Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kuja na wazo la kupitia upya mitaala yetu. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na Makatibu Wakuu kwa utendaji mzuri katika sekta ya elimu.

Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika walimu wa vijijini kufundisha kutoka asubuhi mpaka saa 11 kasoro jioni, lakini walimu wa mijini wanamaliza kazi saa 8.30 mchana.

Mheshimiwa Spika, walimu wote mijini na vijijini, walimu wa vijijini wote wanahitaji muda wa ziada wa kujiandaa na masomo lakini pia kufanya kazi za kujiongezea kipato kama vile kilimo na ufugaji. Naomba sana sana muda wa kazi uwe ni mmoja.

Mheshimiwa Spika, elimu ya watu wazima ni jambo la muhimu, kuna wanaokosa elimu kwa sababu mbalimbali lakini pia kuna watu wazima wanaotaka kujiendelaza, hivyo Serikali iweke mpango wa kuendeleza elimu ya watu wazima.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.