Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

Hon. Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza miaka miwili ya uongozi wake makini unaoleta mageuzi makubwa kielimu, kisiasa, kijamii katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pia nampongeza Waziri wa Fedha kwa kazi kubwa anayoifanya pamoja na Naibu wake na watendaji wake kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, mimi mchango wangu nauelekeza kwenye mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuangalia sekta mbalimbali. Nampongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maendeleo anayozidi kuyatoa kwani shilingi bilioni 1.0 zimewekwa kwenye mfuko wa walemavu kwa ajili ya kusaidia vifaa vinavyohitajika, pia fedha hizo zitatumika kwa Mfuko wa Wabunge wa Kundi la Watu Wenye Ulemavu mchango kwa watoto wanaolelewa kwenye vituo maalum.

Mheshimiwa Spika, tunaomba makampuni binafsi kuchangia mfuko huu kwa kusaidia makundi haya maalum pamoja na programu zinazotolewa chini ya TASAF.

Mheshimiwa Spika, kuhusu elimu naipongeza Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan kwa kutengeneza jambo la kihistoria kwa kuwafutia ada wanafunzi wa kidato cha tano na sita na kufanya wasome kwa utulivu.

Mheshimiwa Spika, Serikali imetenga fedha ya kugharimia programu hiyo ambapo hadi mwezi Aprili, 2023 jumla ya shilingi bilioni 661.9 zimetolewa. Pia kutokana na mabadiliko ya Sera ya Elimu ya mwaka 2014 Toleo la mwaka 2023 na mabadiliko ya mitaala yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita Serikali imepanga kutoa elimu ambayo itamuwezesha mwanafunzi kujiajri au kuajiriwa.

Mheshimiwa Spika, pendekezo la Mheshimiwa Waziri wa Fedha kuhusu kuondolewa kwa ada ya wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne na kupangiwa na Serikali kujiunga vyuo vya ufundi vya Dar es Salaam Institute, DIT, MUST na ATC ili kuongeza idadi ya wataalam wenye ujuzi na elimu inayohitajika katika zama hizi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uzalishaji; ongezeko la bajeti ya kilimo kutoka shilingi bilioni 294.0 mwaka 2021 mpaka shilingi bilioni 954.4 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 na kufikia shilingi bilioni 970.8 kwa mwaka wa fedha 2023 ongezeko hilo limesababisha upatikanaji wa pembejeo za kilimo na kuanzishwa kwa Mfuko wa Maendeleo ya Kilimo na kuanzishwa kwa mashamba makubwa ya pamoja.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali imeendelea kusimamia usalama wa chakula kwa kujenga maghala 16 na vihenge 20 kwa ajili ya kuhifadhj mazao.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.