Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Hon. Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri alifika jimboni kwangu Singida Kaskazini Kitongoji cha Mukulu, Kata ya Mughunga mwishoni mwa mwaka 2021 na kuwaahidi wananchi wa kitongoji hicho kuwa atawajengea josho la mifugo. Wananchi wale walifurahi sana kwa ahadi hii ya Serikali kwa sababu wanapata taabu sana kuogesha mifugo yao ukizingatia ni jamii ya wafugaji na maisha yao yote yanategemea mifugo.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumkumbusha Mheshimiwa Waziri kuhusu ahadi hii kwani wananchi wananikumbusha mara kwa mara na wanaisubiri huduma hii kwa hamu kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuishauri Wizara kuanzisha viwanda vya kusindika nyama. Ni muhimu sana kuanzisha viwanda maeneo ya Singida, Dodoma, Shinyanga, Arusha na maeneo yanayofuga ng'ombe kwa wingi ili kuongeza thamani ya mifugo yetu na kuweza kuuza nyama nje ya nchi hususan Visiwa vya Comoro ambavyo vinategemea sana nyama kutoka Tanzania badala ya kusafirisha ng'ombe walio hai, tuweze kusafirisha processed meet.

Pia ni muhimu kuanzisha viwanda vingi vya maziwa nchini, jambo hili litainua uchumi wetu na kuajiri vijana wetu waliopata mafunzo mbalimbali hususan katika fani husika ya uzalishaji, usindikaji, masoko na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kusisitiza sana suala la josho la mifugo kama alivyoahidi Mheshimiwa Waziri kwa wananchi wa Jimbo la Singida Kaskazini Kitongoji cha Mukulu ambacho hakina kabisa huduma hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja.