Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa kazi kubwa inayoendelea nchini ikiwemo jimbo langu pendwa la Busanda mkoani Geita, mambo kadhaa naomba Wizara iyafanyie kazi; moja, mkandarasi jimboni Busanda aongeze kasi. REA na Geita Nyakanazi Projects.

Pili, transfoma kwenye maeneo ya wachimbaji wadogo zibadilishwe kwa kuweka zenye uwezo mkubwa, mfano Kijiji cha Nyakagwe na taasisi za umma ziwekewe umeme, kwa mfano shule, zahanati na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, ahadi za Waziri mwaka jana mwezi Julai, 2022 jimboni Busanda zitekelezwe, kama vile solar panel katika Zahanati ya Shilungule Kata ya Busanda, taa za barabarani Mji Mdogo wa Katoro (Kata ya Katoro, Kata ya Ludete na Nyamigota).