Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, tunamshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujalia amani, upendo, afya, mshikamano na utashi wa kisiasa katika Taifa letu. Tunampongeza sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdori Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa usimamizi wao thabiti katika utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2022-2025.

Mheshimiwa Spika, tunawapongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Spika, Naibu Spika, Mawaziri, Naibu Mawaziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na watendaji wote Serikalini, kwa kuzitumikia vizuri sana nafasi zao kikamilifu, hongereni.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nitoe mchango wangu kupitia hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii na taarifa ya Kamati iliyowasilishwa katika Bunge letu; tunaiomba Serikali itoe mpango kazi wa shughuli za michezo kwa Kamati za Wilaya na Mikoa ili kufanikisha uibuaji wa vipaji vya michezo kwa vijana wetu kutoka ngazi za shule za msingi, sekondari na wilaya ili kuwalea na kuendeleza vijana wetu katika ngazi mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, tunaiomba Serikali iajiri maafisa michezo na utamaduni katika halmashauri zote nchini ili kufanikisha maendeleo ya michezo hapa nchini na pia tunaiomba Serikali ifanye utaratibu wa kuendeleza viwanja vya michezo kama vile uwanja wa michezo wa Nyerere Stadium, Mbulu kwa kuingia ubia na Chama cha Mapinduzi kwani hali ya hewa ya Mbulu ni nzuri sana kwa michezo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.