Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, kuhusu utalii Kanda ya Kusini (REGROW), utekelezaji wa mradi huu umesaidia kuboresha miundombinu katika hifadhi na utatuzi wa migogoro.

Mheshimiwa Spika, naomba kuipongeza Wizara hii kwa kazi kubwa ya kukuza utalii na maliasili zetu. Pongeza pia za kipekee zimuendee Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mchango wake binafsi katika kuendeleza Wizara hii kupitia Royal Tour.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika kujenga kituo cha Utalii Kusini chini ya REGROW kiitwacho Kihesa-Kilolo ambacho kinatakiwa kujengwa katika Manispaa ya Iringa ambalo ni lango la utalii Kusini. Umuhimu wa vituo hivi vya kitalii duniani ni kutoa taarifa na elimu kwa watalii kuhusiana na mwelekeo au ramani ya eneo husika ambalo mtalii anatakiwa kutembelea, kutoa taarifa ya huduma zilizoko katika eneo hilo la utalii, ni sehemu inayomuunganisha mtalii na eneo la utalii. Hivyo basi, ni lazima tukubaliane kuwa pamoja na uboresha mbalimbali unaofanyika kwenye mbuga na hifadhi zetu, bado tujue ni muhimu sana kuwa na kituo cha utalii au information centre ambacho ni Kihesa Kilolo.

Mheshimiwa Spika, Kituo hiki kitatakiwa kutoa taarifa za Utalii Kusini yote, sio Iringa pekee yake. Utafiti unaonesha ili tufikie lengo la Ilani yetu ya kufikia watalii milioni tano ifikapo mwaka 2025; basi ni muhimu kujenga kituo hiki. Sababu ni kwamba huwezi kupeleka watalii wote hawa Kaskazini, utaharibu kabisa ikolojia ya utalii wenyewe Kaskazini. Tabia za watalii hutaka kupata taarifa mapema kutoka kwenye vituo hivi kabla hawajaanza safari ya kutembelea eneo husika. Sasa kwa wale wanaotaka kuja Kusini wanapata taarifa wapi?

Mheshimiwa Waziri, msiseme tu muda unaturuhusu mpaka mwaka 2025, utakuwa unaenda kinyume na Mpango wa Miaka Mitano na Ilani ya CCM, inayotutaka tuongeze pato la Taifa. Mchango wangu namba mbili, moja ya sababu kubwa inayowafanya watalii kutorudi nchini ni kukosekana kwa huduma bora muhimu ikiwepo, kupatikana kwa fedha za kigeni. Mheshimiwa Waziri fanya jitihada zako binafsi bila kuwategemea Wizara ya Fedha kuhakikisha, maduka ya fedha za kigeni yanarudishwa nchini, hasa maeneo ya utalii. Pigania Wizara ya Fedha kupitia BOT waondoe masharti yasiyokuwa rafiki yanayosababisha maduka ya kubadilishwa fedha za kigeni yasiwepo.

Mheshimiwa Spika, tatu, Iringa Mjini kama lango au reception ya Utalii Kusini, lazima sasa tukuombe Mheshimiwa Waziri kuweka msukumo mahsusi wa kuwaandaa watu wa Iringa kuwa wakitalii. Mamlaka za Iringa kuwa kitalii, mazingira ya Iringa kuwa kitalii ikiwemo kuhakikisha misitu ya asili inalindwa kwa kushirikia na programu za TFS, kama kupanda miti, kutunza miti ya asili, kutoa mizinga ya nyuki ili kupunguza ukataji wa miti hovyo kuifanya Iringa kwa Southern Geneva); ikiwemo kuanzisha zoo, hili mimi mwenyewe naweza kusaidia.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri atakapo wind-up atoe kauli thabiti amejipanga vipi kuwafanya watu, viongozi, mji wa Iringa, mazingira ya Iringa kuwa ya kitalii (Southern Geneva of Africa). Naunga mkono hoja naomba kuwasilisha.