Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi kubwa inayofanyika, nashauri yafuatayo; kwanza, miundombinu kuelekea kwenye vivutio vya utalii ni mibovu sana kiasi cha kukatisha tamaa watalii kuvitembelea; pili, Ukerewe kuna vivutio vingi kama jiwe linalocheza la Nyabulebeka, fukwe za Rubya, mapango ya Handebezyo na vingine vingi, lakini hakuna mfumo maalum uliopo kwa ajili ya kuvitangaza.

Mheshimiwa Spika, nashauri wataalam wa Wizara watembelee Ukerewe na kukaa na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ili wapate masada wa kitaalamu katika sekta ya utalii ili vivutio hivi vilinufaishe Taifa na jamii ya wananchi wa Ukerewe.