Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Hon. Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye hotuba iliyoko mbele yetu leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kutoa mchango wangu nichukue fursa hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya uhai na afya na kutujalia kuwa wazima na kuendelea kulitumikia taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nimshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kutoa fedha nyingi za kuendelea kumalizia miundombinu ya barabara na miradi mikubwa ya reli ya SGR na mambo mengi kwa ajili ya kuendelea kuijenga nchi hii. Pia, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kumwamini Waziri Profesa Mbarawa, kuendelea kuishikilia Wizara hii. Wewe Profesa Mbarawa ni true definition ya maana ya kiongozi. Umeendelea kuwa shupavu, umekomaa kumsaidia Rais, tunakuombea dua Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda, kukupa nguvu, wewe ni kiongozi mzalendo wa nchi hii. Kwa hiyo, tunakupongeza kwa juhudi kubwa unazozifanya kwa ajili ya kulitetea na kuliletea maendeleo taifa hili, hasa kwenye suala la miundombinu ya taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilikuwa na mambo mawili kwenye mchango wangu. Jambo la kwanza, tuna masikitiko makubwa sisi wakazi wa Tanzania wanaokaa Pemba na Unguja. Shirika letu la Ndege la Taifa (ATCL) ni keki ya taifa. Masikitiko yetu sisi bado hatu-enjoy keki hiyo. Kuna tatizo kubwa sana la safari za ndege kutoka Pemba kwenda Unguja na kutoka Unguja kwenda Pemba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ukitaka tiketi ya ndege inabidi uikate kwa wiki mbili kabla la sivyo huwezi kupata tiketi. Kukitokea dharura hakuna usafiri wa anga, usubiri meli na jambo ambalo nalo linasuasua. Kwa hiyo, wito wangu kwa Wizara hii waangalie uwezekano wa kutuwekea route japo mara moja kwa siku ili kutatua tatizo hili. Kama wamefanya tathimini na kuona ndege zao kubwa za Dash 8 - Q400 ni kubwa kwenda Pemba kwa sababu zinahitaji abiria wengi, niwahakikishie abiria wapo au tusubiri hyo ndege yao ambayo iko matengenezoni huko Malta ya Dash 8 Q300 itakapokuja Mheshimiwa Waziri upambane uhakikishe wakazi wa Pemba na Unguja wanpata ku-enjoy na wao keki ya taifa ya kuzitumia ndege hizi za Shirika la ndege la taifa, tunateseka. Kwa hiyo, nafikiria hilo ni jambo ambalo Mheshimiwa Waziri kwa sababu ni mzikivu atali-consider au atalizingatia kwa mapana makubwa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa pili ni kwamba, sisi Tanzania Mwenyezi Mungu ametujalia kuwa kwenye nchi kubwa sana kijiografia. Hiyo ni bahati tuliyopewa na Mwenyezi Mungu. Hii nchi tukisubiri tuijenge wote kwa pesa za ndani aidha tutashindwa au tutachelewa. Hayo mambo mawili yanaweza yakatokea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia imekwisha move huko, hao watu ambao wanatuzidi kila kitu, wanatuzidi per capital income, wanatuzidi makusanyo kwenye revenues, wanatuzidi kwenye GDP, wao aidha wako kwenye PPP au wako kwenye EPC + Finance. Kwa nini sisi masikini bado tunang’ang’ania kutumia kipato chetu kidogo tunachokipata kutaka kujenga miundombinu yote ya nchi hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda umefika tuwaachie private sectors waje wajenge baadhi ya sehemu kwenye miundombinu yetu. Viwanja vya ndege, bandari, barabara tunaziweza kuziendeleza tukazijenga kwa kiasi kikubwa kwa kutumia mtindo wa aidha EPC + Finance au PPP, ule ambao Serikali tutaona unafaa ili kusaidia hizi fedha kidogo ambazo tunazozikusanya au tunazipata zikaenda kusaidia kwenye mambo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo ni mengi; elimu Serikali, afya Serikali, welfare ya watu wa nchi hii Serikali, biashara Serikali, sasa tutafanya yote hayo na kipato chetu si cha kutosha? Kwa hiyo, tuwaachie private sector waingie waje watusaidie tuwabane kwenye negotiations ili wasaidie hiyo miundoimbinu ijengwe, hatutoweza kuvifanya vyote. Kama nchi kubwa kama Russia wamebakisha jeshi tu ndilo ambalo bado linahudumiwa na Serikali itakuwa sisi Tanzania? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, viwanja vya ndege vyote ni private owned (vinamilikiwa na private) na Serikali wana-joint venture, wanakusanya kodi, wanapata kipato na maisha yanaendelea. Hatutaweza, hii Tanzania ni kubwa, na kila siku watu wanasogea kwenye maeneo ambayo mwanzo yalikuwa hayakaliwi na watu. Wakisogea watahitaji barabara, wakisogea watahitaji wajengewe miundombinu hatutaweza halafu tutachelewa. Kwa hiyo, ushauri wangu tuondoke huku tuondokane na huu uzamani. Tuwaruhusu private sector waje wajenge sisi tuwabane kwenye mikataba na negotiations za kutusaidia sisi wasije wakatubana mbele ya safari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchangiaji aliyepita, Mheshimiwa Sangu amelalamika hapa kuhusiana na matrilioni na mabilioni ya fedha zinazokusanya kwenye certificates kwa kuchelewa kulipa riba. Haya yote yanatokana na fedha zetu kuwa ni kidogo, hatuna uwezo wa kuzigawa zote kwa pamoja ukalipa wakandarasi, huku elimu inataka kuhudumiwa, huku hospitali zinataka kujengwa, haiwezekani. Kwa hiyo, tuwaachie watu wajenge sisi tuwakamate tukusanye kodi zetu maisha yaendelee. Huo ndio ushauri wangu na tunaweza kwenda kwenye nyanja zote…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ahsante sana kwa nafasi hii na ninaunga mkono hoja. (Makofi)