Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nakushukuru kwa kunipa hii nafasi ya kuchangia leo kwenye bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani lakini kipekee nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri, kaka yangu Engineer Masauni lakini Naibu Waziri kaka yangu Sagini kwa kazi kubwa mnayoifanya. Nimshukuru sana Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Rais kule kwetu Manyoni amefanya mambo makubwa sana. Ameleteta miradi mingi sana lakini vilevile ametusaidia sana kwenye upande wa Jeshi la Polisi. Ninamshukuru vilevile Katibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Naibu Katibu Mkuu kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya kwa Taifa letu lakini ususani katika Jimbo la Manyoni Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi leo na maeneo mawili takayoenda kuchangia. Eneo la kwanza tachangia upande wa Jeshi la Polisi lakini nafasi ikininiruhusu tachangia kuhusu Jeshi la Zimamoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee nimshukuru vilevile RPC wa Mkoa wa Singida Afande Stella. Kwa kweli huyu dada yetu ametusaidia sana sisi Manyoni. Manyoni kulikuwa na mauaji yaliyokuwa yakiendelea, niliongea hapa Bungeni, lakini vilevile Mheshimiwa Waziri ulitoa maagizo kwa Afande Stella na ukafanya mabadiliko pale Manyoni. Tumepata OCD mpya lakini na taarifa tayari mmeleta mmpelelezi bado hajafika. Kwa hiyo nimshukuru sana Afande Stella lakini kipekee nikushukuru sana Waziri na Naibu Waziri kwa kulichukua hili kwa umakini kabisa na hali ya usalama Manyoni inaendelea kuimairika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini upande wa Jeshi la Polisi kuna suala la Vituo vya Polisi vya Kata. Wenzangu wametangulia kusema, Mheshimiwa Idd ameongea hapa, katika Jimbo langu la Manyoni Mashariki maeneo mengi kwanza hayana Vituo vya Kata vya Polisi lakini Vituo vya Kata vingi vya Polisi ni vibovu na ni vichakavu. Kwa mfano na Kituo cha Kata cha Sanza ni kibovu sana, lakini hata pale Heka ni kibovu sana. Mbaya zaidi nilishawahi kuchangia hapa Bungeni, katika Kata ya Kintinku pale Askari na Polisi wanatumia gala la EFAD kama kituo cha polisi. Hii ni aibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe kaka yangu Engineer Masauni, naomba unisaidie tuanze na hili la Kituo cha Polisi katika Kata ya Kintinku. Lakini pia nina Kata zaidi ya nane ambazo hazina vituo vya polisi, zikiwemo Kata za Sasilo, Chikola, Makutupora, Kata ya Saranda na Kata ya Majiri. Nafasi itakapo ruhusu niwaombe basi na hizi kata nazo tuweze kuziangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine kwenye hii Kata ya Kintinku ulimuagiza RPC, Afande Stella; alishafika katika Kata ya Kintinku akakagua eneo wananchi wametenga ekari tatu kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha polisi cha kata. Kwa hiyo tayari sisi tuna eneo ekari tatu na Naibu Waziri uliniaidi utakuja kuliona hilo eneo, bado ujatimiza kaka yangu Sagini; nakuomba ufike ili uweze kuliona hilo eneo. Lakini ningeomba kwenye bajeti ya mwaka huu twende tukawajengee kituo cha polisi katika Kata ya Kintinku lakini mnifikirie vilevile kwenye kata hizo zingine nilizozitaja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ni uhaba wa vitendea kazi upande wa polisi. Katika Wilaya ya Manyoni kulikuwa na mauaji sana yaliyokuwa yakiendelea lakini hali imeanza kutulia RPC wa Mkoa alimua kuchukua gari kutoka Mkoani kulileta Manyoni kwa sababu Manyoni hawana gari. Nikuombe Mheshimiwa Waziri, itakapotookea fursa ya magari utuletee gari la polisi Wilaya ya Manyoni ili liweze kusaidia katika doria mbalimbali. Lakini vilevile umesema hapa mnaende kununua pikipiki kwa ajili ya vituo vya kata. Naiomba hiyo fursa vilevile kwenye vituo vyangu vya kata vya polisi ili anagalau tuweze kupata hizo pikipiki ziwasaidie ndugu zetu na watu wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuhusu Jeshi la Zimamoto. Kaka yangu Shabiby ameeleza hapa, na mimi naomba niongee hili. Mheshimiwa Rais anazunguka duniani kutafuta wawekezaji. Ile Filamu ya Royal Tour imeleta wawekezaji wengi sana, watu wamekuja wanawekeza. Lakini tuna tatizo moja, zimamoto ya Tanzania ni kama mtoto yatima, amesahaulika ndugu zangu. Unaenda kwa mfano mkoani pale tuna gari moja la zimamoto nalo ni bovu. Sisi tuna wilaya takribani sita, hakuna hata gari moja kwenye wilaya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale kwenye Jimbo langu la Manyoni nina miradi mikubwa. Tuna ujenzi wa shule ya wasichana ya bilioni nne, tuna mradi wa bilioni 12 wa maji, lakini tuna ujenzi wa VETA tumepewa 1.4 bilioni; hii miradi inajengwa, it’s very risk, hatuna zimamoto pale Manyoni, wamejenga kaofisi utafikiri banda la kuku. Mheshimiwa Waziri naomba ufanye mageuzi kwenye Jeshi la Zimamoto. Huu uwekezaji ambao mnauleta hatutatengeneza confidence kwa wawekezaji kama mtu anakuja kuweza billions of moneys halafu hakuna uhakika wa Zimamoto, it’s so risks. Kwa hiyo nikuombe kaka yangu Engineer naomba sasa mkatoa kipaumbele sana kwenye Jeshi la Zimamoto huko ndiko ambako tunahitaji kutengeneza confidence kwa wawekezaji. Mwekezaji anapokuja akagundua kwamba tuna Zimamoto, tuna mifumo ya zimamoto, tuna magari tuna ofisi, tunawafanyakazi anakuwa na uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tuna pigana kujenga viwanda kila eneo lakini unakuta maeneo mengi hayana zimamoto. Kaka yangu pale Shabiby amesema Gairo pale, hapa penyewe mjini ametolea mfano, tuna majengo mengi ya Serikali kule Mtumba, lakini tukiuliza mifumo ya zimamoto, magari ya zimamoto ni machache sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zimamoto ni mtoto yatima, sasa tunataka asiendelee kuwa mtoto yatima, kwa sababu Rais amepeka nguvu nyingi kwenye uwekezaji, tunahitaji kuweka nguvu nyingi na sisi katika kuimarisha Jeshi la Zimamoto… (Makofi)

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Chaya, taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Saashisha.

TAARIFA

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nataka nimpe taarifa tu kwamba hapo awali miaka ya 80 Jeshi la Zimamoto lilikuwa linasimamiwa na local government, kwa maana ya uendeshaji wake ulikuwa chini ya TAMISEMI. Tumeisha shauri hapa nyingi; kama huku imeshishindikana basi bora warudishe kwenye halmashauri hizi zenye nguvu ili waweze kuhudumia chombo hiki na ufanisi uweze kuonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kumpa taarifa hiyo tu. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Chaya taarifa unaipokea?

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa hiyo taarifa lakini bado mimi nisinge shauri lirudi halmashauri. Bado Wizara hii hii ya Mambo ya Ndani inayo uwezo wa kusimamia hiki kitengo cha zimamoto kwa sababu uwezo wanao, watalamu wanao, tukipeleka huko halmashauri tunaweza tukaleta matatizo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi bado naendelea kuishauri kwamba tunahitaji kuhakikisha tunaweka nguvu sana kwenye Jeshi la Zimamoto. Huu uwekezaji ambao tumesema tunawekeza Mama Samia amezunguka nchi nzima anavutia wawekezaji wamekuja Tanzania, wanaweka viwanda, wanaweka mitambo lakini hatuna mifumo mizuri ya Zimamoto kwa hiyo niombe Serikali sasa katika bajeti hii na bajeti ijayo… (Makofi)

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Chaya kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Esther Matiko.

TAARIFA

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimi Mwenyekiti, nilikuwa nataka nimpe taarifa Mheshimiwa Dkt. Chaya kwamba ingefaa kwa zile Majiji au halmashauri zenye uwezo waweze kuchukua hili suala la Zimamoto maana yake tumeo fedha tunatenga kwenye Wizara lakini haziendi. Kwa hiyo ukiacha ile pesa ya Mambo ya Ndani tutaendelea kuona rasilimali za Watanzania zikiteketea kwa sababu hatuna vyombo vya zimamoto, kwenye Halmashauri zenye uwezo zipewe jukumu la kuwa na hizi zimamoto, zitasaidia sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Dkt. Stephene Chaya taarifa unaipokea?

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa hiyo taarifa na nakubaliana na Esther Matiko kwamba kwa Majiji ambayo yenye uwezo wa kununua hii mitambo ya zimamoto wanaweza wakanunua lakini bado hili ni jukumu la Wizara, ninaamini kaka yangu MheshimiwaMasauni bado hajashindwa na ndiyo maana namshauri sasa, kwenye bajeti hii tunataka kuona mnaenda kuwekeza kwenye zimamoto. Wizara mna uwezo wa kusimamia hii sekta, tunataka uwekezaji mkubwa ambao Mheshimiwa Rais anavutia sasa hivi, tutengeneze confidence kwa wewekezaji, hakuwezi kuwa na confidence kwa wawekezaji kama kuna risk kubwa hususana kwenye suala la zimamoto, kwamba mifumo yetu ni mibovu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo mimi niendelee kumshukuru sana Mheshimiwa Waziri, kwakweli kaka yangu Masauni unafanya kazi nzuri sana. Kwanza ni msikivu, pia Mheshimiwa Naibu Waziri ni msikivu, mara nyingi unapokea simu zetu unajibu meseji hata usiku. Baada ya kusema haya naunga mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)