Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kwanza nimshukuru Mbunge mwenzangu kwa kunipa nafasi hii ya dakika tano, lakini naomba pia nianze kwa kumpongeza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano pamoja na Uchukuzi kwa hotuba yake nzuri. Mimi naomba niongee suala moja ambalo hili limekuwa ni tatizo kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba sana Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa kampuni hii ya kuhodhi mali ya reli (RAHCO) iliundwa kisheria atuletee muswada hapa Bungeni ili tuweze kufanya marekebisho waweze kuungana. Kuna tatizo kubwa sana la hii RAHCO. RAHCO ni moja ya tatizo katika uendeshaji wa Shirika la Reli Tanzania na ushahidi upo. Hawa RAHCO ndiyo waliokuwa wanauza hata mabehewa yale ambayo waliuza kwa chuma chakavu ni hawa RAHCO. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine, kuna tatizo la conflict of interest (mgongano wa maslahi) kati ya RAHCO na TRL unafanya lile shirika lisiende vizuri. Naomba labda nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba achunguze vizuri ile Godegode imesemwa sana na Gulwe; yale mabilioni yanayopelekwa pale kila siku na RAHCO yanakwenda wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, TRL inashikilia reli, inaangalia reli na kinachopita juu ya reli. RAHCO wao wanaangalia reli tu, wafanyakazi karibu asilimia 95. Hata wa RAHCO wenyewe wako Shirika la TRL kwa hiyo, ili kuondoa huu mgongano wa kimaslahi haya makampuni ni vizuri yaunganishwe. Naomba Mheshimiwa Waziri atakapokuja kufanya majumuisho kesho kwa kuwa huu pia ni msimamo wa Kamati ya Miundombinu kwamba haya Mashirika yaunganishwe aweze kutupa majibu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine kuna suala la mishahara. Hawa RAHCO ndiyo wanapelekewa pesa zote na wanajilipa mishahara mikubwa kweli kweli tofauti na TRL, wakati uendeshaji wao ulikuwa mmoja, hata Mheshimiwa Rais ameongelea sana hili suala la mishahara kupita kiasi kwa watu ambao wanafanya kazi zinazofanana. Sasa lile suala la kwamba RAHCO wana hodhi kila kitu lina matatizo sana. Kwa hiyo, ningeomba hii kama tulivyokubaliana hata kwenye Kamati ya Miundombinu, ulete muswada wa kuirudisha RAHCO pamoja na TRL. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine kuna mkataba ule wa mwaka 2014 ambao ulikuwa umesainiwa kati ya Afrika Kusini na Tanzania kuhusu kutengenezwa vichwa kumi na moja vya treni. Vichwa tisa viko tayari, sasa ningemuomba Mheshimiwa Waziri sijui hili suala la kulipia vile vichwa tisa, tulipata taarifa ni karibu shilingi bilioni 57 zinatakiwa ili waweze kulifanyia hilo, lakini pia maslahi ya Wafanyakazi ambayo yanafika karibu 7.5 au 6 billion; malimbikizo ya madai yao mbalimbali; haya yanaleta migogoro kila mara katika Shirika la Reli Tanzania.
Naomba Mheshimiwa Waziri wakati unajumuisha majumuisho yako na hili uweze kuliona, ni moja ya matatizo ambayo kila mara yanaleta migogoro katika Shirika letu la Reli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia naomba nizungumzie suala katika…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga Mkono hoja.