Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa fursa hii ya mimi nihutubie pia Taifa kidogo. Kusema kweli wanahitaji pongezi nyingi uongozi wa Wizara lakini zaidi Mheshimiwa Rais ambaye amewezesha fedha kupatikana na Wizara zote zikapata fedha kwa uwiano uliokuwepo mzuri zaidi ya kama alivyosema mwenzangu Mheshimiwa Komanya zaidi ya asilimia 80 Wizara zimepata mpata mpaka hadi Aprili ambaye ni ndugu yangu mzuri na nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Nampongeza pia Mheshimiwa Rais kwa kuweza kupangua wakurugenzi wa halmashauri zetu hiyo ni njia moja ya kupunguza maficho ya ufisadi. Kwa hiyo, nashukuru kwamba amefanya hilo naamini litasaidia na naamini kwamba Wizara nyingine hasa ile Wizara ya Ardhi itaanza na yenyewe kutafuta namna ya kupangua maafisa ardhi kwenye mikoa na kwenye wilaya zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo niseme kidogo kwamba nashangaa Mheshimiwa Kishimba anapata wapi hizo hoja zake anaziibua kutoka wapi lakini nimefurahi hoja zake zimenifurahisha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kwa vile Wizara imeweza kulipa madeni vizuri sana, karibu madeni yote yamelipwa kwa wakati ningeomba niseme kwamba kuna suala la madeni ya fidia, madeni ya fidia hayaonekani kwenye vitabu ni contingency liabilities lakini yapo hayo madeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna madeni kwa mfano kule kwangu Vunjo wakazi wa Eneo la Chekereni, Njia Panda ambako wanajenga kituo cha one stop center ya customs pamoja na kule Uchira toka mwaka 2013 wanadai zaidi ya bilioni 10 na hawajalipwa. kwa hiyo, naona niwa-dominate Waziri alichukue na hilo najua kwamba siku ya karibuni walifanya tathmini upya na naamini zile dhamana zilizokuwa zimepatikana miaka ile wataongezewa fidia yao inavyostahili kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, langu la pili linahusu vyuo vilivyo chini ya Wizara ya Fedha na vingine vipo chini ya Wizara ya Biashara, vyuo ambavyo viliundwa kwa mantiki ya kutengeneza au kutoa skills kwa waliomaliza shule ili waweze kuingia kwenye kazi moja kwa moja. Kwa mfano IFM tulijua kwamba ilikuwa diploma, advanced diploma na post graduate diploma na zingine zilikuwa hivyo hata Mzumbe lakini baadaye hata CBE nayo ilianza sasa kuwa kama university lakini mantiki yake ilikuwa ni vyuo vya kati ambavyo vitataengeneza watu wenye study kwenye fani husika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wamebadilisha kabisa hiyo dira iliyokuwepo toka mwanzo na wameingia sasa kuwa ni vyuo vikuu na kwa bahati mbaya na kwa sababu hiyo utaona kwamba pia hivi vyuo havi-publish nyaraka ambazo za kitafiti ambazo zinaongeza nanii duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi nafikiri hivi vyuo haviko mahali pake. Kwa sababu sasa tumeshabadilisha ile dira tunafikiri vyuo hivi virudi kwenye Wizara ya Elimu ivisimamie kama inavyosimamia vyuo vile vingine vyote, lakini kukaa kwenye Wizara hizi havipati usimamizi unaostahili na ninaamini ndiyo sababu tunaona hata kwenye vyuo elimu inaporomoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nizungumze suala la Kitengo cha Mkaguzi Mkuu lakini naona limeshazungumziwa vya kutosha. Lakini kuna hoja pia zingine nitazungumza; hoja ya kwamba tutenge fungu la contingency la dharura kwenye bajeti (Mfuko wa Dharura kwenye Bajeti). Ni jambo ambalo liko kwenye constitution kwenye katiba na pia ni hitaji la Sheria ya Bajeti. Hatujaweza kufanya vile na mimi nasema kwamba silaumu na mimi nina hoja yangu binafsi, nasema ukianza kutenga fedha kwenye Mfuko wa Dharura unaweka akiba kwa tatizo litakalokuja na unaweza kufanya vile kama una bajeti ambayo haina nakisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti zote tangu tupate uhuru zimekuwa ni bajeti ambazo zina nakisi kubwa ndiyo sababu tunakwenda kukopa na kuomba wahisani na kadhalika. Endapo tutasema tunatengeneza mfuko wa dharura ukienda kwa mhisani atakwambia kwamba kula kwanza uliyoweka akiba ndipo nikupe mimi; kwa hiyo hatakupa na misaada itapungua na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naamini hapo tutakapofikia uwezo wa kuwa na bajeti ambayo ni surplus budget basi tunaweza kuzungumzia suala zima la kuweza kuweka fedha kwenye mfuko wa dharura ambao unahitajika bahati nzuri sasa hivi tunajua kwamba unatenga shilingi bilioni 100 ambazo zinaweza zikatumika wakati wowote, lakini sheria inataka mfuko kamili ambao utakuwa unakuzwa na wenyewe uwe na kanuni zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapongeza sana kwamba tumeanza kutengeneza dira ya 2050. Ninaamini ni jambo jema lakini mimi nilikuwa nafikiri huwezi kutengeneza dira kabla hujafanya tathmini ya ulikotoka, ulipo ndipo uweze kusema ninaenda wapi. Naona kwamba hatujaweza kufanya hiyo tathmini. Tunaambiwa tathmini imeanza kufanyiwa kazi lakini nilishangaa kwamba tumeweza kufungua. Of course, tulizindua mchakato huu wa kutengeneza hii dira lakini bahati mbaya naona kama itakuwa siyo vizuri kama hatujapata tathmini nzuri au hata wale waliopewa kuifanya hiyo kazi watafutiwe kwa upesi sana tathmini hiyo ikamilike ili waweze kutumia na kuelewa ni wapi tumetoka na tumejifunza nini kutokana na utekelezaji wa dira ya 2025. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka pia niseme kwamba mimi naunga hoja mkono, ahsante sana. (Makofi)