Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. NASHON D. BIDYANGUZE: Mheshimiwa Spika, naomba na mimi nikushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia hotuba hii ya Waziri wa Nishati, ndugu yetu Mheshimiwa Januari Makamba. Kwanza naomba nichukue nafasi hii kwa kusema kwamba, mimi naunga mkono hoja kwa sababu eneo hili ni eneo kubwa nani nyeti. Na kama mwenyewe Mheshimiwa Januari anavyoendelea kulizungumzia, ni kwamba kwa kweli, bila umeme nchi itasimama. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nizunguimzie kwenye eneo moja, lile la vinasaba ambavyo kimsingi tulikwishakubaliana kwamba TBS ndio ambao wataendelea kuweka vinasaba kwenye mafuta. Mimi naomba kwenye eneo hili niendelee kusisitiza kwa sababu TBS pia ni Shirika la Serikali. Mheshimiwa Waziri aendelee kusimamia jambo hili kwenye eneo la TBS, TBS waendelee kuweka vinasaba kwenye mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kwanza naomba nimpongeze Meneja wa TANESCO Wilaya ya Uvinza, anafanya kazi vizuri sana tena katika mazingira magumu. Kuna kipindi alikuwa hana hata gari la kubadilisha transformer kuweka nyingine; kwa sababu mradi huu wa REA ulianza na transformer ambazo ni ndogo kidogo ambazo zilikuwa ni 100, lakini yeye anaendelea kubadilisha kwa gharama za TANESCO, anapoomba fedha anapewa kufanya miradi na anabadilisha sasa kutoka 100 kwenda 150 mpaka 200. Kwa hiyo ni jambo la kumpongangeza sana kwa sababu, sasahivi wananchi wanaendelea kutumia umeme na wakati kwingine wanatumia kwa ajili ya mashine za kusaga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini lingine, katika jimbo langu kuna vijiji 61, vijiji 29 vilishapata umeme, vijiji 32 bado. Hata hivyo naomba nimshukuru Mheshimiwa Januari Makamba, sasahivi tunavyozungumza kuna vijiji sita vinaendelea kuwekewa umeme, ni jambo la kupongeza sana, na kwa hili naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Makamba. Lakini pia kuna njia ya umeme ambayo ni kilometa 104.6 ambao unatoka Kirando kwenda Karirani, ni umbali mrefu. Na umbali huo ndio ambao vijiji hivyo viliwekewa umeme wa jua, na siku zote wamekuwa wakilalamika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa unaweza kuona kabisa kwamba, hiyo line ambayo imeanza kujengwa ikikamilika itakuwa na uwezo wa kusaidia kuweka umeme vijiji 13. Kwa hiyo vijiji vyangu ambavyo ambavyo havina umeme vitazidi kupungua. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Makamba kwa kazi hiyo nzuri ambayo anaifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba niseme; jana Mheshimiwa Makamba amezungumzia kwenye bajeti yake kwamba mwaka ujao wa fedha kwa eneo lile la Malagarasi, umeme ule wa Kv 49, kama sijakosea 49, utakwenda kuanza kujengwa. Na taarifa nilizonazo ni kwamba mkandarasi alikwishapelekwa site. Mkandarasi wa kujenga alishapelekwa site, lakini pia mkandarasi wa kujenga njia ya kupeleka umeme kule wilayani ameshapatikana.

Mheshimiwa Spika, lakini pia, naomba nipongeze kwamba, umeme ule ambao unatoka Tabora ambao unakuja pale Nguruka kwenye eneo la pale Mganza ambapo sub station imeshajengwa, bado ku-install, naomba nikushukuru. Hata mkandarasi wa kuja kuifanya hiyo sub station ikamilike amekwishaletwa pale, na mimi taarifa ninazo na mimi nilimuona, hilo ni jambo jema sana. Pia mkandarasi wa kuleta njia ya umeme kutoka Tabora kuja hapo amekwishaletwa pale site, lakini wa kutoka hapo tena kupeleka kwenye eneo ambalo limeandaliwa ameshapatikana. Kitu ambacho naomba nimuombe Mheshimiwa ni kwenye hawa watu wanaoathirika na hiyo njia, kwenye kuwathamini. Naomba kusiwe na mgogoro kwenye eneo hilo, hawa wananchi wamekuwa na ridhaa na wameacha maeneo yao. Sasa ninaomba sana hao nao waweze kuthaminiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jingine ambalo ninamwomba Mheshimiwa Waziri, ni kwenye eneo la Kijiji cha Nguruka na Kijiji cha Uvinza. Naomba sana, hili jambo nimekuwa nikimwambia siku zote kwamba hawa watu walipangiwa shilingi 320,000 lakini uwezo huo hawana, mimi ndiye ninayewajua. Nashukuru Mheshimiwa Waziri alituma tume, ilikwenda, na nadhani taarifa anayo. Naomba sana Mheshimiwa Waziri atakapokuja kujibu atamke neno, Nguruka warudi kulipa shilingi 27,000 lakini pia, Uvinza warudi kulipa 27,000. Na kubwa sana hivi leo wako kwenye runinga wanaendelea kusikiliza jinsi ambavyo Mbunge wao anamwomba Mheshimiwa Waziri, na wangetamani aseme, ili waweze kusikia, naomba sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo naomba niunge mkono hoja kwamba, hii bajeti iko vizuri na mimi nitakuwa tayari kuipitisha. Ahsante sana. (Makofi)