Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kuipongeza Serikali kwa kazi kubwa inayoendelea kufanya kwa kuhakikisha ulinzi na usalama unaendelea kuimarika katika pande zote za nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, polisi wanafanya kazi kubwa sana ila idadi ya polisi ni wachache, naiomba Serikali kuendelea kuajiri askari ili kuendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Igalula lina changamoto kubwa ya vituo vya polisi, kwa kutambua hilo wananchi wameanzisha ujenzi wa vituo vya polisi katika Kata za Tura na Goweko; naiomba sana Serikali kutupatia pesa ili tuweze kukamilisha ujenzi wa vituo vya polisi vya Tura na Goweko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na polisi kufanya kazi kubwa sana ila kumekuwepo na kutokulipwa kwa stahiki zao ambazo zipo kwa mujibu wa sheria, kwa mfano pesa ya pango yaani kodi za nyumba kila mwezi. Polisi wamekuwa hawalipwi pesa hizi kwa muda sana, naiomba Serikali itusaidie kuwalipa ili kupunguza rushwa kwa sababu ya maisha magumu ya polisi. Polisi wamekuwa wakidai malimbikizo mengi sana, niiombe Serikali iwalipe polisi ili waweze kuwa na moyo kwa kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na changamoto kubwa sana kwenye upatikanaji wa Vitambulisho vya Taifa, wananchi wanapata changamoto kubwa sana, kwanza ofisi za NIDA ipo moja kila Mkoa, sasa ipo moja tu wananchi kutoka Kata za Mmale, Loya na Tura wanasafiri umbali zaidi ya kilometa 180 - 200 kufuata vitambulisho mkoani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Serikali naomba sana zoezi la vitambulisho warudie tena kuandikisha kwenye kata zetu ili wananchi wengi wapate vitambulisho kuliko usumbufu wanaoupata wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na malalamiko mengi ya OCD wangu wa Wilaya ya Uyui, unyanyasaji wa kituo cha polisi wamekuwa wanawabambikia kesi sana hasa waganga wa kienyeji. Naomba sana Serikali kuchunguza juu ya mwenendo wa OCD Uyui amefikia anakamata watu anawaweka ndani mpaka siku kumi bila hata kuwafikisha mahakamani mpaka Diwani na Mtendaji wa Kata ya Miswaki amewakanata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba msaada wako kufanya uchunguzi wa kina juu ya polisi Uyui.