Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

Hon. Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Nishati

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na mimi kwa kunipa nafasi hii niwe mmoja wa wachangiaji wa bajeti yetu hiii muhimu ya Wizara ya Nishati.

Mhemiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri lakini pia nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kuweza kuifanikisha Wizara hii kwa kuipatia fedha kwa wingi na kuweza kufikia malengo yake. Pia, nimpongeze Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Mkurugenzi wa REA, Mkurugenzi wa TANESCO Ndugu Maharage Chande na wafanyakazi wao wote kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakiitendea haki Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, leo hii mimi nimesimama, na mara nyingi zaidi ya miaka mitatu minne nilikuwa nikisimama jambo langu kubwa lilikuwa ni kuhusu bei ya umeme Zanzibar. Lakini mimi ninayofuraha, pamoja na Wazanzibari wote jinsi ambavyo Wizara hii chini ya usimamizi wa viongozi hawa na Katibu Mkuu wao Mramba, kuweza kukubaliana na Serikali ya Zanzibar kuweka bei sawa pamoja na Tanzania bara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo hili tunawapongeza sana. Leo nitakuwa na mambo mawili ambayo yanataka Mheshimiwa Waziri utakapo wind up unipe status yake limefikia wapi.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na mpango wa TANESCO wameongea na Wizara ya Nishati ya Zanzibar kuhusu kupeleka cable nyingine ya umeme, kwa sababu cable iliyokuwepo sasa hivi inakaribia kuzidiwa kwa kuwa ina megawatts 100 na sasa hivi tuko abourt 80 na kuendelea. Pia, kutokana na hali ya uchumi wa Zanzibar ambayo Rais wetu wa kule Dkt Hussein Ali Mwinyi ya Uchumi wa Blue uwekezaji umekuwa mkubwa sana. Sasa uwekezaji huu hautoweza kufanikiwa kama itakuwa hatuna umeme wa uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri, nilikuwa namuomba Mheshimiwa Waziri, kama tulivyoweza kuzungumza kwenye Kamati yetu; kwanza na-declare kwamba mimi ni mjumbe wa Kamati hii; kwa hiyo, mengi yanayozungumzwa humu na ambayo ameyazungumza Mheshimiwa Waziri ni kweli, na yote ameyafanya ni kutokana na ushirikiano ambao sisi tunampa ushauri halafu na wao wanauchukua na wanaufanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwapongeze sana watu wa TANESCO, kwa upande wao wamekuwa wakiwasaidia sana watu wa ZECO, zaidi pale inapotokea hitilafu ya umeme mdogo au ukatikaji wa umeme upande wa Bara, yaani Ras Kilomoni kwa ajili ya kwenda Unguja na Majani Mapana Tanga kwa ajili ya Kwenda Pemba, nawapongeza sana wafanyakazi wa TANESCO. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, isipokuwa kwa kumalizia tu na si ka ajili ya muda kwa sababu leo hii katika jambo ambalo umetufurahisha Wabunge ni jinsi ambayo umetuelekeza kujibu hoja na kuuliza swali. Twende moja kwa moja; na mimi ndiyo maana nimeanza moja kwa moja, na huu ni mwendokasi. Nakupongeza sana kwa hili. Style hii tukiendelea nayo tutaweza ku-manage muda wetu. Waheshimiwa Wabunge tuko wengi na kila mmoja anataka kuchangia; na ili tuweze kuchangia ni lazima tu manage time. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hongera sana na bila kusahau nataka nikwambie jambo lako ni letu sisi sote Wabunge humu ndani. Tuko na wewe, na tunajua una jambo lako lakini ni letu sisi. Ahsante sana kwa kunipa nafasi hii nakupongeza wewe, Mheshimiwa Waziri na Wizara yote, naunga mkono asilimia. (Makofi)