Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, naungana na Watanzania wote kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutujalia baraka zake katika nyanja za ustawi wa kijamii, kiplomasia, amani na utulivu na kutuepusha na majanga mbalimbali katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuungana viongozi wenzangu wote, wananchi wote wa Jimbo la Mbulu Mjini na wote wenye mapenzi, kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali nzima kwa jinsi tulivyotekeleza Ilani ya CCM yam waka 2020-2025, kwa kweli kwa miaka miwili sasa yapo mambo mengi sana yaliyoshindikana huko nyuma na sasa tayari yamefanyika.

Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Profesa Adolf Mkenda, Waziri na Naibu Waziri, Kamati yetu, Katibu Mkuu na watendaji wetu wote katika Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, nachukua nafasi hii kuishukururu sana Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa kutupatia fedha za ujenzi wa mabweni mawili mwaka 2017 na 2018 katika Jimbo la Mbulu Mjini hivyo basi tunawaomba watusaidie ujenzi wa mabweni mawili katika Shule yetu ya Sekondari ya Kata ya Daudi (Marangw) kwa kuwa ni shule kongwe iliyoko maeneo ya wafugaji.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba kutoa mchango wangu kupitia mapendekezo ya bajeti ya Wizara hii muhimu sana ya elimu kwa maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Serikali itazame upya muundo wa ngazi za Wadhibiti Ubora wa Elimu kwani kwa sasa shule za sekondari nchini zimekuwa nyingi sana, hivyo basi kuwe na Wadhibiti Ubora wa Elimu ya Sekondari wawepo kwa ngazi ya kanda, mkoa na halmashauri kote nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie vigezo vya usajili wa vituo vya malezi ya watoto wadogo na elimu ya awali nchini hususan walimu wanaoajiriwa wengi wao hawana taaluma ya kutosha kwa ustawi wa Taifa unaanzia malezi na makuzi ya mtoto hivyo eneo hili ni muhimu liangaliwe vizuri.

Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie utaratibu wa kila halmashauri nchini kuwa na shule moja yenye kitengo cha elimu maalum kwani kuna kundi kubwa la watoto wenye mahitaji maalum ambao mazingira yao hayana huduma hiyo muhimu sana, kwa mfano Shule ya Msingi Endagikort katika Halmashauri ya Mbulu Mji ina wanafunzi zaidi ya 30 kwa miaka sita sasa hali inayofanya wanafunzi hao kusoma kwenye mazingira magumu sana, hakuna miundombinu ya madarasa, mabweni, vifaa vya kufundishia na walimu wa elimu maalum, ajira kutoka Serikalini.

Kwa hiyo, ninaomba Waziri wa Elimu afanye ziara mahususi katika Jimbo la Mbulu Mjini, kutembelea Shule ya Msingi Endagikort, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Tango FDC na Chuo cha Ukunga na Uuguzi Mbulu kwani maeneo hayo yana changamoto kubwa sana.

Mheshimiwa Spika, Serikali iangalie utaratibu mzuri wa matumizi ya vituo vya walimu (TRC) kwenye tarafa zetu nchini kwa kujikita kwenye misingi yake ya kuanzishwa kwani kwa sasa mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu na hayafanyiki na baadhi ya vituo havitumiki, hata hivyo uamuzi wa walimu waratibu kupangiwa vipindi vya kufundisha kwenye shule zilizoko karibu utasaidia sana kuongeza vipindi vya masomo kwa wanafunzi.

Mheshimiwa Spika, mwisho, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja na naomba kuwasilisha.