Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mungu kwa uhai pia nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania kwa kazi nzuri anayoendelea kufanya katika Taifa letu, hakika Mungu ampe afya njema.

Mheshimiwa Spika, pongezi nyingi ziende kwa Waziri na Naibu wake wa Wizara hii ya Nishati pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Spika, niende katika Jimbo la Temeke; niwapongeze sana kwani kazi imewezakufanyika kwa ufanisi, tunashukuru umeme umeweza kuwa stable kuliko miaka ya nyuma, lakini niombe kwa kuwa jimbo letu la Temeke limekuwa ni jimbo la viwanda vingi na umeme umekuwa bado ni mdogo kwani hautoshelezi kwa viwanda na matumizi ya majumbani, lakini pia umeme bado tunapata kutoka Ilala. Tunatamani kupata ongezeko la transfoma kubwa ambayo itatuongezea umeme ukizingatia bado hatupati umeme mfululizo kwani katika wiki tunaweza kukosa, baadhi ya kata ukakatika kwa masaa kadhaa na ukirudi unarudi mdogo na wakati mwingine unarudi kwa baadhi ya mitaa ya kata moja na mitaa mingine ikakosa ndani ya kata hiyo hiyo.

Mheshimiwa Spika, niombe sana muangalie upya umeme unaopita chini ya ardhi, tupate vipuli vyake ili urekebishwe maana kila umeme unapokatika tunaambiwa hitilafu kubwa inatoka kwenye Kituo cha TOL pale Pugu Road, naamini mnapafahamu hivyo niombe sana Wizara ituangalie sana Jimboni Temeke, ni jimbo tunategemea sana mapato yetu ya ndani kutoka kwenye viwanda hivyo visipopata umeme kazi hazitafanyika na pia wafanyabiashara wadogo wadogo waweze kufanya biashara zao ili mapato yaongezeke na Watanzania wa jimboni wafaidike na kazi nzuri ya matunda ya uongozi mzuri wa Mama Samia, Rais msikivu na myenyekevu.

Mheshimiwa Spika, nawapeni hongera sana kwa maonyesho ya Bungeni yamenifungua na mengi nimejifunza, naunga mkono hoja.