Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Mungu kwa uweza wake na napenda kumpongeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kwa kazi kubwa na nzuri inayoendelea kufanyika na hata zile alizoziibua kwa miaka hii miwili yote inaendelea kwa kasi sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa pongezi kwa jopo la Mawaziri wote na Naibu Mawaziri kwa kuungana na Rais Samia na Makamu wa Rais Mheshimiwa Mpango na Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa katika kuendeleza mpango mzima wa kuendeleza nchi yetu. Kazi Iendelee.

Mheshimiwa Spika, naomba kuzungumzia jambo la VAT kuongezwa kiwango ndio itapelekea ukwepaji wa kodi na pia ndio inaleta kufanya mazungumzo kati y muuzaji na mnunuzi ya na risiti au bila ya risiti bila kuwa na uelewa wa ukusanyaji VAT bado ugumu wa ukusanyaji wa VAT utakuwa mgumu.

Mheshimiwa Spika, hapa tuangalie zaidi kuongeza wafanyabiashara, ni lazima kuhakikisha wigo unaongezeka ili kuhakikisha idadi ya walipakodi inaongezeka.

Mheshimiwa Spika, katika ukurasa wa 70 wa hotuba ya Waziri wastani wa walipakodi kulingana na ukuaji wa wananchi na ongezeko la mahitaji kwa mwaka 2021/2022 walipakodi waliosajiliwa ni 4,455,028 lakini wenye TIN kati yao ni 1,641,173 ndio maana wafanyabiashara wengi wanakwepa TIN kwa kuona ni usumbufu wa tozo za Serikali.

Mheshimiwa Spika, niiombe Wizara iangalie mfumo mzuri wa malipo, kuwe na sheria inayosimamia malipo yaani angalau kuwe na muda maalum wa malipo kwa Serikali mfano malipo ya SDL/PAYE/WCF/Mifuko ya Jamii/VAT na kadhalika. Pia iwepo tarehe maalum kila mwezi na usipolipa kwa muda kuwe na riba adhabu italipwa na muhusika wa kampuni iliyochelewesha malipo ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, mwisho niishukuru Serikali yangu kwa miradi yote waliyoleta jimboni Temeke; vituo vya afya, shule za ghorofa, barabara za TARURA na kadhalika, lakini zaidi sana Mradi wa DMDP unaokwenda kuanza mwezi wa Aprili, 2024.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Temeke tunamshukuru sana Rais na wasaidizi wake wote, Mungu Ibariki Tanzania Kazi Iendelee.