Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, kutokana na ufinyu wa muda nimeshindwa kusema mengine ambayo nilitamani niyaseme katika mchango wangu katika bajeti ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Maliasili na Utalii bado kuna tatizo la mpaka kati ya ANAPA na Kitongoji cha Momela na eneo lenye mgogoro lilikuwa sehemu ya mashamba Na. 40 na 41 na ukubwa wake ni ekari 604. Walikuja kwangu akina mama kutoka eneo husika wakilia na kulalamika wameolewa na kuishi eneo hilo kwa takribani miaka wamezaa na watoto wao kuolewa na sasa wanaambiwa wahame bila kuelekezwa waende wapi na Meru hakuna tena ardhi iliyo wazi.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Rais kwa huruma yake kama mama aruhusu wananchi wale waendelee kuishi kwenye makazi yao hata kama ni kwa masharti ya kihifadhi kama WMA.

Pili ni kuhusu Ujenzi na Uchukuzi; ahadi za Rais; Arumeru Mashariki tuna ahadi kadhaa za viongozi wakuu ambazo hazijafanyiwa kazi; kwanza barabara ya Kingori kuanzia Malula Kibaoni hadi Ngarenanyuki kujengwa kwa kiwango cha lami ni moja ya ahadi alizotoa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa mwezi Oktoba, 2020 pale Usa River mbele ya maelfu ya wananchi wa Arumeru. Nakumbuka Mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan - Rais wa Awamu ya Sita katika hotuba yake kwa Baraza lake la Kwanza la Mawaziri aliahidi kutekeleza yote yaliyokuwa kwenye mipango ya mtangulizi wake aliyerehemika akiwa kazini ikiwa ni pamoja na ahadi zote alizotoa kwa Watanzania, naomba tamko la Serikali kuhusu ahadi hii.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.