Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Spika, naomba kumpongeza Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa maandalizi ya hotuba nzuri, lakini zaidi kwa kuwa open minded, nimepata wasaa wa kuzungumza na Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu kuhusu sekta ya misitu na kwa kweli walinisikiliza na kupokea mawazo yangu.

Mheshimiwa Spika, sekta ya misitu ni mtambuka kwa kiasi fulani, jana tumepitisha bajeti ya Wizara ya Nishati, moja ya mkakati wao ni kufikisha umeme vitongoji 15 kwa kila jimbo, lakini pia kuna miradi ya REA III, Awamu ya Pili, miradi ya ujazilizi wao wanaita 2A, 2B,2C na kadhalika na miradi ya TANESCO, yote hii inategemea kwa sehemu kutumia nguzo zinazotoka katika sekta ya misitu, lakini pia ujenzi wa miradi mbalimbali ya Serikali kuanzia majengo ya shule, zahanati, vituo vya afya na hospital za wilaya, ujenzi wake kwa sehemu unatumia mazao ya misitu kuanzia milunda, mbao, plywood na kadhalika. Hata Mji wa Serikali Mtumba, majengo mengi kama sio yote yanatumia bidhaa zinazotokana na misitu.

Kwa hiyo, sekta hii ni muhimu sana katika kuchangia pato la Taifa, hata takwimu kwamba sekta hii inachangia 3% sio sahihi kwa sababu takwimu hii inaangalia tu mti/gogo, mara baada ya kuvunwa, bidhaa inayofuatia inaonekana sio msitu tena. Kwa hiyo, kwa ufupi sekta hii ni muhimu na tuendelee kuitizama na hasa katika suala zima la EWP, nashauri kongamano tulilofanya mwaka 2021 tuendelee nalo kila mwaka kwa nia ya kunyanyua sekta hii na hasa suala zima la EWP.

Mheshimiwa Spika, kuhusu REGROW mradi huu ambao ni mkopo wa Benki ya Dunia umekuwa unatekelezwa kwa kusuasua sana, huu ndio ukweli, mradi huu ukitekelezwa kwa kasi utasaidia sana kukuza utalii Kusini, utaboresha mazingira ya utalii na hivyo kuvutia wawekezaji zaidi. Mheshimiwa Rais ametufanyia kazi kubwa katika kututangazia utalii kupitia Royal Tour, kwa hiyo REGROW itasaidia sana kuendana na kasi ya kuongezeka kwa watalii.

Mheshimiwa Spika, mimi ni mmoja wa watu ambao nimeusemea sana mradi huu, nashauri tuongeze kasi ya kuutekeleza, ninaamini kwa kasi ambayo Mheshimiwa Waziri na Katibu Mkuu wake walionesha kwenye sekta ya michezo, wataitumia kusukuma mradi huu, kama alivyosema Mheshimiwa Waziri kwamba mzigo mzito mtwishe Mndengereko, basi mimi namtwisha mzigo huu ili twende kwa kasi.

Mheshimiwa Spika, ndege ndogo; kuna gharama kubwa sana ya usafiri wa anga kutembelea mbuga zetu, ushauri, kaeni ndani ya Serikali tupate ndege za ability ya kati ya watu nane hadi 14 ambazo zitaweza kutua mbugani, na hizi ziwe za ATC, kwa kuanza hata mbili zitafaa kuwa zina shuttle kati ya Dar es Salaam, KIA na mbuga zetu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.