Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nimpongeze sana Waziri wa Nishati Mheshimiwa January Makamba na Naibu wake Mheshimiwa Stephen Byabato pamoja na jopo la wataalam wa Wizara kwa kazi kubwa wanazofanya kupeleka umeme na nishati nyingine muhimu kwa wananchi wetu hapa nchini Tanzania.

Mheshimwa Spika, tunaishukuru Serikali kwa kuongeza bajeti ya Wizara hii kutoka shilingi trilioni 2.91 kwa mwaka wa fedha wa 2022/2023 hadi shilingi 3,048,632,519,000 kwa mwaka wa fedha wa 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utahusu kukosekana umeme katika baadhi ya maeneo ya Jimbo la Moshi Vijijini ambayo hayajaunganishwa.

Mheshimwa Spika, pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali kupeleka umeme vijijini, bado wananchi wengi wa Jimbo la Moshi Vijijini hawajapatiwa nishati ya umeme.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi ninaiomba Wizara ya Nishati isaidie kutatua changamoto za nishati ya umeme katika Jimbo langu la Moshi Vijijini kwani bajeti iliyotengwa ni kubwa na Wanamoshi Vijijini watafurahia kufikiwa.

Mheshimiwa Spika, maeneo yenye changamoto ya umeme katika Jimbo la Moshi Vijijini ni kama ifuatavyo; Kata ya Mabogini; kama nilivyoomba kwenye bajeti ya mwaka jana na mwaka juzi, katika Kata ya Mabogini sehemu ambazo hazijapata umeme hadi sasa ni Vitongoji vya Sanya "Line A" na Mjohoroni vilivyopo katika kijiji cha Mabogini.

Pia katika Kitongoji cha Uru - katika Kijiji cha Muungano; katika Kijiji cha Maendeleo, Vitongoji vya Mshikamano na Uarushani; Mgungani - katika Kijiji cha Mtakuja; katika Kijiji cha Mserekia, hakuna umeme katika Vitongoji vya Mbeya Kubwa, Mbeya Ndogo, Remit, Mkwajuni na Mafuriko. Kijiji cha Mji Mpya, Kitongoji cha Utamaduni hakijaunganishwa. Ninaiomba Serikali ipeleke huduma kwenye maeneo yaliyotajwa.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Arusha Chini kwenye Kijiji cha Mikocheni, Vitongoji vya Masaini na Mashimo ya Mchanga hakuna umeme. Ninaiomba Serikali ipeleke huduma kwenye maeneo haya.

Aidha katika Kata ya Kimochi, Kitongoji cha Kiwalaa kilichopo Kijiji cha Sango; Kitongoji cha Iryaroho kilichopo katika Kijiji cha Mowo; na Kitongoji cha Maryaseli katika Kijiji cha Lyakombila havina umeme. Ninaiomba Serikali ikamilishe ujenzi wa miundombinu ya umeme katika maeneo niliyotaja hapo juu.

Katika Kata ya Kibosho Mashariki kama nilivyoomba kwenye bajeti ya mwaka jana na mwaka juzi, Kata ya Kibosho Mashariki inahitaji huduma katika Kijiji cha Sungu Vitongoji vya Kyareni na Nkoitiko havijaunganishwa; katika Kijiji cha Singa, Kitongoji cha Singa Juu hakijaunganishwa; katika Kijiji cha Mweka, Kitongoji cha Mweka Juu na Omi havijaunganishwa. Ninaiomba Serikali ipeleke huduma kwenye vijiji na vitongoji vilivyotajwa.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Kibosho Kati kama nilivyoomba kwenye bajeti ya mwaka jana na mwaka juzi, katika Kata ya Kibosho Kati, vijiji vya Uri na Otaruni umeme una nguvu kidogo (low voltage) na kunahitajika transfoma. Katika Kijiji cha Otaruni, Kitongoji cha Ngoroshi hakuna umeme, na tunaomba wananchi wapatiwe huduma.

Katika Kata ya Okaoni - Vijiji vya Sisamaro, Omarini na Mkomilo vinahitaji kuunganishwa japo baadhi ya maeneo nguzo zimepita ila bado kuunganishwa.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Kindi, Kijiji cha Chekereni Weruweru, Vitongoji vya Miembeni na Kisiwani havina umeme kabisa. Pia baadhi vitongoji vya vijiji vya Kindi Juu na Kindi Kati havijapata umeme, ninaiomba Serikali ipeleke huduma kwenye vijiji na vitongoji hivi.

Mheshimiwa Spika, katika Kata ya Uru Mashariki, kama nilivyoomba kwenye bajeti ya mwaka jana na mwaka juzi, Kijiji cha Materuni, Kitongoji cha Wondo hakijaunganishwa. Ninaiomba Serikali ipeleke huduma kwenye kitongoji hiki.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mbokomu ni kama nilivyoomba kwenye bajeti ya mwaka jana na mwaka juzi, Kitongoji cha Mmbede Kyaroni, Tema na Masanga na baadhi ya maeneo ya Korini Kati havijaunganishwa. Ninaiomba Serikali ipeleke huduma kwenye maeneo haya.

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo yangu hapo juu, naunga mkono hoja.