Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia fursa hii. Kwanza kabisa mimi nadhani nimpongeze Profesa anawizara ngumu ameuikuta pagumu anajitahidi enedelea kujitahidi, anajitahidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama kawaidia mimi natoa ushauri cha kwanza Profesa, hebu ile VETA ya Musoma Vijijini, na nilikueleza ukinipatia mimi VETA itakuwa ni ya mfano nchini; kwa sababu sitaki VETA ya mambo ya hoteli ya kutengeneza magari, hapana, mimi VETA yangu itakuwa mambo ya kilimo uvuvi na ufugaji. Naomba hiyo homework Profesa imalizie.

Mheshimiwa Spika, sasa Waheshimiwa Wabunge mimi natoa ushauri ifuatavyo. Elimu yetu, nilikuwa sipo, nimesikiliza, na ukweli ni kwamba iko kwenye hali mbaya, lazima kwanza tukiri hivyo. Lakini hakuna wa kulaumu, ni sisi wote. Tukitaka kumlaumu mtu ni kama hatujui tunalolifanya.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa muda umefika wa kujiuliza na pendekezo langu ni kwamba elimu ya awali kuipeleka TAMISEMI, imekaa TAMISEMI kwa muda matokeo yake siyo mazuri. Kama inawezekana, maana huko nyuma tulivyopeleka madaraka ya ndani si ndiyo tulifanya mabadiliko? Sasa tukifanya evaluation mabadiliko hajazaa matunda. Kwa hiyo mimi napendekeza, kwa sababu tumerudi nyuma Wizara ya Elimu irudishwe tena. Yaani mambo ya elimu yawe ndani ya wizara moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, inakuwa ngumu sana eti shule za msingi primary zinakuwa na Waziri wake na Ofisi zake ikifika university nayo na ya kwake halafu baadaye mnamlaumu huyu wa juu, mnamuonea, mnamuonea. Kwa hiyo mimi napendekeza Profesa lipeleke kwenye cabinet, mwambie PM alifikirie, uwe na wizara inaitwa Wizara ya Elimu, Sayansi Utafiti na Ubunifu Ministry of Education, Science, Research and Innovation. Huna haja ya kutaja teknolokjia, teknolojia kwa sababu innovation maana yake una innovate kwenye technology, kwa hiyo huna haja ya kuitaja. Hilo ni pendekezo langu la kwanza, tukifanya hivyo tutona mabadiliko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni miundombinu kwenye mashule yetu. Profesa wewe na TAMISEMI, yaani wizara mbili lazima mkae chini mkubaliane kwamba, ili tuwe na elimu iliyo nzuri na inaweka msingi mzuri lazima kila shule; vyumba vya madarasa sawa lakini ni wanafunzi wangapi? Kwa hiyo, homework yako ya kwanza na wahusika turudi nyuma tuone kama tutarekebisha. Huko nyuma enzi yangu Waheshimiwa Wabunge shule ya msingi tulikuwa 45, sekondari tulikuwa 35, high school tulikuwa 25. Sasa hebu turudi huko kwanza. Hii mitaala hata ukiwa nayo mizuri namna gani ikiwa wanafunzi wamerundikana madarasani hautafanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, shule yoyote inayoitwa shule duniani kote; na mimi nimezunguka kwelikweli duniani hapa; sijawahi kwenda shule nikakuta shule haina maabara haina maktaba, hiyo ni shule gani? Mimi sasa hivi Musoma vijini shule za msingi tatu nimeweza kujenga maktaba. Na watu wananishangaa, wanasema Profesa mbona unang’ang’ana shule ya msingi iwe na maktaba? Nikasema kama unaona watu hawaelewi ushibishane nao sana, inabidi ukae kimya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ninaomba wanaoshughulika na elimu wahakikishe kwamba kila shule ina maktaba. Maktaba kwa nini, kwa sasa hawatahitaji vitabu? lakini maktaba zile tunakoenda tutaweka kompyuta zenye capacity kubwa na spidi kubwa; hata vitabu vingine mnavyovinunua sasa hivi vinatolewa bure, sasa kama hauna hizo kompyuta ndiyo maana ya hizi library lazima ziwe na computer, hata kama vitabu ni vichache mno, kusudu waweze kupata vitabu vya bure ambavyo sasa hivi vinagawanywa duniani.

Mheshimiwa Spika, lazima shule iwe na maabara, sekondari zetu zote lazima ziwe na maabara, hilo ni tatizo. Kwa hiyo ninaomba hayo yarekebishwe hayo. Kingine ninachokuja sasa nije kwenye mambo ya juu, Profesa haya yanakuhusu wewe na wengine wengine, nije Elimu ya Juu kidogo, na nilishapendekeza hapa.

Mheshimiwa Spika, hiyo COSTECH tuliyonayo hata tukimwaga humo fedha muundo wake COSTECH imekuwa kama idara ya Wizara. COSTECH haipaswi kuwa hivyo, inapaswa kwanza jina la COSTECH libadilishwe, iitwe National Research and Innovation Foundation. Iweke mkazo kwenye utafiti na mambo ya ubunifu, halafu na yenyewe ianzishe kufanya rating ya wasomi. Unajua haiwezekani, Maprofesa hawalingani jamani, au ma-Dkt. wote hawalingani. Sasa kwa kuwa hatuna rating hakuna Profesa wa grade “A" Profesa wa grade D, hakuna Dkt. wa grade A, grade D, kila mtu anaruka tu na title. Mimi Profesa, mimi Dkt., sasa inabidi wengine wale halali wakae kimya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hii kazi hii ni lazima tuiachie National Research and Innovation Foundation na duniani kote foundations ndio zimefanya vizuri. Uende Marekani, uende South Africa, uende wapi na wanapata fedha wanakuwa na watu wengi, hapo mambo yetu yataenda vizuri.

Mheshimiwa Spika, nije kwenye vyuo vikuu, hapa ndio naomba Profesa aache legacy kwamba hiyo Wizara ilikaliwa na Profesa. Ni lazima ainge kwenye kila chuo, tatizo letu moja sasa hivi ndio maana ukichukua vyuo vya Tanzania, vyuo vya Tanzania vyote hakuna ambacho kiko kwenye kumi bora ndani ya Afrika, hatumo. Inamaanisha kwamba utafiti kwenye vyuo vyetu umeenda chini.

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri ni kwamba mimi bado napokea ripoti ya machapisho. Kila niki–check Tanzania naona hamna, tuko chini, hivyo, Mheshimiwa Profesa akae na Vice Chancellors wake, watu wameanzisha journals, majarida kwa sababu ya promotion na yatazidi kudidimiza elimu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, siku moja Mwalimu alitutembelea, nashukuru mimi nilisoma Dar es Salaam University, Chancellor alikuwa Nyerere, akaja pale alikuwa amezowea kuonana na wafanyakazi na mimi ndio nilikuwa naanza kazi. Akasimama mtu mmoja senior akasema Mwalimu hiki chuo kina upendeleo sana, mimi sijapandishwa cheo. Mimi sikujua Mwalimu anamfahamu vizuri kumbe alimpa scholarship kwenda kusoma Marekani. Kaongea kaongea Mwalimu akatujibu wote akasema, jamani mimi nilikuwa nadhani mtu anayekuwa profesa, ni kweli mnahakikisha kweli kweli kwamba uprofesa unamstahili, kama ni suala la mshahara si wapandishieni tu mishahara, lakini msiwape hizi titles kwa urahisi rahisi hivi.

Mheshimiwa Spika, sasa vyuo vyetu vimefikia hatua hata idara zimekuwa na journals, hizo ni just for promotion. Sasa Mheshimiwa Profesa nimsaidie najua anayafahamu,

atakavyokaa na Vice Chancellors wake atamwambia kila Vice Chancellor aje na journal za chuo chake. Wakikaa kwenye meza na wote wakae sehemu ambapo kuna internet au na nini, anamwambia anaanza ku–check journal yake moja baada ya nyingine. Ambazo hazifai, nyingi hazitafaa kwa sababu mimi nimeshazifanyia utafiti.

Mheshimiwa Spika, kuna kitu kinaitwa citation index (CI), wanaonisikiliza andikeni CI, Citation Index au kingine kinaitwa IP (Impact Factor). Citation Index maana yake ni kwamba hilo journal, hilo jarida unalolitumia ni wangapi wanafanya rejea zao, wanaofanya utafiti. Profesa Mkenda akikuta zina– impact factor ya 0.05 nitamwomba tuje tuongee, nadhani hazipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, narudia 0.05, Impact factor au Citation Index, inamaanisha hizi journal wanazozitumia duniani hazijulikani, kwa hiyo ni zetu tu hapo, backyard journals, lazima azipige vita Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, mwisho, kuna maeneo matatu ambayo lazima tuwekee mkazo na lazima vitu viunganike humu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Profesa muda wako umekwisha.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Spika, namalizia hako ka mwisho.

SPIKA: Nakuongezea dakika tatu umalizie.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tena unaona maprofesa waungwana, ahsante profesa. Ni hivi, jamani tulieni mtafanya anisimamishe, stop. Ni kwamba Profesa Mkenda kuna maeneo matatu lazima ayaanzishe akiwa kwenye hiyo Wizara, ni space science and technologies na hiyo ndio yanaingia mambo ya satellites na mambo ya nini. Lazima aanzishe research kubwa na elimu kubwa kwenye eneo la mbegu, seed science, lazima si tunataka kwenda kwenye kilimo? Hata hii space science ni kwenye kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwisho kuna ambalo ni kubwa, non- sciences, non-technologies hata wale wagonjwa wa TB duniani wameacha kutumia vidonge vingi siku hizi wanachukua kidonge size kama ya unywele inatibu TB, huko ndio dunia inakokwenda.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)