Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwanza mtihani wa darasa la saba usifutwe kwani hali hii itafanya walimu wasiwajibike. Wale ambao hawatafanikiwa kuendelea na kidato cha kwanza waingie kusoma masomo ya ufundi na iwe kwa mseleleko.

Pili, wahitimu wa kidato cha nne na darasa la saba ambao hawatafanikiwa kufaulu vigezo vya kusonga mbele hawa iwe lazima waingine elimu ya ufundi.

Mheshimiwa Spika, tatu, walimu wa kufundisha elimu ya msingi na sekondari ifundishwe na mwalimu ambaye alipata division one au two kidato cha nne na sita. Walioko makazini wataendelea kujiendeleza.

Mheshimiwa Spika, nne, Serikali ianzishe Wizara ambayo itasimamia mambo ya kujiajiri vijana ambayo itaitwa Ministry of Self Employment and Micro Business.

Mheshimiwa Spika, Serikali ipitie umri wa kustaafu uwe miaka 55 ili kutoa fursa ya vijana walioko mtaani kutumikia Taifa wakiwa na nguvu na kupata muda wa kujiajiri.