Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya njema na tuko hapa leo tuna afya nzuri sana. Pili, nimpongeze Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa filamu ya Royal Tour, filamu ya Royal Tour imefungua nchi yetu imetuongezea watalii wengi sana, tatu nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Ndugu Mchengerwa, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu nzima ya Maliasili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache sana leo na I think ndiyo wakati pekee nitaongea leo a bit calm, kuliko wakati mwingine wowote. Utalii na uhifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utalii ni sekta muhimu sana inaongezea nchi yetu mapato lakini inasaidia kufungua nchi yetu, kuna uhifadhi vilevile ambayo ndiyo conservation, sasa na mimi nafikiri Mheshimiwa Waziri utalii na uhifadhi ni vitu viwili tofauti. Uhifadhi ndiyo hard core ya uhifadhi lakini utalii ndiyo soft part, the business element, sasa hivi ni vitu viwili tofauti tukivichanganya sana pengine tutashindwa ku - appreciate tofauti zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini mtu anayelinda maeneo ambaye ni mtaalam wa wanyamapori, ambae atakuwa natuambia study za wanyamapori zikoje, atakuwa anapambana na majangili huyo huyo mtu ndiyo atuuzie kweli hifadhi zetu the business element? Mimi siamini hivyo. Mheshimiwa Waziri hebu angalia tengeneza timu zako, timu inayo - deal na watalii peke yake na timu ambayo inafanya mambo ya uhifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukifanya hivyo nadhani tutapata namna ya kufaidika vizuri zaidi. Wale ambao ni wahifadhi tena ambao ni Jeshi USU siku hizi, tena ndiyo kabisa wanatakiwa wao waanze kupambana na majangili, mimea vamizi, waandike vitabu, waandike articles waende kwenye scientific conferences, wajaribu kuuza nchi yetu kwa scientific element part ya conservation. Watu ambao watafanya kazi ya utalii ambayo ndiyo business element, lazima tuwe na timu ambayo ni tofauti kidogo ambayo ni sharp ni creative ni innovative, kwa sababu biashara tunashindana na wengine it is about competitiveness, lazima tuwe na timu nyingine, hebu mui–organize kidogo tunaweza tukanufaika zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahishwa sana na pengine ndiyo maana leo am very calm na kauli zako mbili ulizotoa baada ya kuteuliwa. Umesema wananchi ni wahifadhi namba moja, lakini ukasema vilevile watu wa hifadhi watapimwa kutokana na wanachosema wananchi juu yao. Mheshimiwa Waziri hizi kauli zote mbili ukishikilia unaweza ukawa the best Minister of our life tangu nchi hii ipate uhuru. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitizama mahusiano kati ya wananchi na wahifadhi wanyamapori maeneo ya hifadhi ni mbaya, Mheshimiwa Waziri Ilani ya Chama cha Mapinduzi nikupe tu comfort ukurasa wa 113 inazungumzia kwamba tulisema tutaimarisha mahusiano kati ya wahifadhi na maeneo ya hifadhi na wananchi na Ilani inasema kabisa hivi na ninukuu “kuimarisha mahusiano kati ya maeneo ya hifadhi na wananchi na kulinda mali za wananchi na wananchi wenyewe, vilevile kutoa elimu. Ili sekta ya Maliasili iwe endelevu ni lazima ijali haki na maslahi ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, ukienda na hizi mbili, kwa kweli utakuwa an exceptional Minister of our life nikuambie tu ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu mwingine Mheshimiwa Waziri, unajua kati ya maeneo ambayo bado tuna elements za kikoloni ni kwenye eneo hili la conservation. Nilikuwa naangalia Sheria ya Fauna Conservation ya mwaka 1951, nikakutana na kipengele ambacho kinatutesa mpaka leo, hiki cha forfeiture. Ku-forfeit magari, mifugo ya wananchi pale ambapo wanaingia kwenye hifadhi zetu. Kumbe nikagundua kwamba ilianza wakati ule wa ukoloni, forfeiture! Fauna Conservation, Section 53, utakutana nayo na bado ipo mpaka leo kwenye Sheria yetu ya Wanyamapori. Mheshimiwa Waziri lazima tu-decolonize hizi sheria na policies ambazo zinaendelea kutesa watu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuingia kwenye hifadhi ni kosa, lakini isiwe sababu ya mtu kuwa maskini. Mimi na-subscribe na conservation ambayo, na kauli zako zina-support kwamba, conservation for people and by the people. Hiyo tukienda hivyo tutafanya vizuri sana kwa sababu, after all hifadhi for whose benefit?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ni wananchi hawa wa Tanzania hawa wanufaika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri ukienda hivyo tuangalie sheria hizi ambazo zina-colonize. Sasa kwa mfano siku hizi ng’ombe wakikamatwa watu wanafanya compound halafu una-charge laki moja kwa kichwa cha ng’ombe, which is fifty percent of the price. Sasa kama tukiamua kwenda kwa njia hiyo, basi tukiwa tunakamata magari on traffic offences kama gari lako ni Vits tuseme fifty percent ya bei ya hili gari tu¬-charge kama fine kama ndiyo tunataka kwenda huko, lakini mimi siamini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lilishasema maximum fine na minimum fine, una-charge kwa kosa siyo kwa kichwa cha ng’ombe. Hapa nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo hapa kwamba, Wizara yenu mkapitie na mkaangalie sheria. Haiwezekani ng’ombe ni laki moja na nusu, halafu unataka kunichaji laki moja kama fine, siyo sawa! lakini Mheshimiwa Waziri kuna ng’ombe wengi sana wamekatwa kwenye maeneo haya, kuna watu wamekwenda wameshinda kesi Mahakamani, lakini mpaka leo wananchi hawa hawajapewa mifugo yao na wapo wengi sana. Hebu wewe tizama na uangalie vizuri sana na pengine ukae na timu yako tena mu-re-evaluate hii kushika ng’ombe kila wakati. Mtengeneze mahusiano, mkitengeneza mahusiano mimi nadhani hakutakuwa na matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naongea na Mheshimiwa Dkt. Mbunge wa Muleba nae ana shida hiyohiyo, wananchi wake wanahangaika kila mahali. Mimi nadhani Mheshimiwa Waziri tengeneza mahusiano haya, wananchi wakifurahi uhifadhi utaendelea na sote tutafurai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakupongeza unajua wakati mwingine ukipata report za hawa wataalam wako wa maliasili na utalii, achana na hizo ripoti njoo field tena, tembea. Nenda kaongee na wananchi wale, tembelea maeneo yale, utanufaika zaidi kwa kuwasikia wananchi wanasema nini kama ulivyofanya Serengeti. Hiyo ilikuwa ni innovation kubwa na nzuri sana, Mheshimiwa Waziri ukiendelea hivyo itakuwa nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo jingine ni WMA. Mheshimiwa Waziri hii strategy ambayo umeianzisha na nikushukuru kwamba, juzi mmezindua strategy ya kuendesha WMA. Nami najua wewe kwako una WMA hata mimi nina WMA, wananchi hawa wamefanya mambo mengi sana na kutoa ardhi hizi ziwe kwenye WMA na wao sasa waanze kushindana na mbuga za wanyama na maeneo mengine yote yenye WMA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nikuombe Mheshimiwa Waziri, hapa tuna Wabunge wengi sana wa WMA, tufanye mpango, tengeneza group la Wabunge wa WMA. Zile WMA zi-protect kutokana na wale investors ambao wengine wakorofi, wanawashitaki Mahakamani. Ukifanya hivyo nadhani sekta hii itafanya vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda naunga mkono hoja na ninakutakia kila la heri. Ahsante sana. (Makofi)