Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Suleiman Haroub Suleiman

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SULEIMAN HAROUB SULEIMAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia afya njema na kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara yetu muhimu kwa ustawi wa Taifa letu. Aidha, naomba kuchukua fursa hii adhimu kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu kwa kutuongoza kwa umahiri na uweledi mkubwa, ninamuombea kwa Mwenyezi Mungu amjaalie afya njema na mafanikio mema zaidi.

Pia pongezi kwa Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wote Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Lakini pia nampongeza Waziri Mheshimiwa Engineer Hamad Yusuf Masauni na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza pia IGP, Makanda, RPC, OCD na maafande wetu wote walio chini ya Wizara hii. Nchi ipo salama na kwa mipango na mikakati ya Wizara hii nina imani thabiti kuwa Tanzania itaendelea kuwa salama na Watanzania tutaendelea kuwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo naomba kuchangia na kushauri machache kama ifuatavyo; kwanza kutoa mafunzo ya ukarimu na matumizi ya lugha nzuri kwa wananchi. Kuna baadhi ya askari hasa Zanzibar unapokwenda kutafuta huduma za usalama na ulinzi baadhi ya askari wanawajibu raia lugha zisizoridhisha na zinazovunja moyo, haziendani na heshima ya Jeshi letu

Pili, utoaji wa huduma nzuri hasa katika sehemu za kuingia nchini kwa mfano uwanja wa ndege na bandarini, mfano Zanzibar uchumi wake unategemea zaidi sekta ya utalii hivyo basi askari wa Uhamiaji wa maeneo hayo ni vizuri watoe huduma nzuri na stahiki kwa Watanzania na wasio Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni kuhusu Vitambulisho vya Mtanzania kwa wenye sifa za kupatiwa. Kuna ukakasi kwa baadhi ya maeneo katika upatikanaji wa vitambulisho hivyo.

Nne ni kuhusu doria; ni jambo zuri sana kwa kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yetu sehemu tofauti za nchi yetu hivyo ninashauri Jeshi la Polisi liendelee na doria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hitimisho, naipongeza Serikali inayoongozwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan; Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar na wasaidizi wao wote. Aidha nikutakie kheri na mafanikio mema zaidi Waziri - Mheshimiwa Hamad Yussuf Masauni na Naibu Waziri - Mheshimiwa Jumanne Sagini katika kutimiza majukumu mliokabidhiwa na Mheshimiwa Rais kwa maslahi ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia, ahsante sana.