Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru tena kwa nafasi, nimesikiliza maoni yote ya Waheshimiwa Wabunge ambao wametoa na kwa upande wa Serikali.

Mheshimiwa Spika, Wabunge tuseme tuko hapa siyo kwa lengo la kupinga maoni ambayo Serikali imetoa na mpango wote ambao wameutoa. Waraka ambao Mheshimiwa Waziri aliutoa tarehe 23 Mei, 2023 kuelezea namna na mchakato ambavyo tunapaswa kutoa mazao nje ya nchi, mimi niseme unaonekana una tija kwa Serikali, una tija kwa wananchi wetu, lakini changamoto iko hapa tu, ametoa jambo hili ghafla sana, jambo hili amelitoa siyo rafiki kwa mazingira yetu.

Mheshimiwa Spika, kwenye Waraka wake ukisoma kwenye para ya kwanza roman number three amesema hivi “wafanyabiashara na wanunuzi hao wanatakiwa kuwa na nyaraka zote muhimu ikiwemo na utambulisho wa mlipa kodi - TIN, certificate of clearance, leseni ya biashara ambayo ni export license, namba za NIDA na wamiliki wa makampuni.

Mheshimiwa Spika, kwenye TASAF peke yake tukiwa hapa ndani watu wanakosa TASAF kwa ajili ya kukosa namba za NIDA. Iwe leo, yaani leo ndani ya mwezi mmoja mtu ataweza kupata namba za NIDA ili aweze kufanya hilo jambo, siyo uhalisia. Jambo ambalo Mheshimiwa Waziri amelileta ni rafiki lakini haliendani na mazingira.

Mheshimiwa Spika, biashara ya mazao ni biashara ya msimu, sasa hivi tunavyoongea Zambia imefunga mipaka yake kupeleka mazao ya chakula nchini DRC. Tafsiri yake sisi huku kwetu ni opportunity. Kwa hiyo, kama Mheshimiwa Waziri ame-raise haya mambo mapema hivi safari hii hatuwezi ku-meet hiyo demand ya soko la Congo.

Mheshimiwa Spika, ombi letu kwa Serikali tunaomba mambo haya yaanzishwe mwakani mwezi wa kwanza au kama Mheshimiwa Waziri yuko tayari jambo hili liendelee awe rafiki yeye kupitia Wizara yake aseme mambo yote haya kila kinachotakiwa mwananchi huyu au Mtanzania huyu anaweza akayapata ndani ya wiki moja ili aweze kuendana na hiyo demand ya wakati huo, yaani yeye Mheshimiwa Waziri awe kiungo kwenye hizo Taasisi nyingine.

Mheshimiwa Spika, kwa ridhaa yako naomba Mheshimiwa Waziri apelekewe hii document kwenye para la pili roman six ambapo anaongelea lazima upate export permit pamoja na phytosanitary certificates. Wameweka link hapa ya Wizara ya Kilimo ambayo unapaswa ku-apply kupitia mfumo.

Mheshimiwa Spika, mimi nimesoma IT degree yangu ya kwanza, ona vile system inavyoonyesha inaonyesha system iko under maintenance, sasa huyu mwananchi ata-apply kitu gani? Naomba mhudumu aje achukue ampelekee Mheshimiwa Waziri hili jambo labda yeye atufafanulie system yake inavyosema hivi inamaanisha nini? Inasemaje yaani huyu mwananchi wa kutoka Momba, kutoka kule Kalambo anapata nini hapa, hizo ndiyo permit ambazo tunaziongelea.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Haya sekunde 30 maliazia, kengele imeshagonga.

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nia ya Serikali ni njema lakini ndani ya muda mfupi wameweka masharti lukuki ambayo hata hao wafanyabiashara wetu au Watanzania wetu ambao tunawazuia wafanyabiashara kutoka nje bado hayawa-favor. Kwa hiyo, tukuombe Bunge litoe Azimio ili Mheshimiwa Waziri alegeze masharti kwa lengo la kuwasaidia wakulima. (Makofi)