Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. CONSTATINE J. KANYASU: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ije na mkakati wa kukuza mawasiliano kutokea vijijini, kwa sasa habari zinazotolewa asilimia 95 ni za mjini pekee, hivyo kuna haja ya kuja na mkakati wa kuupatia umma mzima haki ya kutoa na kupata habari.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ishugulikie tatizo la waandishi zaidi ya asilimia 90 kufanya kazi kama vibarua, hawalipwi mishahara na wale wenye mishahara hawalipwi kwa wakati, Wizara iunde timu maalumu kupitia kila chombo kujua haki za watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Wizara kwa kuja na hoja ya minara mingi nchini, lakini bado matumizi ya minara yanatufanya kuwa analogue siyo digital, sasa hivi nchi nyingi zinatumia satellite, kwa nini tusiwekeze huko kuachana na minara?