Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Awali ya yote nakushukuru kwa udhati wa nafsi yangu kunipa nafasi hii adhimu ambayo nilikuwa naamini nitaipata. Baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu, napenda sana kumshukuru Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna usukani alivyoukamata barabara kutuongoza katika nchi yetu. Nchi imetulia, nchi ina amani wawekezaji wanakuja, hakuna longolongo ndogondogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo kwamba Zanzibar nimewahi kusikia hotuba moja ya Mheshimiwa Dkt. Samia kwamba ni eneo maalum tengefu kwa kuwa limezungukwa na square mita 2,800 za mraba na zote hizi square mita zimezungukwa na bahari yote. Kwa hiyo, nikawahi kumsikia kwamba linahitaji kupata zana za kisasa ili liwe na ulinzi wa kisasa kuepukana na maharamia ambao wanaidowea nchi yetu. Kwa hiyo, naamini timu nzuri inayoongozwa na Ndugu yangu Mheshimiwa Masauni na Mheshimiwa Jumanne wanaweza wakakidhi haja ya nchi yetu kupata ulinzi imara ndani ya bahari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ni mbaya mno, walishawahi kunyemelea nyemela eneo la Kaskazini Pemba lakini Majeshi yetu ya Ulinzi yalikuwa imara na yakawafukuza wale maharamia. Kwa hiyo, ipo haja kupata mgao maalum wa zana za baharani pamoja na zana za nchi kavu ili shughuli za Jeshi la Polisi ziweze kuimarika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu niingie katika Bunge hili nilizungumza kuhusu Kituo cha Polisi cha Chukwani ambacho ni cha ghorofa, nikapata matumaini katika bajeti iliyopita kwamba kitajengwa au kitamaliziwa maana yake wananchi wamechangia milioni 60 wenyewe kukijenga. Nikapata matumaini kwamba katika bajeti tunayoendelea nayo, ziko zimetengwa milioni 60. Nimekwenda panda shuka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi nimeonana na Kamishna wa Polisi, sijapata matumaini ya aina yoyote kiasi kwamba nimeanza kuvunjika moyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo natumia nafasi hii kuwaambia kwamba mimi sina nia hata siku moja ya kuzuia shilingi ya mtu yeyote, hata mia! Naomba nipate maelezo kamili ya kituo kile juu ya wananchi waliochangia milioni 60 nguvu zao na baadhi ya wengine ni wageni baada ya matokeo makubwa ya uvunjifu wa amani. Wameshakufa watu watatu na akitaka nani na nani nitamuambia, Wazungu wawili wamekufa mwaka jana, kwenye uchaguzi kuna Mzungu alivamiwa na mmoja Mwanasheria ambae alikuwa anashughulikia uchaguzi, mwanae Mwanasheria Hamili kadhalika alivyamiwa. Kwa hiyo, hali ni mbaya mno. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo machache naomba sana nipate jibu rasmi ya kuwa kile kituo ni lini kitamalizika lakini yote kwa yote naunga hoja mkono asilimia 100. Ahsante sana. (Makofi)