Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuiwezesha Wizara hii kuipatia fedha kuweza kupata kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo kwenye Wizara hii. Nampongeza sana sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na Katibu Mkuu bila kumsahau Naibu Katibu Mkuu.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu kwa leo sina zaidi ya kuipongeza Wizara hii. Ukiangalia tulikotoka na tulipofikia Serikali imepiga hatua kubwa sana. Nilikuwa na maneno mengi siku za nyuma lakini sasa sina maneno zaidi ya kupongeza. Napongeza pia kuja na mkakati wa nishati bora ya kupikia, kweli ni ukombozi kwa mwanamke, shukrani kwako Mheshimiwa Waziri na timu yako yote kwa jambo kubwa mlilofanya la kuwajali wakina mama wa Tanzania, mbarikiwe sana.

Mheshimiwa Spika, ombi langu naomba mradi wa usambazaji wa gesi asilia utengewe fedha ya kutosha, gesi ifike Mbagala, Tandale, Gongo la Mboto na maeneo ya pembezoni. Nawashukuru sana sana na kuwapongeza sana Mheshimiwa Waziri na timu yako, endeleeni hivyo na Mungu atasimama na ninyi.