Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge Kuhusu Pendekezo la Kuridhiwa Mkataba Baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwa Lengo la Kuanzisha Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii katika Uendelezaji wa Maeneo ya Bandari Nchini

Hon. Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge Kuhusu Pendekezo la Kuridhiwa Mkataba Baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Dubai kwa Lengo la Kuanzisha Ushirikiano wa Kiuchumi na Kijamii katika Uendelezaji wa Maeneo ya Bandari Nchini

MHE. DKT. LEONARD M. CHAMURIHO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii kuweza kuchangia hoja hii muhimu ambayo imewekwa mbele yetu.

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze na preamble ya haya makubaliano tukiangalia ile ya kwanza kabisa chimbuko ni ziara ya Mheshimiwa Rais alipokwenda kule Dubai. Kwa hiyo, kwa ziara hilo tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kututafutia rasilimali za kuweza kuendeleza miundombinu ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, katika preamble hiyo hiyo kifungu cha pili kinaongelea chimbuko lingine ambalo ni maombi ya TPA na DP World. Ningependa kuwapongeza Wizara pamoja na TPA kwa kuweza kufahamu udhaifu uliokuwepo TPA na kutafutia changamoto cha kuweza kutatua.

Mheshimiwa Spika, kwa wengi wanaweza kuwa hawafahamu kwa nini hawa waliweza kumtafuta mwekezaji mahiri. Nitatoa mifano mitatu ambayo itaonesha ni kwa nini unahitaji mtu mahiri ili uweze ku-deal na hivi vitu vikubwa vikubwa.

Mheshimiwa Spika, mfano wa kwanza tulitaka kununua spare za engine za TAZARA zinaitwa tracks and motors, tulipotoa ile order tuliambiwa tunaweza tukaipata baada ya miaka mitatu na kosa letu lilikuwa ni moja tu kwamba sisi tulikuwa niwaagizaji wadogo, hatuwezi kuweza kuitoa design team ya wale manufacturer wahame watutengenezee sisi kitu kidogo, kwa hiyo tutakwenda baada ya miaka mitatu.

Mheshimiwa Spika, mfano wa pili ambao nitautoa kwa nini tunahitaji wawekezaji mahiri, ni pale tulipoagiza vichwa vya treni. Tulipoagiza vichwa vya treni tulipata changamoto moja kubwa, klila ukiagiza unaambiwa kwamba order yako ni ndogo mno kuweza kuhamisha design team yetu ikafanya kazi yako ili upate hiyo order yako. Kwa hiyo, unajikuta unawekwa kwenye foleni ya miaka mitatu au minne mbele na ikitokea changamoto yoyote unasukumwa mbele zadi? Ni kwa sababu ni mdogo.

Mheshimiwa Spika, mfano wa tatu ambao ningependa kuutoa utahusu bandari wenyewe. Katika hayo maendelezo ya bandari yaliyofanywa sasa hivi tuliagiza hizo sea to shore gantry ambazo ni crane ambazo zinatumika pale. Tulipata muda ambao ni wa miaka mitatu mbele, kosa letu moja tu ninyi ni wadogo mno kuweza kutoa hiyo order mkapata moja kwa moja. Kwa hiyo, inabidi uwe una mwekezaji mahiri ambaye akiagiza order yake ni order kubwa ambayo itasababisha uweze kupata hiyo order. (Makofi)

Sasa huyu mwekezaji mahiri kama tulivyoambiwa amewekeza kwenye bandari nyingi sana. Kwa hiyo, hata kama akitoa order yake ni kubwa, kwa hiyo uwekezaji wake unakwenda moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile katika uendeshaji huu vifaa hivi huharibika, vinapoharibika tunapambana na changamoto hiyo hiyo kwamba unapoagiza vipuri na wewe ni mtu mdogo unaingia kwenye foleni ndefu sana, imeharibika crane yako moja unataka upate hicho kipuri unaambiwa kipuri chako utakipata baada ya miaka mitatu. Sasa huwezi kuwa unasubiri hapo na wenzako wanapata vipuri kwa sifa moja tu, kwamba wao order zao ni kubwa kwani ni wakubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa nataka kuchukua fursa hii kuwapongeza Wizara kupitia TPA kwamba kwa kutafuta mwekezaji mahiri ili aweze kutuboreshea bandari zetu ili tuweze kupata uendelezaji wa haraka.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu wa tatu utaenda kwa wale waliojadili huu mkataba. Kama ilivyojieleza katika preamble pale, sisi tulikwenda kuomba kusaidiwa. Sasa unapoenda kuomba katika majadiliano huwa uko kwenye weaker position, lakini unaona kwamba katika majadiliano haya hawa waliojadiliana wameweza kabisa kutuletea mfumo mzuri kabisa ambao unaweza kutuondolea changamoto hii.

Mheshimiwa Spika, mfumo waliouweka ambao unaanzia IGA unatoka kwenye IGA unakuja kwenye Host Government Agreement ambayo ni kwamba mnajadiliana Serikali itampa nini mwekezaji, lakini wa tatu tutakwenda kwenye land lease ambayo utampangisha mwekezaji ili apate sehemu ya kufanyia biashara na mwisho ni hiyo concession agreement, ni mfumo ambao ni mzuri ambao unaweka hatua mbalimbali ambazo zinaweka. Kwa hiyo, ningependa kuchukua hatua hiyo kuwapongeza hao ambao waliweza kufanya hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile pongezi ambazo ninawapa hao ni kuweza kuweka mikataba ijadiliwe wakati ule ambapo inapotakiwa. Hili litawezesha hawa watakaojadili hiyo mikataba inayokuja kuweza kuangalia changamoto za nyuma ambazo tulikuwa nazo na kuweza kuzichukulia katika mukhtadha wakati uliopo. huu nao ni mtindo mzuri sana ambao inabidi tuwapongeze katika hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano ukiangalia kifungu cha nane ambacho kinaongelea ardhi, maana yake ni kwamba wameweka kwamba kwa sababu kitajadiliwa kwa sheria za kwetu kitajadiliwa kwa mukhtadha wa sheria zilizopo. Ukiangalia kwenye kifungu cha tisa, vivutio; vivutio wamesema vitawekwa kulingana na sheria za kwetu, kwa hiyo kwa sababu wameviweka vitajadiliwa kule mbele, jukumu letu ni kuangalia hizi hofu za Watanzania na kuziingiza katika ile mikataba kama vizuizi hatarishi ambavyo tunavilania. Kwa hiyo, hizi hoja ambazo zinatolewa na hofu za wananchi nashauri tu kwamba Serikali izichukue ili ziweze kuingia katika majadiliano hayo tuweze kupata kilicho bora ambacho Watanzania wote wanakitaka.

Mheshimiwa Spika, vilevile ningependa kuwapongeza kwa kuweza kulinda ajira za Watanzania. Katika miradi hii mikubwa huwa kuna mvutano mkubwa sana katika kulinda hizi ajira. Ukichukulia mfano wa mkataba wa SGR kwa wafanyakazi wa kawaida asilimia 80 wanatakiwa wawe Watanzania na asilimia 20 ndio wawe wageni. Hiyo ni ratio nzuri tu na kwa wale kwa upande wa management asilimia 20 wanakuwa Watanzania, asilimia 80 watakuwa wa kwao.

Kwa hiyo, hii ni mifano ambayo imeangaliwa huko nyuma na sasa hivi inaweza ikaangaliwa vizuri zaidi katika mikataba inayokuja. Kwa hiyo, tuwapongeze hawa kwa kutuwezesha kuruhusu tujadili mikataba hii mbele ili tuangalie huko nyuma tulivyofanya na tuweze kuboresha kwa kadri ambavyo tutaona inafaa.

Mheshimiwa Spika, sitakuwa nimetenda haki bila kuongelea machache ya hofu. Napenda kujadili hofu ambayo imejitokeza katika majadilano huko nje.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Mheshimiwa kengele ya pili imeshagonga. Ahsante sana.

MHE. DKT. LEONARD M. CHAMURIHO: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)