Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuwa mchangiaji wa kwanza jioni hii, sauti yangu haipo vizuri sana kwasababu ya furaha tuliyokuwa nayo kule tulikotoka, furaha ya kupata miradi ile ya maji kama tulivyosema kule leo Waheshimiwa Wabunge tumetoka kusaini ile Miji 28 tumeisemea sana. Kwa hiyo, tumekuwa na furaha sana tunampongeza sana Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan na Bunge kwa ujumla kwa sababu limesukuma sana ajenda hii, na kwakuwa maji ni kila kitu tunaamini sasa hata kama viwanja vilikuwa vikavu sasa vitakuwa vinamwagiliwa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo nipongeze Wizara kwa kazi nzuri inayofanya, pia nitumie nafasi hii kuwapongeza mabinti zetu ambao wamefuzu kwenda World Cup, pia niweze kupongeza Simba Sports Club kwa kuendelea kutubeba katika michezo ya Afrika mwakani tena msimu ujao tutakuwa na timu nne, tutakuwa na timu nne kutokana na performance ambayo Simba imekuwa ikiifanya kwenye michuano ya Kimataifa na ninaona kuna dalili wenzetu pia wanaweza mwakani tukawa nao sasa waje kujifunza kutokana na uzoefu ambao Simba tumekuwa tukiupata mpaka kuwezesha kupata nafasi nne. (Makofi/Vigelegele)

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa David Cosato Chumi kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Ester Amos Bulaya.

T A A R I F A

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, wanasema wali wa kushiba unaonekana kwenye sahani, nakubaliana na performance yao lakini unapozungumzia timu iliyojiandaa kuiwakilisha vema Taifa letu ni Dar Young African kwa kuanza kuchukua ubingwa mapema kwa gap kubwa zaidi ya point 10 mpaka sasa hivi, hamna namna na hii haijaja tu ni maandalizi mazuri ambayo tumejipanga wanayanga kuhakikisha tunaenda kuipeperusha bendera yetu vizuri. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana. Mheshimiwa David Cosato Chumi, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, mimi nataka nijielekeze kwenye mambo ya msingi na kwa sababu hiyo siipokei. Waheshimiwa Wabunge naomba mnisikilize vizuri. (Makofi/Kicheko)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, kweli.

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, ninataka nitoe ushauri wa muhimu sana, mwakani tutakuwa na timu nne, tulishakuwa na timu nne lakini yaliyowakuta wale tunawaita wanajeshi wa mpakani biashara wakaishia njiani kutokana pengine na kukosa uzoefu wa namna gani unatakiwa ujipange unapokwenda Kimataifa. Pamoja na kucheza na kadhalika nikufahamishe kwamba kushiriki Kimataifa kuna mambo mengi na hapa niwaombe TFF watusaidie sana zile timu ambazo zitakuwa zimepata nafasi kwenda kushiriki Kimataifa ikiwezekana wawape hata rehearsal. Kwa mfano; nakumbuka Biashara walienda Djibouti siku hiyo hiyo wakashindwa kwenda Libya kwa sababu unapoenda nje lazima ujue je, ile nchi unayoenda je, unahitaji visa? Je, kama unahitaji visa ni ile refereed visa ambayo inabidi uombe in advance au unahitaji visa ambayo ni visa on arrival, haya mambo yote ya logistics haya lazima uwe na weledi nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana natoa wito kwa TFF hizo timu nne zitakazoshiriki michuano hiyo ya Kimataifa wawape hayo mafunzo, hapa natoa wito kwa vilabu vyetu kama ambavyo tunao wasemaji katika vilabu vyetu, kama ambavyo tunao Madaktari katika timu zetu ifike wakati sasa tuwe na ma-protocol officer kwenye vilabu vyetu. Mimi nimefanyakazi Foreign Affairs, nimefanyakazi Idara ya Protocol mtu wa itifaki ni muhimu sana kwa sababu ndiyo anashughulika na logistic zote. Je, timu ina passport, wachezaji wana passport, masuala ya visa, mambo ya Airline kwamba je, hii route tunayoenda tuunganishe wapi au tufanye vipi iwe route fupi timu isifike imechoka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ndiyo maana naendelea kutoa wito kwa TFF na Serikali maana tunaweza tukawa tunapata timu nne, nafasi nne kila mwaka, Simba wanatoka jasho wanatubeba tunakuwa na timu nne lakini zikifika kule zinaishia njiani. Naomba hilo Waheshimiwa Wabunge tulichukulie kwa uzito sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la pili mchezo wa riadha. Huu ni mchezo ambao unaweza kusaidia sana kututangaza tena si kwa gharama kubwa sana. Kwa mfano, katika marathon kubwa duniani New York Marathon, Tokyo Marathon, Boston Marathon, London Marathon, Chicago Marathon. Kwa mfano, New York Marathon tu wakati wale wakimbiaji wanakimbia kuna zaidi ya watu milioni mbili along the road wanafuatilia. Sasa kama pale una wanariadha wa Tanzania watatu, wanne wamevaa ile nguo ya kukimbilia imeandikwa Tanzania unakuwa umetangaza Taifa kwa gharama bure kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zaidi ya watu milioni 300 wanafuatilia kwenye tv hizi marathon, sasa sioni sababu gani sisi watushinde Wahabesh, watushinde Eritrea, watushinde Kenya ambao mazingira tunafanana. Kwa hiyo, ninaiomba Serikali hebu tuwekeze pia katika mchezo huu tuwe very serious ili kusudi tuweze kuitangaza nchi yetu kupitia mchezo wa riadha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunajipanga sana kwenda Kombe la Dunia, tunaenda na hii timu ya mabinti zetu, je, tumejiandaaje? Mheshimiwa Waziri lazima tujue kama Taifa tunao makocha wangapi wa leseni gani na wako wapi, je, tunao matabibu wa michezo, tunao sports psychologist wangapi, wale watoto wameenda Cameroon kuna mazongezonge wamekutana nayo nani kulikuwa na psychologist ambaye anakuwa sports psychologist wa kuwaandaa hawa watoto kukabiliana na kwenda ugenini? Waamuzi ni mambo ambayo kama tunakataka tuwe serious, ndugu zangu kitu kama mpira wa miguu hakina muujiza it needs serious preparation. Preparation kubwa kwa watanzania hamasa jamani tumeshafika mbali, hamasa ya mpira ipo juu tunashida ya mambo mawili, miundombinu ya viwanja na suala la waamuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri kama unataka uache legacy jielekeze kwenye hayo mambo mawili. Viwanja Mheshimiwa Waziri bahati nzuri tunaweza kushirikiana na Chama cha Mapinduzi vile viwanja tayari miundombinu ya msingi ipo, lakini pia viwanja hivi tukivitengeneza viwe kwa ajili ya mchezo wa mpira wa miguu labda na riadha. Siyo sahihi sana kiwanja hicho hicho leo ikija sijui tamasha la muziki humo humo, tamasha la muziki wa injili humohumo, tamasha sijui la nini humohumo haiwezekani. Ndiyo maana tunaendelea kushauri kujenga Sports Arena na kujenga facilities kwa ajili ya mambo ya entertainment na burudani kwa sababu ni kitu ambacho kinapeleka sana Taifa mbele.

Mheshimiwa Spika, mwisho; mchezo wa netball; nashukuru sana umerudi mikononi mwa watu wenye mpira wao, kina Shyrose Banji nakumbuka miaka mitatu iliyopita tumeshinda kwenye South Africa kushiriki wakati nafasi tumeipata. Tunaomba nao tuupe support.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho kabisa Mheshimiwa Waziri Chama cha Mpira wa Miguu wanawake, kwa kweli kwenye soccer kimataifa sasa hivi wanawake wanatubeba. Uchaguzi Mheshimiwa Waziri unajua ulisitishwa kimazongezonge na mimi huwa ni mtu honest niwaombe TFF, TFW muilee, msiiletee mazongezonge acheni wafanye uchaguzi wao. Figisu kwenye kile kitu si vizuri kama ningepata nafasi kwenye Maendeleo ya Jamii ningechangia hebu tuwanyanyue na wenyewe wanawake kwa sababu Mwenyekiti wa Chama cha Soka cha Mpira wa Wanawake pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, lakini saa hizi karibia mwaka wanakosa kule uwakilishi na sisi tunasema tuwawezeshe wanawake tutawawezesha nini kama hatutengenezi hiyo platform? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, itoshe kusema kwamba michezo ni zaidi ya burudani, nikazi, ni ajira but we have to be very serious Mama ametusaidia Royal Tour imetangaza nchi yetu na kupitia michezo, kupitia riadha, kupitia hawa watoto juzi, kupitia hawa watakaokwenda timu nne kimataifa tutaendelea kulitangaza Taifa letu lakini lazima tusaidie katika kutengeneza logistic, mambo ya protocol, mambo ya viwanja na mambo ya waamuzi na haya yote tukidhamiria inawezekana. Mungu Ibariki Tanzania, Mungi Ibariki Nchi yetu, Mungu wabariki viongozi wetu. Ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)