kupanga na kupitisha matumizi ya Serikali na baadaye kuhoji matumizi ya bajeti tengwa.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu huo ni muhimu tukajikumbusha kwamba nchi yetu imepata makusanyo makubwa kutoka kwenye sekta mbalimbali. Moja ya sekta muhimu sana ambayo nchi imekuwa ikikusanya mapato hayo makubwa ni Sekta ya Utalii. Tuna taarifa kwamba kabla ya COVID - 19 sekta hii ilikuwa inakusanya takribani asilimia 17.9 na baada ya COVID-19 inafanya vizuri kuelekea kufikia kiwango kilekile ambacho kilikuwepo awali.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya mchanganuo huo na mchango huo wa sekta hii kwa pato la Taifa, ni muhimu sasa Serikali na wananchi tunapaswa kujua tuna wajibu wa kulinda vya kutosha sekta hii kwa wivu mkubwa. Ni wakati muafaka nafikiri wa Serikali kuweka wazi na kuwaeleza wananchi wa Tanzania kujua vita kubwa inayoendelea kiuchumi hasa hasa kwenye sekta hii upande wa East Africa. Tusidanganyane hapa, kumekuwa kuna maneno mengi sana na kuna watu wamekuwa wakizungumza mambo mengi wakijinasibu kwamba wao ni wazalendo, mimi nasema hivi hakuna mahali popote katika dunia hii anakuwepo mzalendo wa Taifa lake anakuwa na guts za kwenda kwenye public na ku- damage nchi yake kwenye ajenda ambayo inahusiana na masuala ya kimataifa. Ni wakati wa kuwaeleza wananchi wa Tanzania ukweli, wajue ukweli ili tuweze kushikamana sana kwenye vita hii ya kiuchumi inayoendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitaenda kwenye mjadala unaoendelea sasa, mjadala wa National Cake Ngorongoro; yanasemwa mambo mengi sana na mambo haya yanayosemwa na yana pollute mind za Watanzania, ni vema tukaweka mambo sawasawa hapa mezani kwangu na ukihitaji nitakupatia hapo nina ripoti ya TAWIRI, TAWIRI ni Tanzania Wildlife Research Institute ya mwaka 2020 ambayo inaonyesha kwamba idadi ya watu Hifadhi ya Ngorongoro kwa miaka 30 mfululizo kuanzia mwaka 1970 na kuendelea mpaka 2018 imeongezeka mara tano zaidi hii ni ripoti ya utafiti. Ukiangalia the citizen gazeti lilinukuu takwimu ya sensa maalum ya Ngorongoro mwaka 2017 ilikuwa ni sensa maalum kabisa kwa ajili ya National Park ya Ngorongoro inaonyesha idadi ya wananchi kwenye Hifadhi ya Ngorongoro ilifika 98,183 kutoka wananchi 8,000 mwaka 1959. Ukiangalia upande wa mifugo ilitoka mifugo 16,100 mpaka mifugo 805,000 kwa muda huo huo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa kwa hesabu ndogo tu ambayo haihitaji records science, ukiangalia eneo la Ngorongoro ni kilometa za mraba 8,292 kwa mwaka 1959 uwiano wa mtu mmoja na eneo ilikuwa hivi; mtu mmoja anakaa kilometa za mraba moja lakini kufikia mwaka 2019 uwiano ukabadilika mtu mmoja anakaa kilometa za mraba 0.084 sawasawa na hivi watu 11 wanakaa kilometa za mraba moja. Hapo bado sijataja nafasi ya wanyama katika eneo hilo. Naomba niseme hivi, hesabu hazijawahi kudanganya, nimejaribu kuyasema haya yote kwanza ili kuthibitisha hoja ya msingi ya idadi ya watu kuwa kubwa kwenye hifadhi na ndiyo maana Serikali ikaona umuhimu wa kupunguza idadi ya wananchi na wanyama katika maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wanasiasa na wanaharakati waache kupotosha wananchi kwa kutumia kiraka cha haki za binadamu. Kwenye vita hii naomba nitangaze, naungana na Mkuu wa Nchi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kulinda urithi wa Tanzania, naungana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kulinda Taifa na urithi wa Taifa letu, naungana na wananchi wote wa Tanzania wanaosimama na kulinda Taifa letu na urithi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namwomba sana Mkuu wa Nchi, Mheshimiwa Rais kwenye hili asirudi nyuma, vizazi na vizazi vitamkumbuka katika hili, hili suala limekuwa likijaribiwa kwa muda mrefu bila mafanikio. Tunahitaji rasilimali hii I mean tunahitaji keki hii ya Taifa ambayo Mwenyezi Mungu ametupa, inufaishe vizazi na vizazi. Pia tuambiane ukweli hivi ni wapi katika Taifa hili kimewahi kufanyika kilichofanyika kule Msimiro? Ni wapi acha Tanzania, East Africa ni wapi kimewahi kufanyika kilichofanyika Msimiro, leo wananchi wanahamishwa Msamiro I thinkā€¦ (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, Handeni.

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, Handeni huko. Leo wananchi wanahamishwa unapelekwa eneo unajengewa nyumba, unakuta hospitali, unakuta shule, unapewa hati kama una wanawake watatu unapewa hati za nyumba tatu, naomba leo nitangaze rasmi mimi naitwa Ole-Kishoa ili nipelekwe kule Msamiro na mimi nikapewe nyumba ya bure kabisa. Na wanao pinga hili wanatakiwa ku-declare interest, tuna taarifa kuna wabunge wengine humu ndani wanatetea haya kwa maslahi ya mashemeji zao huko, tunajua. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kuna wanaosema kwamba wananchi wa Loliondo na Ngorongoro hasa hasa wananchi wa Ngorongoro kuhamishwa eneo lile ni makosa kwa sababu maeneo yale wameshayazoea. Nataka niseme jambo moja tunatengeneza double standard ya hali ya juu sana katika Taifa letu, kwa sababu kama hili likisikilizwa maeneo mengine watu watakapokuja kuhamishwa kwa kupisha miradi ya maendeleo watajenga experience ya Ngorongoro, watakataa watasema mbona Ngorongoro hawakuhama kwa sababu walikuwa wamezoea maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nina mambo manne ya kushauri; la kwanza, ni muhimu sasa Serikali ikaweka wazi ime-target kiwango kiasi gani cha wananchi wanaotakiwa kubaki pale katika Hifadhi ya Ngorongoro. Pili; Wizara iongezewe bajeti kwa ajili ya kuhakikisha kwamba zoezi hili linafanyika ufanisi mkubwa sana. Tatu; mbinu rafiki za kuhamisha wananchi hawa ziendelee kufanyika kwa sababu tunahitaji wananchi hawa wahamishwe kama ambavyo inafanyika sasa, wamehamishwa kwa hiari kabisa, hakuna ambaye amelazimishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho; tunahitaji kwenye yale maeneo ambayo wamepeleka vituo vya afya wapeleke Madaktari wa kutosha. Eneo ambalo wamepeleka shule wapeleke Walimu wa kutosha ili wananchi wa Ngorongoro ambao wamehamia maeneo hayo waweze kupata haki zao stahiki.

Mheshimiwa Spika, nakusihi sana kupitia Bunge lako hili Tukufu liendelee kuwasihi wananchi wa Tanzania, ni vema tukalitazama suala hili kwa sura ya kizalendo katika nchi yetu, ni vema ifike mahali tujue kwamba hakuna mtu mwenye nia ovu katika suala hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wapo watu wanaoaminishwa kwamba eneo hili kuna sijui mwarabu anataka kulichukua, yaani kuna propaganda za ovyo, watu wanatafuta kiki. Wanasiasa wanatafuta kiki. Tusiruhusu mambo haya. Najisikia vibaya sana kuona kwamba leo niko kwenye nchi ambayo kuna mwananchi from know where yuko nchi nyingine anamtukana Rais wa Tanzania. Hili suala haliwezi kukubalika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kwa kumalizia nigusie jambo moja linalohusiana na Jimbo la Mkalama, Singida. Nimekuwa nikisikiliza sana watu wengi sana humu ndani wakiwa wanachangia, wanazungumzia kwenye suala la miundombinu, wanazungumzia ukubwa wa barabara zao kutokuwa na lami, mtu anazungumzia kilomita mbili, mwingine anazungumzia kilomita tatu na mwingine anazungumzia kilomita tano.

Mheshimiwa Spika, kuna Wilaya moja Mkalama ipo Singida kule pacha na Wilaya ya Mheshimiwa Waziri alikotoka, Wilaya ya Iramba. Hii Wilaya ya Mkalama kuna kilomita zaidi ya 42 kutoka barabara kuu mpaka kufika Halmashauri. Barabara ni ya vumbi, barabara ni rough road, ni mbaya, madaraja hayafai, hayapitiki mvua ikinyesha. Wananchi wa kule wanajishughulisha sana na suala la kilimo cha vitunguu. Ikifika wakati wa mavuno wanapata taabu sana.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Spika, namwomba kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, kama kuna jambo ataliacha kuwa na alama kwenye Wilaya ya Mkalama ambalo ni pacha na Jimbo lako la Iramba, fanya jambo kwa ajili ya Wilaya hii Mheshimiwa Waziri. Inasikitisha sana kuona kwamba Iramba... (Makofi)