Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ABEID R. IGHODO: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mchango wangu wa maandishi kama ifuatavyo; kwanza kabisa nachukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi anayoifanya ya kuiheshimisha nchi yetu katika sekta ya utamaduni, michezo na sanaa na kuwapongeza Waziri na Naibu wake.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu mkubwa ni kuhusu kufanyika kwa matamasha ya utamaduni; Wizara ione namna bora ya kuendelea kuenzi utamaduni wa Mtanzania. Kwa mfano leo tarehe 6 na 7 Juni, 2022 Mkoani Shinyanga linafanyika Tamasha la Utamaduni wa Msukuma pamoja na kuzindua Kijiji cha Makumbusho ambapo itakuwa sehemu ya kupata historia ya eneo hilo kuanzia utawala wa kimila na desturi za Wasukuma. Sasa ni vyema Wizara ikatambua jitihada za Mkoa wa Shinyanga kwa kuwa imetekeleza kwa vitendo agizo la Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan la kuandaa matamasha ya utamaduni lakini pia iwe ni chachu kwa Mikoa mingine kuweza kufuata mfano huo ili na maeneo mengine nayo yawe na vijiji vya makumbusho na itaweza kuwa kama sehemu ya utalii ambapo itasaidia kwa wananchi kujua asili ya makabila na historia zake, lakini pia itasaidia kuongeza vyanzo vya mapato kutoka kwa watu watakaotembelea maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, lakini pia nashauri ili kuenzi utamaduni wa Mtanzania, itengwe siku au wiki ya utamaduni kwa nchi nzima ambapo mikoa yote itatumia vijiji ambavyo vitajengwa kwa kushirikiana na machifu ili Taifa liwe na siku ya kuenzi utamaduni wake. Lakini pia katika kukazia siku hiyo kuwe na sehemu ambayo itakuwa ya kitaifa ambapo kila mwaka mnaweza kufanya mzunguko (rotation) ili liwe na ladha tofauti.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tuweke utaratibu wa kuandaa au kuchapisha vitabu vya kihistoria ambavyo vitaonesha asili ya kila sehemu kwa wakati huo na namna utawala wa kimila ulivyokuwa ili kuongeza wigo wa utalii kupitia fasihi andishi kwa kuwa vitabu hivyo vitakuwa vikielezea utamaduni wa kila mikoa.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.