Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi, kwanza ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa afya njema na tuko hapa leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili tumpongeze Mheshimiwa Rais Mama Samia kwa kuja na ubunifu wa EPC + Finance. Nilizungumza mwaka jana hapa kuhusu barabara hizi za Kongwa – Kiteto na Simanjiro na kwa kweli nimpongeze Profesa Mbarawa - Waziri wa Ujenzi, Engineer Kasekenya – Naibu Waziri Ujenzi, Mheshimiwa Mwakibete- Naibu Waziri Uchukuzi, Makatibu Wakuu na timu nzima kwa kazi kubwa ambayo kwa kweli mmefanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka nilizungumza hapa ilikuwa ni tarehe 17 Mei, 2021 nikawa nazungumza habari ya barabara hizi za Kongwa – Kiteto – Simanjiro mpaka Arusha, lakini nimezungumza habari ya barabara kutoka Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Chemba mpaka Singida. Leo jioni hii Mheshimiwa Waziri kwa kweli wananchi wa Kiteto wamefarijika sana. Nimesoma bajeti yako hapa na hotuba hapa ukurasa wa 11, kwamba Barabara ya Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Orboloti – Talai – Chemba - Kwamtoro mpaka Singida, kilometa 460 ipo kwenye mpango wa bajeti. Kwa kweli, nakushukuru sana Mheshimiwa Waziri na wananchi wa Kiteto kwa kweli wamefarijika sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili barabara ya kutoka Kongwa – Kibaya – Simanjiro mpaka Arusha vilevile naona hapa kwenye hizi barabara hizi kilometa 2,000 zinazojengwa kwa mpango huu wa EPC + Finance. Kwa kweli tumefarijika sana na hii kwa kweli itafungua sana siyo tu maendeleo kwenye Majimbo haya lakini uchumi kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uzuri wa barabara hii ya Tanga mpaka Singida kupitia Kiteto kwa kuwa tumeshafanya maamuzi kama nchi kujenga bomba hili la mafuta kutoka Hoima – Uganda mpaka Chongoleani – Tanga, barabara hii itasaidia sana kufungua uchumi na itakuwa inaendana na bomba la mafuta. Kwa hiyo, kwa kweli big up huu ni mradi ambao kwa kweli uta- complement vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ya Kongwa – Kibaya hizi barabara mbili hizi mimi naita ni barabara za vijijini. Kwangu tu Kiteto peke yake inapita zaidi ya vijiji 20, na kwa kweli Kiteto kutoka sasa kilometa nne za lami za pale Mjini ambazo hata taa hazina mpaka karibu kilometa 300 za lami baada ya hizi barabara zote mbili kujengwa, kwa kweli itafungua uchumi mkubwa sana.

Mheshimiwa Waziri huu mpango mpya wa EPC + Finance karibu sasa tutaitia majina ya watoto kule Majimboni EPC + Finance kwa sababu kila wakati tumekuwa tunasema kwenye mikutano ya hadhara, barabara zetu zitajengwa kwa EPC + Finance. Kwa hiyo, labda mtafute Kiswahili nzuri ya EPC + Finance kwa sababu ni kitu kizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizi kwa umuhimu wake, kilimo, mifugo na usafiri kwa wananchi ambao wanapitiwa na barabara hizi kwa kweli itaondoa changamoto ya muda mrefu sana ambayo kwa kweli wananchi wamekuwa nayo. Kwa hiyo, kwa kweli kwa Kiteto simu leo zimekuwa nyingi sana kutoka Kiteto huko baada ya bajeti hii kusomwa na kwamba wananchi wale wamesikia barabara zao. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri nakushukuru sana na Mwenyezi Mungu awabariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili tunasubiri sana kama ulivyosema hapa kwamba sasa tunachosubiri ni kutiwa saini kwa ujenzi wa barabara hizi na vizuri uemesema ni kabla ya Juni mwaka huu. Kwa hiyo, kwa kweli tunasubiria sana na hii tarehe kwa kweli mtufahamishe, hata baadhi ya wananchi wanataka kuja kabisa hata kuona mikataba hii ikisainiwa. Hii kwa kweli italeta maana kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoomba sasa kwa barabara hizi mbili kazi ambazo wananchi watakuwa na sifa nazo ni vema mkaongea na wakandarasi ili wananchi wanaotoka kwenye maeneo haya wakapate hizo kazi kwenye barabara hizi na mhakikishe kabisa kwamba wananchi wanalipwa. Kwa hivyo, kama wakandarasi kuna sifa za wananchi zipo huko basi na wananchi waweze kunufaika na tender za barabara hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie habari ya ATCL (Shirika la Ndege la Taifa). Mimi nadhani ni expensive sana ticket ya ndege ya ATCL ni ghali kidogo. Kwa hivyo, pengine ni vizuri mkaangalia namna kwa sababu Watanzania wanapenda kutumia ndege yao hii, imekuwa ni ghali kidogo. Jambo ambalo linasikitisha kidogo eti ni ukipiga simu saa mbili ya usiku wamelala! Sasa hiyo kwa kweli kwa nchi ambayo sasa imefunguka na tunataka tuanze kusafiri, inaeleweka kwa Uwanja wa Ndege wa Dodoma hakuna taa sawa, lakini kwa Arusha na Kilimanjaro na Dar es Salaam na Mwanza kwa kweli nashangaa sana kwa nini hawa ndiyo wanaenda huko, na simu ya customer care, sasa wakienda kulala na wao saa mbili kweli itakuwa Hapana! Lazima hilo tubadilishe kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru Mheshimiwa Waziri nimeona pia barabara ya Dongo – Sunya – Kijungu mmetengea bajeti kwenye hotuba yako na kwa kweli kubwa kwangu leo unajua nimeishiwa maneno, leo kwa mara ya kwanza baada ya kuona hizi barabara hizi mbili hizi, barabara hizi mbili ambazo tumezipigia kelele kwa muda mrefu sana kuona leo kwamba ziko kwenye mpango wa EPC + Finance na faida zake zinajulikana, for once nimekosa cha kusema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa tuwapitishie bajeti wakafanye hii kazi haraka sana. Ninakushukuru ahsante sana. (Makofi)