Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Mwanakhamis Kassim Said

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Magomeni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii kuweza kuchangia Wizara hii ya Maliasili.

Mheshimiwa Spika, leo ni siku ya jumatatu ni siku tukufu ni siku nzuri sana kwa hivyo nakuombea dua kwa Mwenyezi Mungu akujalie kwa jambo lako hilo unalokwenda kulifanya la huko Duniani ufanikiwe. Kufanikiwa kwako ni kufanikiwa watanzania, kufanikiwa kwako ni kufanikiwa Wabunge, kufanikiwa kwako ni kufanikiwa Wanawake hususani wa Jimbo lako la Mbeya Mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan bado kuendelea kupambana na nchi yake lakini kuiletea maendeleo nchi yake. Nimpongeze Dkt. Hussein Ali Mwinyi wa Zanzibar kwa kazi kubwa anayoifanya, lakini nirudi kumpongeza Dkt. Hussein na Mama Samia Suluhu walivyotangaza Royal Tour walitangaza jambo hili kwa upendo mkubwa, kwa ukakamavu mkubwa na kwa kuwa na moyo wa dhati wa nchi zao au wa nchi yao ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Dkt. Hussein Ali Mwinyi walitangaza utalii wa fukwe, walianza huko wa Bahari halafu wakaja kwenye zetu za utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa nini jambo hili Viongozi wetu wa nchi kutangaza utalii? Kwa sababu hizi ni rasilimali za nchi yetu na ndizo tunazozitegemea na rasilimali zetu hizi ikifika miaka kumi, kumi na tano basi Mheshimiwa zitapotea. Kwa hivyo, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Mama Samia walisimama kidete kutangaza utalii wa nchi zetu mbili hizi iliyobaki Watanzania nasi lazima tuwaunge mkono Viongozi wetu waandamizi wa Nchi kwa juhudi kubwa waliyofanya kutangaza utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninampongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri, kwa kweli wanakazi kubwa sana kwa sababu Mheshimiwa kila aliyenyanyuka alimzungumza tembo. Sasa siye kama kazungumzwa tembo kwa kweli tunasema ni jambo kubwa sana hili kuzungumzwa tembo kama amekuwa anapiga watu sasa ni hatari! Namuomba Mheshimiwa Waziri hii tembo aidhibiti kwa nguvu zake zote pamoja na Naibu Waziri. Kwanza ana Naibu Waziri mkakamavu, muelewa, mchapakazi na Waziri umeingia kwenye Wizara ni Wizara ngumu sana, lakini Mungu atakusaidia. Kwa vyote anavyochakatwa huyo tembo lakini bado uendelee kupambana tembo wasiathiri wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwakweli ni hatari tena hii ni hatari kubwa sana, tembo wasiumize. Unao Askari wakakamavu, unao Kamati yako nzito, madhubuti na Waziri Mkuu anasaidia sana kutatua migogoro, sasa hii migogoro ya tembo sasa ataitatua vipi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwakweli Mheshimiwa Waziri ni mchapakazi, Wizara hii ni Wizara ngumu, nzito sana ni Wizara iliyo na mambo mengi sana, lakini sisi tunasema unaweza, kwa sababu kule utamaduni ulifanya vizuri Alhamdulillah. Kwa hivyo na hapa tunataka uendelee kuchapa kazi, una Naibu Waziri ni Mwanamke lakini mwanamke shujaa sana, mtume Naibu wako Waziri anatumika usimuogope.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri Askari wetu kwa kweli wanazungumzwa sana wao ni wanyonge, wamezaliwa kama sisi kila mmoja mwenye mama yake naye anao mama yao. Leo askari imekuwa wapo kwenye matatizo makubwa sana, tunakuomba Mheshimiwa Waziri uwasaidie askari wetu, wapambane lakini uwasaidie kwa nguvu zako zote. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa ahsante sana, kengele imeisha gonga.

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)