Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Mapitio ya Hali ya Uchumi wa Taifa 1.3.1. Pato la Taifa na Ukuaji wa Uchumi katika kipindi cha Januari hadi Septemba, 2022, Uchumi wa Taifa ulikua kwa wastani wa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 4.8 katika kipindi kama hicho mwaka 2021. Ukuaji chanya wa uchumi ulichangiwa na jitihada mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ikiwemo mikakati ya kukabiliana na athari za vita kati ya Ukraine na Urusi; ruzuku kwenye mafuta shilingi milioni 100 kila mwezi, uwekezaji wa kimkakati katika miundombinu ya nishati (trilioni 6.55 limefika 86.89%), maji (trilioni 1), afya (trilioni 1), elimu, barabara, reli na viwanja vya ndege; kuongezeka kwa uzalishaji wa madini, hususan dhahabu na makaa ya mawe na kuongezeka kwa mikopo katika sekta binafsi ambayo imechochea shughuli za kiuchumi.

Aidha, ukuaji huu ulichangiwa na kuongezeka kwa shughuli za utalii kutokana na kampeni ya Royal Tour. Ukuaji huu wa uchumi unaashiria kuimarika kwa shughuli za kiuchumi katika sekta mbalimbali pamoja na kuongezeka kwa ajira na mapato ya ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, mambo matatu ambayo yatasababisha Watanzania kuhamisha uwanja wa vita; kwanza Bureau De Change - BoT/masharti ya kuanzisha Bureau De Change yawe rahisi ili kurahisisha upatikanaji wa dola nchini na kukuza utalii; pili, madeni ya kodi za muda mrefu - TRA lifanyiwe kazi; tatu, gawio kwa Watanzania kwenye makampuni ya hisa- kama Vodacom wafuatiliwe ili wawe wanatoa gawio.

Mheshimiwa Naibu Spika, madaraka ya Kamishna ni makubwa mno kiasi cha kukiuka haki za binadamu na baadhi ya sheria hasa Kamishna akiwa negative thinker.

Mheshimiwa Naibu Spika, machinga wa Iringa waliahidiwa na Rais fedha zao shilingi milioni 700; tunaomba Wizara ya Fedha itoe.

Kuhusu utoaji maamuzi chanya kwa viongozi wa juu wa taasisi unazoziongoza uko chini sana, wawe wanatoa maamuzi mapema na kwa wakati ili kuepusha migogoro kama migomo na kufifisha uzalishaji kwa wananchi; kupuuza maagizo ya viongozi ikiwemo Mheshimiwa Rais, mfano kutotoza kodi za miaka ya nyuma na ya muda mrefu, kutorudisha fedha za Bureau De Change na kusingizia Bunge na vyombo vingine vya sheria waache. Wawajibike! Nia ovu isiwepo kama ku-seize fedha za Community Banks kama Mucoba bank milioni 600, ni kutowatendea haki wananchi.