Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumshukuru Rais kwa kazi kubwa anayofanya katika kuisaidia sekta ya uvuvi. Pia nimpongeze Waziri na Naibu pamoja na uongozi kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichangie kuhusu zao la samaki ambalo wananchi wa maeneo ya maziwa na bahari wanategemea sana kwa kufanya biashara ya Samaki. Kwa vile samaki wanawategemea kufanya biashara naiomba Serikali iwawezeshe wavuvi kwa kuwanunulia vyombo vya kuvulia ili waweze kukuza zao hili, na wananchi waweze kukuwa kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nichangie kuhusu leseni kuwa inaleta changamoto katika maeneo ya pwani, hivyo niiombe Serikali iweke njia rahisi ya kupata leseni ili kuondoa changamoto hii ili wananchi waweze kufanya biashara hii na kujipatia kipato na kuongeza mapato katika Serikali yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wangu; katika kuudumisha Muungano wetu namuomba Waziri wa Wizara ya Uvuvi awe na mawasiliano mazuri na Wizara ya Uvuvi Zanzibar ili kuwafanya wavuvi wadogo wadogo kupata kipato na kuongeza uchumi wa nchi yetu na pia kuiunga mkono dhana ya uchumi wa buluu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.