Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi ya kuanza kuchangia. Kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema na leo tuko hapa salama kabisa. Pia, tumpongeze Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka fedha nyingi sana kwenye Wizara hii ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Waziri, rafiki yangu Nape Nnauye na Naibu Waziri, Engineer Kundo, kwa kazi nzuri sana ambayo mnafanya na tukianzia na hafla ile ya kusaini mikataba kwa ajili ya minara karibu 158. Kwa kweli hongereni sana ile ilikuwa ni innovation nzuri sana na sisi tunaotoka vijijini mmetufurahisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wizara hii ni muhimu sana. Huko duniani sasa digital economy ni kitu muhimu sana na ndio dunia ya sasa inakokwenda. Pia, nilikuwa nasoma ripoti ya World Bank hapa tunaambiwa digital economy ina range between 14 to 16 percent ya GDP. Kwa hiyo, ni eneo zuri sana na lazima kwa kweli tuendeleze na tuweke pesa nyingi zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Katibu Mkuu na timu nzima ya wizara hii na hasa hasa Mkurugenzi wa UCSAF unajua sisi tunaotoka vijijini ni lazima tumsifie Mkurugenzi wa UCSAF, I think she is the best CEO in my opinion. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niliandika ripoti hapa 2021, Mheshimiwa Waziri, nilileta kata karibu 15 za Kiteto zilikuwa na shida ya mawasiliano lakini leo kwenye bajeti yako hapa nimefurahi sana. Nimesoma ukurasa wa 100 nimekuta kata 12 zipo kwenye minara hiyo. Kata za Laiseri vijiji vyote kata hiyo ilikuwa haina mnara hata mmoja leo naona hapa. Mheshimiwa Waziri, nakushukuru ulimtuma Mheshimiwa Naibu Waziri, alifika Kata hii ya Laiseri. Kwa hiyo, wananchi wa huko Kiteto wa Kata ya Laiseri, Lengatei, Loolera, Magungu, Namelock, Partimbo, Sunya, Loitepesi, Songambele, Peresa, Njoro, Dosidosi, Ndirigishi. Sasa, tutaachaje kusifia kwa namna hiyo? Honestly kata karibu 12 na vijiji zaidi ya 23. Mwenyezi Mungu awabariki sana na wananchi wa Kiteto kwa kweli watakuwa wamefarijika na bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, liko jambo hapa la wizi unaotokana na mitandao. Imekuwa ni janga kubwa kidogo na linawasumbua sana watanzania walio wengi. Ninakuomba sana Mheshimiwa Waziri, tuendelee kuongeza teknolojia ili wezi hawa na matapeli wa mitandao wasiwatapeli watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, tumekuwa unajua kwa mujibu wa Sheria kila mtu anatakiwa aripoti kosa na tumekuwa tuki–volunteer. Hawa matapeli wanaotupigia tumekuwa tunaripoti kwa makampuni ya simu. Ambacho hatupati ni feedback kutoka kwa makampuni ya simu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima mkampuni ya simu yatuambie kama wateja kwamba ile simu uliyoripoti na sisi tumefanya moja, mbili, tatu na tunaendelea. Hiyo itajenga customer care nzuri. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri, wewe waandikie makampuni ya simu hapa. Haiwezekani sisi turipoti halafu tena wakati mwingine wanasema kabisa kwa quality control tunarekodi hii simu yako tusikilize halafu tunaripoti hizi simu na hawatupi mrejesho. Wakifanya hivyo itasaidia kupunguza wizi huo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Mheshimiwa Waziri, vyombo vya habari. Vyombo vya habari ni sekta muhimu sana na kwa kweli nakumbuka incident yako moja wapo jana nilikuwa naangalia YouTube, vyombo vya habari vilifanya kazi nzuri sana. If it wasn’t wao sijui tukio lile lilikuwaje. Kwa hiyo, please wasaidie sana na mkae. Ni taaluma ambayo ni nzuri sana inatupatia habari na kupata habari ni jambo la kikatiba.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Waziri, alisema Mheshimiwa Rais, siku ile ya kusaini mikataba, kwa sababu ya Sheria hizi za manunuzi kutengeneza mlolongo ambao ni bureaucracy kubwa inachukua muda wakati fulani, tungependa minara hii ifike vijijini kwa haraka. Pia, Mheshimiwa Rais, alisema mwezi mkoja tu na ilikuwa tarehe 13 karibu wiki moja sasa hivi imekwishakatika. Sisi ambao tumefurahi kupata minara hii tunategemea baada ya mwezi mmoja vibali vile vinavyotakiwa viwe vimepatikana lakini lazima mlete Sheria ya Procurement tuangalie ipunguze hii bureaucracy.

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani tupate pesa halafu tuendelee kukaa miezi sita, nane kwa sababu ya kuleta vifaa. Tunataka wananchi wapate huduma hii kwa haraka sana. Nadhani kwa sababu tunazungumzia habari ya kidijitali na TEHAMA, nilifikiri wewe ungekuwa na regime tofauti kabisa. Yaani wewe lazima uende haraka zaidi kuliko wengine. Haiwezekani wewe uwe na sekta hii ambayo tunazungumza habari ya kidijitali halafu bado Procurement Law ile ambayo inachukua muda mrefu zaidi inafanya kama vile ni manual system.Vile vile, hata hapa Mheshimiwa Naibu Spika, amesema wewe umetumia muda mfupi sana hapa, hiyo ndio TEHAMA, ndio digital. Kwa hiyo, lazima ninyi muwezeshwe mwende haraka zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, nilizungumza mwaka 2021 na 2022, kuhusu Radio Tanzania kutokusikika Kiteto lakini vilevile nafarijika kwenye hotuba yako ya mwaka 2022 na hata safari hii nimeona Kiteto ukurasa wa 125 kwamba mtaongeza usikivu, watanzania wale wa Kiteto ni vema wakaanza kufuatilia redio yao ya Tanzania. Haiwezekani miaka 60 baada ya uhuru bado wana Kiteto hawapati taarifa kutoka redioTanzania. kwa hiyo, nakushukuru sana kwamba Kiteto sasa itafunguka.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Mheshimiwa Waziri, suala hili la mawasiliano, tulikuona ukienda Mlima Kilimanjaro kupandisha internet. Unajua wakati tunapandisha Mwenge wa Uhuru Mlima Kilimanjaro kulikuwa na quotation nzuri sana ya Baba wa Taifa. Sasa lazima tuwe na slogan sasa kwa kuwa Mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu Afrika lazima tuwe na slogan ya kupandisha ile na mantiki yetu ni nini?

NAIBU SPIKA: Ahsante, ahsante.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ya muda naunga mkono hoja na Mungu awabariki sana.