Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi hii niweze kutoa maoni yangu kwa hoja iliyopo mbele yetu. Naomba nianze kwa kuunga mkono hoja Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Fedha lakini pamoja na maoni ya Kamati ya Bajeti ambayo ni mmoja wa Wajumbe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri anazofanya ikiwepo kurejesha nyongeza ya mshahara wa watumishi annual increment hii ni faraja kubwa kwa watumishi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Waziri Dkt. Mwigulu Nchemba na Naibu wake na wataalam wote waliopo chini ya Wizara ya Fedha, kwa kweli kazi nzuri wanafanya katika kutekeleza majukumu yao lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kuendelea kulipa madai ya watumishi na watumishi wanafurahi. Nimewauliza wakasema hawana changamoto zilizopo ni ndogo ndogo lakini kubwa kurudisha on call allowance, kwa sabbau tunatambua kwamba watumishi wetu ni wachache. Mtumishi mmoja wa afya anafanya kazi ya watumishi ambayo ingefanywa na watumishi watatu, hivyo kurudisha on call allowance ni faraja sana kwa watumishi wetu. Lakini nikupongeze kwa namna mnavyolipa madai ya wakandarasi, madai ya watumishi, kwa hiyo, hata uchumi wa Nchi unaendelea kuwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kushukuru kwa Mheshimiwa Waziri katika majukumu ya Wizara ya fedha niongelee jukumu moja ambalo amelifanya vizuri na sisi wote tunaona kuhusu kuratibu upatikanaji wa fedha kutoka taasisi za fedha za kikanda na za kimataifa kwa ajili ya kutekeleza bajeti ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika katika miaka ya nyuma upelekaji wa fedha hususan fedha za maendeleo katika halmashauri za Serikali za mitaa ulikuwa chini kabisa. Hadi kumaliza mwaka ni asilimia 30 au 20 ya miradi ya maendeleo ndio iliyokuwa imepelekwa lakini sasa tumeona wote ni mashahidi na zaidi ya asilimia 90 na wengine kuvuka malengo na wengine kuletewa fedha ambazo hazikuwa kwenye mfumo wa bajeti ya halmashauri za wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nishukuru wengi tunaona wananchi wanaona miradi inatekelezwa katika halmashauri zetu kila kata ukienda, kila kata watumishi wako bize kutekeleza miradi ya maendeleo. Huu ni ushahidi tosha kabisa katika Wizara ya Fedha kwa awamu hii upelekaji wa fedha katika ngazi za chini unaendelea vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mapato mengi yanatumika pia yanatumika pia mapato ya ndani. Nishukuru tunatumia fedha zetu wenyewe kupeleka kutokana na tozo mbalimbali lakini niipongeza TRA kwa mwezi Desemba ilivunja rekodi ya makusanyo ambayo ilikusanya trilioni 2.7 ambayo haijawahi kutokea. Niombe tuendelee kuwatia moyo watumishi wa TRA pamoja na Kamishna. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niongelee na niipongeze Serikali kwa kutumia mifumo yetu wenyewe iliyotengenezwa na wataalamu wetu. Kiupekee nimpongeze Mkurugenzi wa Mifumo wa TAMISEMI, nimpongeze Mkurugenzi wa Mifumo wa Hazina lakini niombe sasa, niishauri Serikali tuendelee kuwajengea uwezo, tuendelee kuwapa motisha ili waweze kufanya kazi vizuri, kwa sabbau wameokoa fedha nyingi za kigeni ambazo tulikua tunatumia kulipa mifumo iliyotengenezwa nje lakini mifumo hiyo inatengenezwa na wataalamu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sikuchangia TAMISEMI, naomba niongelee maboresho katika ukusanyaji wa mapato ya halmashauri kwa kuboresha Mfumo wa LGRCIS na kuupa jina la Tausi. Ni ukweli usiopingika katika mfumo uliokuwepo wa POS mapato ghafi mengi yalikuwa yanapotea kabla ya kufikishwa benki. Fedha nyingi zilikua zinakusanywa na kutumia kabla ya kufika benki na hivyo kupunguza mapato ya halmashauri husika. Lakini sasa kwa kutumia Mfumo wa Tausi niipongeze TAMISEMI kutakuwa na udhibiti wa mapato ghafi kwa kutumia matumizi ya zuio la kiwango katika ukusanyaji ambayo ni float management. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe ushauri wangu kwa kutumia mfumo huu wa float management, nina uhakika sasa ule wasiwasi uliokuwepo wa halmashauri kumpa wakala chanzo kwa kuhofu kwamba atakusanya mapato mengi yasifike halmashauri na yeye akanufaika. Sasa tatizo hili linaenda kutatuliwa na float management kwa kuwa wakala yule atatoa kwanza fedha ambazo alitakiwa kulipa aikusanye, ikiisha anapewa nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika niiombe Serikali, niwaombe watumishi wetu waongeze umakini katika kutumia mfumo huu kwa sababu kwa kutumia float management sasa halmashauri inaweza ikafanya tathmini ya chanzo kimoja baada ya kingine. Niwaombe wakala anapofikia kile kiwango ambacho alitakiwa kulipa mwisho wa mwaka, basi tusifanye udanganyifu wa kukusanya mapato nje ya mfumo, tumuache akusanye mpaka mwisho wa mwaka na itatupa dira ya kiwango kwa kila chanzo kinachotakiwa kukusanywa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na hii itasaidia sasa kuondokana na tatizo lile la underestimate na niombe sasa niombe Serikali kwa kutumia mfumo huu basi ipo haja sasa baadaye watumishi wetu wajitoe katika kukusanya mapato ya halmashauri, tuwaachie mawakala kama mfumo huu utatumika ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naunga mkono hoja.