Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja Kuhusu Bei ya Kuuza na Kununulia Mahindi

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza naunga mkono hoja hii. Uwazi na ukweli ni kwamba hadi tunavyoongea ni kwamba hadi tunavyoongea sasa NFRA hawajaanza kununua mazao mahali popote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi Wilaya ya Manyoni tunalo ghala ambalo NFRA wananunua mahindi, hakuna hata mtu mmoja wa NFRA pale, lakini wakulima wa Itigi, wakulima wa Mkoa wa Dodoma, wakulima ambao wanauza katika Soko la Kimataifa la Kibaigwa, mahindi yalikuwa yamefika katika bei nzuri sana. Leo kilo moja imeshuka zaidi ya nusu ya bei iliyokuwepo kutokana na zuio.

Mheshimiwa Spika, dhamira yetu ni nini? Tuna nia ya kuwasaidia wakulima wetu, nia ya kuwasaidia pembejeo lakini bado hazijafika. Sasa wanapofanya jitihada zao wanalima na wanunuzi wanakuja kununua mazao, leo tunapoweka zuio tunawadhulumu wakulima wetu. Naomba sana Serikali ione ni namna gani ya kutengeneza matajiri kutoka kwa wakulima wa nchi hii. Tusiwafanye wakulima ni watu dhalili, wakati wakulima wanatumia nguvu zao, wakati wa kuuza Serikali inaingilia kati. Kwa nini isifanye uwezeshaji mkubwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata kule mipakani kwa nini visitolewe vibali hivyo? Kama ni leseni nchi hii ni moja kwa nini zisitolewe leseni mahali popote, wananchi wakaomba leseni ilimradi awe na vielelezo vile kama TIN, Clearance na vile ambavyo ni vigezo vya biashara? Tunaomba Serikali irahisishe ufanyaji wa biashara katika maeneo mengi hususani katika kilimo. Wakati Serikali hainunui mazao, basi wale wangeweza kununua. Sasa hivi wananchi baada ya kulima, uhitaji ndio unakuwa mkubwa, wanataka kupeleka watoto wao shule, wanataka... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa ahsante sana, kengele imeshagonga.

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja kwa mara nyingine. (Makofi)