Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, pongezi za pekee kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiangalia kwa jicho la kipekee Wizara hii na kuisaidia hasa katika miradi ya kipaumbele, LNG, Mwalimu Nyerere Hydro Power na mengineyo. Pongezi kwa Wizara, Waziri Mheshimiwa January Makamba, Naibu Waziri Wakili Mheshimiwa Stephen Byabyato, Katibu Mkuu Engineer Mramba, Naibu Katibu Mkuu Bwana Mbutuka pamoja na watendaji wakuu wote wa mashirika na taasisi mbalimbali bila kusahau watumishi wenzangu kwa kazi kubwa na nzuri inayoendelea.

Mheshimiwa Spika, maombi; kwanza pamoja na shukrani za kutuongezea umeme katika vitongoji (Underline T/F) jambo ambalo litaongeza ustawi, ubunifu na uchumi kwa ujumla. Pamoja na shukrani hizo nina maombi rasmi ya kupeleka umeme katika vitongoji viwili vilivyopo mpakani na nchi ya Msumbiji. Ni muhimu kwa ajili ya usalama, ni muhimu kwa ajili ya uchumi kwani maeneo hayo yana dhahabu na pia ni centers za kibiashara. Vitongoji hivyo ni Nindi na Ngeapori. Kwa kuwa Wizara ya Nishati ni sikivu, basi naomba mnisikilize katika ombi langu hili la kuhakikisha kuwa maeneo haya ya mpakani yanasaidiwa.

Pili, napongeza mradi wa nishati safi ya kupikia. Nashauri pia kuwepo na mradi maalum wa ku-supply mitungi ya kilo 30 katika vituo vya afya na zahanati japo tutaanza na michache tuliyopewa kwa ajili ya uhamasishaji. Nawatakia utekelezaji wenye mafanikio.