Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Dr. Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya na hatimaye kupata nafasi ya kuchangia kwenye Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Naibu Spika, niungane na wenzangu kumshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. Kwa kweli ameendelea kufanya mambo makubwa kwenye nchi yetu, ameendelea kuifungua Tanzania lakini kwa mkataba huo tulioshuhudia wa utiaji saini, ujenzi wa minara zaidi ya 700 ni kielelezo tosha kwamba Mheshimiwa Rais anafanya kazi nzuri isiyo na mfano.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Habari kwa kazi nzuri anayoifanya pamoja na Naibu Waziri na watendaji wake wote. Mheshimiwa Naibu Waziri, Wizara hii ndio coordinator wa Wizara zingine. Wizara hii ikifanya vizuri wote tunakubaliana kwamba mawasiliano kwa sasa ndio habari ya dunia. Habari ya TEHAMA kwa sasa ni habari ya dunia, Mheshimiwa Waziri Nape anafanya kazi nzuri, anafanya kazi nzuri na kwa kweli tunajivunia namna ambavyo Tanzania inakwenda kidijitali, hakuna mfano. (Makofi)

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

TAARIFA

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kumpa taarifa mchangiaji anachangia vizuri sana kuisifia na kuwasifia Waziri na Naibu Waziri na kwa ushahidi tu ni kwamba Jimbo la Kilolo limepata minara tisa na kata tisa ambazo hazikuwa na minara zote sasa zinaenda kuwa na mawasiliano. Kwa hiyo sifa anazozitoa ninao ushahidi na nimependa kumpa taarifa ili aelewe kwamba hakosei. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Amandus taarifa hiyo.

MHE. AMANDUS J. CHINGULE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa hiyo naipokea kwa sababu ndio hali halisi iliyoko kwenye maeneo yote ya Tanzania kwa sasa. Kwa kweli tukipongeza kitu ambacho kiko wazi kila mmoja anakubaliana na sisi na ndio maana hata michango ya leo ya Waheshimiwa Wabunge imekuwa ni ya kidijitali kama ambavyo Mheshimiwa Waziri amesoma hapa na mimi nitajitahidi kutumia dakika chache sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri sana umefika Nachingwea, wakati wa kampeni ulikuja kufanya kampeni kule Nachingwea na nakushukuru sana. Yako maeneo kwenye Jimbo la Nachingwea ukifika unazima simu kwa sababu haina kazi tena, inakuwa ni kama kopo. Baada ya hapo maana yake ni kwamba kuna maeneo ambayo sasa hayo ndiyo unaweza ukatumia simu. Sasa nishukuru kwanza Serikali na nimshukuru Mheshimiwa Waziri nimeona hapa kwenye ukurasa wa 100, nimeona minara inakuja Nachingwea.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa pamoja na shukrani hizo nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, jiografia ya Nachingwea ni kubwa, nimwombe kwa heshima na unyeyekevu mkubwa atuongezee minara Nachingwea, tuongezewe minara ya Nachingwea. Mji wa Nachingwea kwa namna ulivyo jiografia yake Waziri anafahamu, misitu ni mingi na mbuga kule Selous anajua ipo. Kwa hiyo ukienda katika baadhi ya maeneo, kwa sababu ya miti na maeneo yale kuwa na mbuga hii ya Selous, unakosa mawasiliano kwa namna ya jiografia ya wilaya yenyewe ilivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilisema kwamba nitazungumza kwa ufupi sana. Mheshimiwa Waziri aendelee kuchapa kazi, aendelee kuchapa kazi. Sisi tupo na tunaona kazi inayoendelea na kwa kweli hata suala la utapeli wa kwenye mitandao, niwaombe tu hao ndugu kama wapo na wanasikia, watafute shughuli zingine za kufanya. Kwa namna spidi ya Wizara hii inavyoendelea ni imani yangu kwamba muda si mrefu hao nao wanakwenda kufa. Sasa ili wasife kifo kibaya cha kutangazwa kwenye mitandao, wakati ni huu wa kujisalimisha kuacha shughuli hiyo na kutafuta shughuli nyingine halali ambayo itawapatia kipato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, naunga mkono kwa asilimia mia moja. (Makofi)