Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia Wizara hii ya Mambo ya Ndani. Kabla sijaenda katika mchango wangu kwa moyo kabisa wa dhati naomba nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan. Pamoja na mambo mengine mazuri sana ambayo anaendelea kuyafanya, Mheshimiwa Rais ameweza kuweka utulivu katika nchi, ameweza kuweka amani na ametengeneza mshikamano. Lakini zaidi sana Mheshimiwa Rais ametufanya Watanzania kuwa wamoja bila kujali itikadi zetu za vyama lakini pia bila kujali itikadi zetu za dini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa leo nitakwenda kujikita katika hoja moja inayohusiana na uraia pacha. Mnamo tarehe 15 mwezi wa tano, 2023 nilisimama mbele ya Bunge lako tukufu nikihitaji kupata ufafanuzi kutoka kwa Serikali ni kwa nini inapata kigugumizi kuhusiana na suala zima la kuwapatia wenzetu diaspora haki yao ya msingi kwa maana ya uraia pacha. Majibu ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ndiyo yanayonisababisha hivi leo nisimame kuchangia kuhusiana na suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua hoja yangu ya leo itakwenda kugusa Wizara ya Mambo ya Ndani lakini pia itakwenda kugusa Wizara ya Mambo ya Nje. Sasa kwa sababu Wizara ni moja kila Waziri atanisikiliza kinacho muhusu basi atakwenda kukijibia katika eneo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema nitakwenda kuchangia suala zima la uraia pacha. Tunafahamu na tunatambua wazi wazi kwamba wapo watanzania wenzetu ambao tunawaita ma diaspora ambao walizaliwa katika nchi hii ya Tanzania, wamezaliwa katika Mikoa hii ya Tanzania katika vijiji na vitongiji ndani ya Tanzania. Diaspora hawa, hawa Watanzania wenzetu wazazi wao uhalisia wao ni Utanzania ni Watanzania na kwa lugha nyingine Watanzania hawa na wenyewe ni Watanzania kwa kuzaliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunatambua kwamba wapo diaspora ambao wamekulia ndani ya nchi hii kwa maana ya kukulia, wamelelewa lakini Watanzania hawa wamepata elimu zao ndani ya Tanzania, na wengine wamesomeshwa na kodi za Watanzania wanyonge wakiwa ndani ya nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua na tunafahamu kwamba hata sisi tulio katika Bunge hili tumeacha mikoa yetu, vijiji vyetu tunakwenda katika miji mingine kama ni Dar es Salaam Mbeya au ni wapi kwa lengo moja la kutafuta maisha kwa sababu Mtanzania yeyote ana haki ya kwenda popote kwa ajili ya kutafuta maisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania hawa waliondoka ndani ya Tanzania wakiwa wamepitia process zote za kiusalama kwa maana ya uhamiaji. Watanzania hawa walipewa passport na uhamiaji. Na kwa lugha nyingine, watanzania hawa Serikali iliwathibitisha kwamba ni Watanzania safi, ni Watanzania wazalendo, na ikawapa kibali cha kwenda kutafuta ng’ambo ili mwisho wa siku waje kuifaidisha nchi yao au Taifa lao la Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua suala zima la ajira nchini ni changamoto sugu. Kwa hiyo tunapopata Watanzania wenye elimu, wenye uwezo wa kwenda kule kwenye mataifa mengine ili waweze kutafuta tunapaswa kama Taifa kuhakikisha watu hawa tunalinda uraia wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua kwamba zipo nchi ambazo ili uweze kupata kazi, ili uweze kufanya biashara, ili uweze kufanya lolote ndani ya nchi hiyo huna budi kuwa na uraia wa pale. Wakati naongelea hili naomba tujikumbushe. Nimesema Watanzania hawa walitoka nchini wakiwa ni salama salimini, kwa maana ya vyombo vyote vya usalama vilithibitisha kwamba hawa watu ni safi kabisa. Sasa, walipofika katika mataifa yale, kwa sababu wameingia katika nchi hizo na wanaonekana ni watu safi na wana passport za Tanzania na ni wazalendo wakaamua wawape uraia ili waweze kufanya maisha yao kuwa mazuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukubaliane jambo moja; kwamba hakuna sababu yoyote ile ya kisheria inayopaswa kumwondolea Mtanzania uhalisia wake wa kuzaliwa. Nayasema haya kwa sababu gani? Mnamo mwaka 1995 ndani ya Bunge hili ilitungwa sheria kandamizi inayohusiana na uraia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante sana muda wako umeisha.

MHE.AGNESTA L. KAIZA: How can it be?