Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara iimarishe shughuli za Jeshi la Magereza hususani Gereza la King'ang'a kwa kufanya mambo yafuatayo; kwanza, kupima eneo la gereza lote na kupata hatimiliki ili kuepuka uvamizi wa eneo hilo na kulipangia matumizi bora ya ardhi.

Pili, kuwe na ufugaji wenye tija kuliko ilivyo sasa kuna kundi kubwa la ng'ombe lenye tija ndogo sana. Wanafuga kienyeji, hawana shamba la malisho, hawana kisima cha maji, hawana josho la koushea mifugo, hawana wataalam wa kusimamia mifugo matokeo yake hata product ya mifugo yao ni kilo chache sana. Wananchi hawana cha kujifunza kutoka Gereza la Mifugo King'ang'a.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kumaliza mgogoro kati ya gereza na wananchi wa Kingale, tunapenda kupata askari ambao wataimarisha mahusiano na jamii inayolizunguka gereza tofauti na ilivyo sasa. Askari waliokaa muda mrefu gerezani pale wangehamishiwa maeneo mengine ili kupata askari wengine watakaoleta maarifa mapya ya maendeleo. Tunapenda kupata askari wenye taaluma ya mifugo, kilimo, umwagiliaji na wachumi ili kulisaidia gereza kujiimarisha kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Mji wa Kondoa umekuwa na unaendelea kukua, tunahitaji kupatiwa vifaa vya Jeshi la Zimamoto ikiwemo gari kwa maana hakuna huduma hiyo hali tukiwa tunashuhudia mali za wananchi zinateketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni tumeshuhudia mabweni ya wanafunzi yakiteketea bila msaada wowote kwenye Shule ya Sekondari Kondoa Islamic na kituo cha kulelea mayatima cha Bicha, magari yameungua moto, viwanda vya mafuta ya alizeti vimeteketea na nyumba za wananchi. Tunaomba gari la zimamoto na vifaa vya askari wa zimamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu magari ya polisi yamechakaa sana tunaomba polisi wilaya wapatiwe gari la kufanyia doria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo naunga mkono hoja.