Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, kwanza napongeza kazi nzuri ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya uboreshaji miundombinu ya elimu na uboreshaji wa bajeti ya elimu. Nampongeza pia Waziri Mheshimiwa Profesa Mkenda, Naibu Waziri Mheshimiwa Kipanga, Katibu Mkuu Profesa Nombo na wataalam wote wa Wizara kwa jinsi wanavyoendelea kuipaisha sekta ya elimu hususan kwa kufanya maboresho ya sera ya elimu na mitaala.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwanza suala la elimu ya awali lizingatiwe na kujumuishwa kama ni elimu ya lazima kwani hapa ndipo sehemu muhimu ya kumjenga mtoto.

Pili, kuna tatizo kubwa la uhaba wa walimu katika nchi yetu lakini vibali vya ajira ni vichache. Nashauri Serikali yetu ifanye kila liwezekanalo idadi ya walimu iongezeke kwani zipo shule zina madarasa ambayo hayatumiki kutokana na uhaba wa walimu.

Mheshimiwa Spika, tatu, wakati elimu ya amali itakapoanza ni vyema Serikali ikatumia mfumo wa PPP ili kuweza kupata mazoezi ya vitendo kwa wanafunzi wetu kutoka sekta binafsi. Kwa mfano wanafunzi wataweza kwenda katika garage, hoteli, maduka, vituo vya ushonaji nguo, mashambani na kwingineko ili kujionea na kushiriki kufanya shughuli husika kwa vitendo.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.