Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Wakati najiandaa asubuhi ya leo kuja kuchangia Wizara hii wezeshi kwa sekta zote za uzalishaji nchini, nilimwomba Roho Mtakatifu anipe hekima, maarifa na busara ili niweze kuwatendea haki Watanzania wote wa nchi hii siku ya leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuja na Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/2025, nimekuja na hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati anahutubia Bunge. Wakati najianda kuchangia, labda nieleze maeneo nitakayopita, eneo la kwanza ni kuhusu mradi, matumizi ya fedha za mradi wa bilioni 345 ambazo ni mkopo wa Benki ya Dunia, mkopo ambao kila Mtanzania atalipa, mimi nitalipa, wananchi wa Mlimba watalipa na wananchi wa Mlimba wameniambia katika hili hapana, wengine mkikubalia sawa lakini wananchi wa Mlimba wamesema hapana! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni migogoro ya ardhi, eneo lingine ni usimamizi wa watumishi wa sekta ya ardhi na mwisho nitahubiri kidogo injili. Nianze na mradi wa bilioni 345 mkopo kutoka Benki ya Dunia. Nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kulihangaikia Taifa letu kwa kutafuta fursa mbalimbali huko Duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha hizi inasikitisha matumizi yake. Tumeambiwa na Kamati hapa bilioni takribani 46.8 zinakwenda kwa ajili ya uratibu, uendeshaji na dharura, katika Taifa ambalo limepimwa kwa asilimia 25 tu, katika Taifa ambalo lina vijiji takribani 12,318, vilivyopimwa ni viijiji 2,868 tu. Katika Taifa ambalo vijiji ambavyo havina mpango wa matumizi bora ya ardhi ni takribani 9,541, katika Taifa ambalo wananchi wamekuwa wakifa kila siku, watu wanakufa kutokana na migogoro ya ardhi, inasikitisha! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwa dhati maana ukichangia hapa kuna minong’ono huku wanasema huyu anataka uwaziri, kama uwaziri unakuja kwa ajili ya kuchangia acha uje tu! Kama kwa style hii acha uje tu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, I am not speaking out of nothing, I am speaking on something that I know, nazungumza jambo ambalo nalifahamu sekta ambayo naifahamu vizuri sana na nime–practice sibahatishi kwenye ardhi na nimeweka matokeo makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nieleze katika fedha hizi matumizi yake vijiji 500 tu vinakwenda kupimwa na thamani ya kupima kijiji, gharama ya kupima kijiji kimoja ni milioni 12 mpaka Milioni 15, kwa hiyo kwa vijiji hivi vilivyotajwa 500 itatumika fedha bilioni 5.5 tu katika mpango wa fedha bilioni 345 are we serious? are genuine? ni kweli tunamsaidia Mheshimiwa Rais? ni kweli are genuine? au tunasema tu mdomoni mioyo yetu inakataa, hapana mi bado ni kijana mdogo nategemea kutumikia Taifa langu kwa miaka ijayo. Kwa hiyo no matter what will happening to me lakini leo tasema ukweli daima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeeleza hapa nilijaribu kufanya tafiti kidogo nikajiuliza maswali asubuhi…

MHE. SOUD MOHAMMED. JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kunambi kuna taarifa.

TAARIFA

MHE. SOUD MOHAMMED. JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba tu kumpa taarifa Mheshimiwa Kunambi kwamba upimaji wa ardhi ni process, siyo kama labda ni upimaji wa ardhi utapima tu mara moja. Kwa hiyo nilikuwa naomba tu kumwambia kwamba upimaji huu ile miundombinu ambayo inakwenda kutengenezwa ina saidia kuweza…

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, naomba tusikilizane.

MHE. SOUD MOHAMMED. JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba tu kumfahamisha Mheshimiwa Kunambi kwamba ile miundombinu kwamba ambayo itakwenda kutengenezwa katika mradi huu wa uwishaji usalama na rasilimali za ardhi ndiyo utakwenda kusaidia kuweza kuipima ardhi kwa haraka baada ya kwisha kuitaarisha ile miundombinu. Ahsante sana.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Godwin Kunambi unaipokea hiyo taarifa?

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua unapoteza muda kwa mtu ambaye any way siipokei. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sina mzaha hapa! Nimefanya hesabu ndogo tu ya kujumlisha na kutoa ambayo kila Mtanzania anaweza kuifanya. Ukipima vijiji 2,000 katika mradi huu fedha hii ya mkopo ambayo kila Mtanzania analipa, vijiji 2,000 thamani yake ni bilioni 30 tu. Ukipeleka bilioni 30 tu, na mimi nakutaarifu Mheshimiwa Waziri nakuja kushika shilingi nataka kuona bilioni 30 inakwenda Tume ya Taifa ya Mipango. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilijaribu kuangalia Ilani nimesema nimekuja na Ilani naomba niisome, naomba ninukuu Ilani ya Chama cha Mapinduzi Chama changu kwa ufupi Ibara ya 74 Ukarasa wa 120 mwenye Ilani arejee, naomba nisome Chama cha Mapinduzi kimeelekeza Serikali kwa miaka hii mitano kupanga na kupima vijiji takribani 4,131 na Wilaya 54.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika fedha hizi unaenda kupima vijiji 500 huu ni mwaka gani huu? Mwaka 2023 bado miaka hii miwili, kutoka 2021 mpaka sasa Wizara wamepima vijiji 618 tutafika lengo hili la Chama? Ndiyo maana nauliza are we serious? Are we genuine?

MBUNGE FULANI: No.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Hapa tunacheza na changamoto za Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikajiuliza kuhusu migogoro ya ardhi, nikauliza wenzetu wa jirani wa Uganda hivi kuna migogoro ya ardhi Uganda? Wakasema Hapana, nikauliza Rwanda kuna migogoro ya ardhi? Wakasema hapana. Nikauliza hapa Kenya kuna migogoro ya ardhi? Wakasema Hapana! Migogoro ya Ardhi ni matokeo ya kushindwa kwa sekta nchini, nataka nipigie mstari hapo, migogoro ya ardhi ni matokeo ya kufeli kwa sekta ya ardhi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi naomba nijielekeze kuhusu wasimamizi wa sekta ya ardhi. Kama kuna eneo Wizara imekosea kuwachukua watumishi kutoka Halmashauri kuwapeleka wakawasimamie mfano, wanasema TARURA, wanasema RUWASA, RUWASA ni taasisi inayojitegemea ndiyo maana ina perform, TARURA ni taasisi inayojitegemea ndiyo maana ina- perform, sasa Wizara imechukua tu watumishi mi nadhani basi waanzishe taasisi na wenyewe basi ili wapime na kupanga, iwe mamlaka ya upangaji isiwe tena Halmashauri wanawaonea tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa ya pili dakika mbili, hamna zaidi ya hapo, Mheshimiwa Musukuma.

TAARIFA

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Utanisamehe sana rafiki yangu Kunambi maana Bunge hili tuko live calculation unazozipiga unalipotosha Bunge na Watanzania. Kwa hesabu unazozipiga hata tunatoka kwenye Halmashauri, tunaongoza Halmashauri zetu tunajua tunapima kwa style gani, kuna kupima kwa kudhulumu na kuna kupima kwa kulipa haki za watu. Sasa calculation unazolieleza Bunge hapa na bahati nzuri wewe ulikuwa Mkurugenzi hapa na mimi nimewekeza hapa nime-deal na wewe, nakufahamu na Wabunge wote wako hapa, kwa style ya wewe uliyoifanya hapa tukiruhusu hizo hesabu zako Waziri akazichukua hii Tanzania tutachinjana kwa ajili ya ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kunambi, unapokea hiyo taarifa?

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei taarifa. Ninachosema ni kwamba kinachofanyika sasa unasema mamlaka ya nidhamu ni Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Mtumishi yuko Kakonko, mtumishi yuko Mlimba hivi utendaji kazi wake kule anajuaje? Anasema kuna Kamishna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamishna yuko ngazi ya Mkoa na niseme kuna mgomo Mheshimiwa Waziri kama hujui nakusaidia, kuna wale Watumishi mliyowashusha vyeo Wakuu wa Idara, mtu alikuwa na mshahara alikuwa na mshahara 3,400,000 leo hii anakuwa Afisa Ardhi wa kawaida, wamegoma kwenye Halmashauri huko. Ndiyo maana hilo nenda kafanye uchunguzi nakusaidia tu na uchukue tu positive mchango wangu, nakupa tu hiyo siri kuna mgomo unaoendelea, wale watumishi mliowashusha vyeo huko kwenye Halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyewkiti naomba nihitimishe, nahitimisha kwa mahubiri. Ukisoma…

MWENYEKITI: Muda wako umeisha.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti naomba dakika moja tu.

MWENYEKITI: Nusu dakika.

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Dakika mbili tatu. Mtume Paulo kwa Wakorintho aliwahi kusema habari hii kwa Wakorintho jamani tusikilizane kidogo “Nikiitazama Dunia ni ubatili mtupu” lakini ndugu zangu kizazi chetu ni cha nne, uhai wetu ni miaka 70 jamani tafuteni kwanza ufalme wa mbingu mengine mtazidishiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Quran tukufu inasema maneno haya; “Quburwa Twanii’h ninal manii” kuipenda nchi yako ni sehemu ya imani Watanzania tuwe wazalendo kwa Taifa letu. (Makofi)